Ananipenda kweli?

tabasham

Member
Joined
Jan 16, 2014
Posts
66
Reaction score
19
Habari wana jf, hii mara yangu ya kwanza kupost kuomba ushauri na ninaomba ushirikiano.
Miezi miwili iliyopita nimekuwa na uhusiano na mwanaume ambaye anaonekana kunipenda na mimi ninampenda sanaaa.Tatizo ni kuwa mpenzi wangu nilimpata nikiwa na mahusiano na mtu mwingine ambaye nilimwacha baada ya kuona sina mapenzi nae ya kweli, huyu mpnz wangu nae alikuwa na mahusiano na mwingine,lakini hakuwahi kuachana nae japo hawakuwa na mawasiliano mazuri,zaidi ya yote ananiambia hana mpango nae ila msichana huwa anamtafuta mwanaume na kumtaka wakutane ila mwanaume anakataa ila hawezi kumwambia waachane,hofu yangu ni kuwa siku moja watarudiana maana hawajaachana. Siwezi kumwambia kwa lazima amuache ila naona anamuonea huruma kumwacha. Naombeni ushauri maana ninampenda na sitamani hata kumkosa yani, nahofia siku wakikutana watapendana upya.
 
Picha moja stelingi wawili umeona wapi? Kama anakupenda kweli hakikisha amepiga chini huo mpango mwingine.
 
Una hakika hawakutani?

Hapo amekuwezea kweli kweli.... Ni namna tu ya kukufanya usijisikie vibay zaidi ukijakuwagundua.. Hapo wanaendelea kama kawaida.
 
hapo sasa ni wewe kuwa na makeke kama kweli unahitaji kuwa na future nae... awezi fanya maamuzi ya kumwacha mpenzi wake kama ataona na wewe ni mzigo jitume deka mjali mpende akisha kaa kwenye mstari tulia sasa acha kazi kwake
 
hapo sasa ni wewe kuwa na makeke kama kweli unahitaji kuwa na future nae... awezi fanya maamuzi ya kumwacha mpenzi wake kama ataona na wewe ni mzigo jitume deka mjali mpende akisha kaa kwenye mstari tulia sasa acha kazi kwake

asante sana
 
tulizana vunja mtandao:kwa hisani ya watu wa marekani :usa2::usa2::usa2::usa2::usa2:
 
Una hakika hawakutani?

Hapo amekuwezea kweli kweli.... Ni namna tu ya kukufanya usijisikie vibay zaidi ukijakuwagundua.. Hapo wanaendelea kama kawaida.

sina uhakika ila ninamuamini tuu kwa asemayo
 
sina uhakika ila ninamuamini tuu kwa asemayo
Kati yako na yeye nani alimuanza mwenzie? ( kuanzisha mahusiano).

Maana kama ni yeye mwambie kwanini aanzishe uhusiano na wewe halafu ashindwe kuvunja uhusiano uliotangulia ana maana gani?

Kama ni wewe ndo ulianza basi jamaa bado yupo njia panda endelea kumbana aamue moja.
 
Habari yako dada mm ninachokushauri ni kwamba kwanza kaa nae na muongee kuhusu hali halisi ya mapenzi yenu na kila mmoja atoe ya moyoni bila hata kuja kuasilitiana ww umpe sababu za kuachana na mpz wako na yy akupe sababu za kutokuachana na hyo mpz wake kwani ww unampenda na yy anakupenda ni bora kila mtu awe mkweli kwa mwenzake!kwani hyu mpz wako unamuona anamsimamo gani na ww na hyu mpz wake ambae unasema kama una ws ws nae kama watakuja kurejeana na kuja kukuuumia moyo wako?
 
Mrembo,moyo wakupenda haupendi kusikia ukweli,lakini ivi kweli moyo wako unakubali kua na mtu mwengine wakati wewe pia ni mwanamke kama huyo anaeonewa huruma kuachwa? kwani yeye amezidi nini na wewe umepungua nini?
sikwambii muache au achana nae sababu moyo wako unamtaka lakini jiulize mpaka lini utakua nyuma ya mlango? yani akipiga cm yeye wewe ukae kimnya huna uhuru na mpenzi wako? ningekua wewe ningejitahidi kimapenzi zaidi na yakinishinda najipanga lakini kua na mwengine huku najua na eti hawezi kuondoka kwasababu eti anaunewa huruma,basi huyo bawana ana moyo kama bahari.....
 
hapo sasa ni wewe kuwa na makeke kama kweli unahitaji kuwa na future nae... awezi fanya maamuzi ya kumwacha mpenzi wake kama ataona na wewe ni mzigo jitume deka mjali mpende akisha kaa kwenye mstari tulia sasa acha kazi kwake
Wengine unapompenda,kudeka na kuwa na makeke ndiyo unazidi kumboa.
 
Yani umemuacha uliekuwa nae mara ya kwanza kisa umepata mwengine??, alafu ndio ukangudua kwamba hukumpenda??
Yani kama uliua kwa panga, basi utakufa kwa panga tu..
 
vumilia hivyo hivyo, kizuri kula na mwenzako
 
umemwongezea mshkaji option, inabid utafute taarifa za kiintelijensia za msimamo wa jamaa ukoje kwenye mahusiano, kama anajua anachotaka au la
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…