Amos Makalla awe mfano wa kuigwa katika ubunifu wa kusikiliza na kutatua kero za Wananchi

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Jul 28, 2022
15,305
9,734
Ndugu zangu Watanzania,

Nimefurahishwa na Habari niliyoisoma katika Gazeti la Mwananchi,likielezea utaratibu ambao mkuu wa mkoa wa Mwanza mh Amos Makalla amekuja nao na kuuzindua katika kuwafikia wananchi wenye kero na changamoto mbalimbali kwa jina la Ongea Live na mkuu wa Mkoa. Ambapo katika wazo hilo ni kuwa mh mkuu wa mkoa Anatoka ofisini na kwenda kuzungumza na wananchi kwa kuwasikiliza kero zao wilayani huko kutoka ngazi ya mkoa na kuzitatua kwa kutoa majibu. huku akiwataka wakuu wake wa wilaya kufika hadi ngazi ya kata.

Kwa utaratibu huu ni kuwa mkuu wa mkoa kwa kushirikiana na wakuu wake wa wilaya wanakwenda kuwafikia wananchi wenye kero mbalimbali hadi ngazi za mitaa,hali ambayo itapunguza na kuondoa changamoto nakero sugu za wananchi ambao wamekuwa wakihangaika na kuhangaishwa na baadhi ya watumishi wa umma ambao wanakuwa siyo wasikivu kwa wananchi,maana hapa ni lazima RC ama DC atoe maelekezo ya utekelezaji wa chochote atakachokibaini.

Utaratibu huu unakwenda kupunguza hata mabango yanayojitokeza wakati wa ziara za viongozi wetu wakuu yaani Rais ,makamu wa Rais pamoja na Waziri Mkuu. Kwa kuwa kero nyingi za wananchi zitakuwa zinamalizwa na ma RC na DC na zile zilizo inje ya uwezo wao watakuwa wanatafuta namna yakuwasiliana na ngazi za juu ikiwepo wizara ili kupata ufumbuzi.

Utaratibu huu ukifanywa na wakuu wa mikoa na wilaya nchi nzima kwa hakika italeta matumaini makubwa sana na kupunguza kero mbalimbali za wananchi. itaondoa adha na machungu ya watanzania kuporwa haki zao,kuonewa,kutosikilizwa na baadhi ya watumishi na kukosa mahali pa kukimbilia, Italeta Tabasamu kwa wajane,yatima na wazee wanaokuwa wameonewa au kunyanyaswa na wenye nguvu na itawasaidia wanyonge kupata haki zao.

Rai yangu na ushauri wangu kwa mh Amos Makalla na wengine pia Ni kuwa katika utaratibu huu mzuri ahakikishe kuwa anafuatilia utekelezaji wa maagizo anayokuwa ameyatoa pindi anapopokea kero ya mwananchi, kuhakikisha kuwa kama mwananchi anatakiwa kupata haki yake na akatoa maagizo ya kushughulikia kero hiyo ,basi awe na utaratibu wa kuhakikisha kuwa anapewa mrejesho wa kimaandishi na kinyaraka juu ya utekelezaji wa maagizo yake. Ili wananchi wapate haki. Kwa kuwa kuna baadhi ya watumishi anaweza akapewa maagizo ya utekelezaji halafu akafanya upuuziaji wa maelekezo ,hivyo ni vyema kwa mkuu wa mkoa na wilaya kuagiza kupewa mrejesho wa kimaandishi wa namna maelekezo na maagizo yake yalivyo tekelezwa.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge.

Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Nimefurahishwa na Habari niliyoisoma katika Gazeti la Mwananchi,likielezea utaratibu ambao mkuu wa mkoa wa Mwanza mh Amos Makalla amekuja nao na kuuzindua katika kuwafikia wananchi wenye kero na changamoto mbalimbali kwa jina la Ongea Live na mkuu wa Mkoa. Ambapo katika wazo hilo ni kuwa mh mkuu wa mkoa Anatoka ofisini na kwenda kuzungumza na wananchi kwa kuwasikiliza kero zao wilayani huko kutoka ngazi ya mkoa na kuzitatua kwa kutoa majibu. huku akiwataka wakuu wake wa wilaya kufika hadi ngazi ya kata.
Anasikiliza kero zipi wakati alikuwa na mkakati wa kuwapa kero wakazi wa Dar ati abiria wote washukie Magufuli wapande pikipiki na bajabi zake
 
Anasikiliza kero zipi wakati alikuwa na mkakati wa kuwapa kero wakazi wa Dar ati abiria wote washukie Magufuli wapande pikipiki na bajabi zake
Soma mada uone kama nimezungumzia habari za stendi ya Dar. Kwa sasa Ni mkuu wa mkoa wa Mwanza.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Nimefurahishwa na Habari niliyoisoma katika Gazeti la Mwananchi,likielezea utaratibu ambao mkuu wa mkoa wa Mwanza mh Amos Makalla amekuja nao na kuuzindua katika kuwafikia wananchi wenye kero na changamoto mbalimbali kwa jina la Ongea Live na mkuu wa Mkoa. Ambapo katika wazo hilo ni kuwa mh mkuu wa mkoa Anatoka ofisini na kwenda kuzungumza na wananchi kwa kuwasikiliza kero zao wilayani huko kutoka ngazi ya mkoa na kuzitatua kwa kutoa majibu. huku akiwataka wakuu wake wa wilaya kufika hadi ngazi ya kata.

Kwa utaratibu huu ni kuwa mkuu wa mkoa kwa kushirikiana na wakuu wake wa wilaya wanakwenda kuwafikia wananchi wenye kero mbalimbali hadi ngazi za mitaa,hali ambayo itapunguza na kuondoa changamoto nakero sugu za wananchi ambao wamekuwa wakihangaika na kuhangaishwa na baadhi ya watumishi wa umma ambao wanakuwa siyo wasikivu kwa wananchi,maana hapa ni lazima RC ama DC atoe maelekezo ya utekelezaji wa chochote atakachokibaini.

Utaratibu huu unakwenda kupunguza hata mabango yanayojitokeza wakati wa ziara za viongozi wetu wakuu yaani Rais ,makamu wa Rais pamoja na Waziri Mkuu. Kwa kuwa kero nyingi za wananchi zitakuwa zinamalizwa na ma RC na DC na zile zilizo inje ya uwezo wao watakuwa wanatafuta namna yakuwasiliana na ngazi za juu ikiwepo wizara ili kupata ufumbuzi.

Utaratibu huu ukifanywa na wakuu wa mikoa na wilaya nchi nzima kwa hakika italeta matumaini makubwa sana na kupunguza kero mbalimbali za wananchi. itaondoa adha na machungu ya watanzania kuporwa haki zao,kuonewa,kutosikilizwa na baadhi ya watumishi na kukosa mahali pa kukimbilia, Italeta Tabasamu kwa wajane,yatima na wazee wanaokuwa wameonewa au kunyanyaswa na wenye nguvu na itawasaidia wanyonge kupata haki zao.

Rai yangu na ushauri wangu kwa mh Amos Makalla na wengine pia Ni kuwa katika utaratibu huu mzuri ahakikishe kuwa anafuatilia utekelezaji wa maagizo anayokuwa ameyatoa pindi anapopokea kero ya mwananchi, kuhakikisha kuwa kama mwananchi anatakiwa kupata haki yake na akatoa maagizo ya kushughulikia kero hiyo ,basi awe na utaratibu wa kuhakikisha kuwa anapewa mrejesho wa kimaandishi na kinyaraka juu ya utekelezaji wa maagizo yake. Ili wananchi wapate haki. Kwa kuwa kuna baadhi ya watumishi anaweza akapewa maagizo ya utekelezaji halafu akafanya upuuziaji wa maelekezo ,hivyo ni vyema kwa mkuu wa mkoa na wilaya kuagiza kupewa mrejesho wa kimaandishi wa namna maelekezo na maagizo yake yalivyo tekelezwa.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge.

Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
Fanya kazi acha kusifu ujinga ili ubebwe.

Pale EPZA alifungua pagale la hosptl ambayo haijaisha hadi leo, majengo yapo chini ya kiwango na kituo cha polisi hakijahamishwa ili kupisha uendelezaji wa hosptil

Na aliyajua hayo kabla ya ufunguzi wake. Majengo yamekaa tu hayatumiwi na hayajamalizika
 
Fanya kazi acha kusifu ujinga ili ubebwe.

Pale EPZA alifungua pagale la hosptl ambayo haijaisha, majengo chino yabkiwango na kituo cha polisi hakijahamishwa ili kupisha uendelezaji.

Na aliyajua hayo kabla ya ufunguzi wake
Kama kuna ubadhirifu wa fedha za umma na uzembe basi nakuhakikishia hatua kali zitachukuliwa kwa wahusika.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Nimefurahishwa na Habari niliyoisoma katika Gazeti la Mwananchi,likielezea utaratibu ambao mkuu wa mkoa wa Mwanza mh Amos Makalla amekuja nao na kuuzindua katika kuwafikia wananchi wenye kero na changamoto mbalimbali kwa jina la Ongea Live na mkuu wa Mkoa. Ambapo katika wazo hilo ni kuwa mh mkuu wa mkoa Anatoka ofisini na kwenda

0742-676627.
Hakuna mzalendo anayeshabikia matapeli. Ni mashetani ndiyo yapo hivyo. Mungua chukua huyu shetani haraka
 
Ndugu zangu Watanzania,

Nimefurahishwa na Habari niliyoisoma katika Gazeti la Mwananchi,likielezea utaratibu ambao mkuu wa mkoa wa Mwanza mh Amos Makalla amekuja nao na kuuzindua katika kuwafikia wananchi wenye kero na changamoto mbalimbali kwa jina la Ongea Live na mkuu wa Mkoa. Ambapo katika wazo hilo ni kuwa mh mkuu wa mkoa Anatoka ofisini na kwenda

Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
Ata naye ata pungua tu hii inshuu ni political wiling toka huu hadi chini kabisa haiwezi chipuka katikati ila dumu
 
Back
Top Bottom