Mimi naitwa Halima ni msichana wa miaka 19 Nasoma kidato cha tatu (form 3) hapa Arusha.... nimejitokeza kwenu kuomba ushauri
Mimi nina mpenzi wangu ambae yupo chuo kikuu, ana miaka 25... kutokana na upendo anaonionyesha sitamani tena kuendelea na shule... kwani nikiwa darasani muda wote namuwaza yeye tu
Nilicho penda kutoka kwa huyu BOYFRIEND wangu ni kua ananijali sana na ana pesa kwan kwao wanajiweza kifedha... ananionga sana PESA kwani nikitaka hela ya CHIPS KUKU hua ananipa, hela ya lotion, pafyumu na saloon hua ananipa kila mwezi kwahiyo sina shida na shule wala sioni umuhimu wa shule.
NAOMBENI ushauri wenu jamani.. niwaambie nini WAZAZI wangu ili wanikubalie niache SHULE ili niolewe na huyu MWANAUME nifaidi pesa zake na mali za nyumbani kwao