Analazimisha awajue ndugu zangu.

Analazimisha awajue ndugu zangu.

Mr mgeni

JF-Expert Member
Joined
Apr 27, 2014
Posts
1,222
Reaction score
810
Habari za mda huu,
Nipo kwenye mahusiano na binti mmoja wa hapa mjini yapata miezi 3,cha ajabu anataka nikamtambulishe nyumbani kwetu,eti mama,baba na ndugu zangu wamjue.Najiuliza sipati jibu mbona ni mapema sana anakua na kisebusebu na ana kiherehere balaa nikiongea tu na simu kama hata ni na mama nae akiwemo hapo anadakia sim anataka aongee nae.Tabia yake inanikera sana namvumilia tu,Sasa sijui ndo upendo wa dhati au anataka kunisolola tu.Au ndo tabia zenu wakina dada ya kutaka kujulikana ukweni haraka?Nijuzeni basi nijue.
 
Sikia Brother ,, Ukitaka kumpima mwanamke nikatika Upendo wake Wa kwatu ,raafiki ndugu jamaaa.

Hata km anafake utajua hii niyakufake au lah ....Mpende uyo mwanamke !!.
 
Ninyi ni wale mama zenu wanawauliza kama mna demu mnakataa. Shenzi kabisa
 
Mzee baba huyo ana hamu ya harusi kuliko ndoa hakufai mpe muda wa maangalizi.
 
Nyie viumbe hamna jema kabisa mkipendwa mnalalamika hivi huwa mnataka ninii kama hapo unaona kama usumbufu huwa hamjui ninii mnataka
ni mapema mno asubiri nimfanyie uchunguzi wa kutosha
 
mpende sana huyo mwanamke shauri yako... vuruga uone nilikuwa namaanisha nini..!!!
 
Huyo dada ni wa kuhurumiwa sana kwani anapoteza muda wake bure.
 
Ukimtongoza na mkiwa mnaongea unamuambia nini!??
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom