Mkuu wa Mkoa wa Dar, Amos Makala umetoa matamko sana tangia ule kiapo cha kuwa Mkuu wa Mkoa, cha ajabu hakuna linalotekelezwa hata moja
1) Ulianza na machinga ukachimba biti weeeh mwisho siku hakuna lililotekelezwa.
2) Ukaenda kukagua mradi wa mwendo kasi Mbagala ukachimba biti ukatoa siku 3 wananchi watoke kupisha ujenze ila wananchi wamekugomea huko Mbagala.
3) Umetoa tamko la kuvaa barakoa na kukaa level seat kwenye vyombo vya usafiri lakini hakuna lililotekelezwa.
Mkuu wa Mkoa Amos Makalla unafeli wapi? Jitathimini kwanza kabla ya kutoa matamko ama sivyo itaonekana Hayati alikupiga benchi sio kwa bahati mbaya.