Anang'ang'ania watoto wangu

Anang'ang'ania watoto wangu

Nyrum

Senior Member
Joined
Aug 11, 2013
Posts
124
Reaction score
41
Habari wanajamvi, nadhani mambo yanaenda vyema.

Leo nimepata ugeni mdogo wangu mtoto wa mama mdogo kaja kunitembelea nyumbani kwangu.

Kanieleza tatizo lake nimeshndwa jinsi ya kumsaidia nikaona nijaribu kushare nanyi nipate chochote chakumsaidia.

Haya wandugu mkasa wenyewe upo hivi, bidada ni mfanyakazi muajiriwa katika kampuni fulani na ni mke wa mtu pia amebarikiwa kupata watoto watatu wote ni mapacha.

Sasa kabla hajaolewa alikuwa na boyfriend wake ambae kwa kipindi hicho alikuwa na maisha duni ukilinganisha na hali ya bibie na mumewe.

Wakati huo anadate na huyo jamaa pia wapo katika uchumba na mumewe, bibie akafunga ndoa after 1year akiwa tayari mjamzito.

Akajipatia hao twins wake watatu, mabinti wawili na njemba mmoja.

Huyo njemba kafanana sana na mumewe jambo ambalo shemu anafurahi sana.

Watoto mpaka sasa wana miaka minne, kasheshe limeibuka juzi, jamaa yule wa zamani anadai watoto ni wake na ukiangalia kwa mbali wanafanana, jamaa amekuwa mkali anataka watoto wake yaani amempa bidada siku mbili ampe jibu watoto ni wanani?

Mumewe anampenda sana na anajali sana family.

Anawapenda watoto wake hatari yaani walipozaliwa tu shemu aliomba likizo kazini ili alee watoto wake kwanza.

Sasa bibie amechanganykiwa hajui afanyeje na anamuogopa mumewe.

Hapo naomba tumsaidie mawazo.

Yupo humuhumu.

Nawasilisha.
 
Amwambie si watoto wake tena afanye hivyo bila woga, najua hapa kuna uwezekano wa kuishia kwenye DNA ili kuhakikisha ni yupi mwenye uhalali wa kuwaita hao watoto wa kwake. Mwambie asipepese ila ajue DNA hapa inanukia.
 
Hizi stori za uongo uongo zimeshamiri sana MMU.

Ngoja nisepe.
 
Ahsante mkuu, yani mambo haya basi tuu! Jamaa kataman tu mapacha huyu
 
Hivi inakuaje unakua na nahusiano na watu wawili na wote,Na wote unakutana nao bila kinga,kwanini kama umeamua Kuwa na wawili mmoja usitumie nae kinga,Ili kuepuka jakamoyo..sasa hapo ndugu yangu moja haikai mbili haikai .!!!
 
Kama yumo humu kwa nini asiandike yeye...

Tunataka kumuuliza maswali magumu ambayo wewe hutaweza kujibu...
 
Kuna watu wanatia hasira!!! Si alijua ataolewa soon hicho kiranga cha nin cha kuendeleza kampeni za pembeni???

Matatizo mengine tunajitakia sana kwan angejituliza ingekuaje... Kwan alivoolewa alitembea na nan ktk siku zake za hatar??? Yeye anamjua baba wa watoto amtaje sasa
 
Sipatii picha sura za hao watoto! Wamefanana na mume wa ndoa na pia wamefanana na mchepuko! Khaaa.....

Sent from my WhiteBerry using JamiiForums
 
Waende na mchepuko kupima DNA bila mume halali kujua wakikutwa ni wa huyo mchepuko bas ampe kiroho safi maana hata akijifanya mjanja siri itafichuka tu. Mwisho wa ubaya ni aibu....dhambi imekwisha kuchukua mimba kuificha ni ngumu
 
Sipatii picha sura za hao watoto! Wamefanana na mume wa ndoa na pia wamefanana na mchepuko! Khaaa.....

Sent from my WhiteBerry using JamiiForums

Teh
upande mume upande mchepuko!!!!
 
Miaka 4 yote alikuwa wapi kudai hao watoto? Alingoja kazi ngumu imeisha ndio aanze kudai watoto?
Kuna maswali ambayo unapaswa kuyajibu kwanza.
Je, mume anajua kuwa mkewe alikuwa na huyo boyfriend kabla hawajaoana? Kama anajua na hana tatizo na ukweli huo amueleze kuhusu hayo madai ya huyo mwanaume kuhusu watoto ili wao ndio wapambane.
Swali tena, huo mchepuko wa zamani umeoa? Kama ana mke basi amwambie suala hilo anapaswa kumshirimisha mkewe maana mwisho wa yote yeye ndiye atakayelea watoto hao kama jamaa atawachukua na sio kulelewa na bibi au shangazi.
Mwisho naona hili suala ni gumu sana na huenda lengo lake sio watoto bali kuvuruga tu ndoa kwa sababu ya wivu. Yeye asimame imara adai ishahidi kama wa huyo mwanaume au la.
 
Hivi inakuaje unakua na nahusiano na watu wawili na wote,Na wote unakutana nao bila kinga,kwanini kama umeamua Kuwa na wawili mmoja usitumie nae kinga,Ili kuepuka jakamoyo..sasa hapo ndugu yangu moja haikai mbili haikai .!!!

Nashangaa!
 
Back
Top Bottom