Amiri Jeshi Mkuu mlemavu wa miguu

Amiri Jeshi Mkuu mlemavu wa miguu

kibaizi kiki

Senior Member
Joined
Dec 23, 2012
Posts
160
Reaction score
39
Natambua katiba ya nchi ya sasa na hata rasimu ya pili ya katiba inatambua kuwa rais wa nchi ndiye atakua amiri jeshi mkuu. Na moja wapo ya matukio baada ya kuapishwa rais na katika matukio mengi ya kitaifa rais ukagua goalie la majeshi yake yote.

Naomba wana JF mnisaidie kunielimisha juu ya hili. Hivi kama rais ni mlemavu wa miguu anawezaje kukagua gwalide la majeshi yake? Je aweza kutembezwa kwa wheelchair? Au mlemavu hawezi kuwa amiri jeshi mkuu? Naomba kujua
 
Kwani unadhani rais wa marekani aliyepinganisha vita ya pili ya dunia alikuwa anatembelea miguu?.
Frankling Rooselvet alikua anatembelea wheelchair(mlemavu miguu yote).
 
Sina uhakika kama rais wa USA ndie pia amiri jeshi mkuu
 
Cha msingi kama ulemavu wake haumzuii kufanya shughuli za rais kama kiongozi wa nchi na amiri jeshi mkuu then anaweza kukagua gwaride la jeshi kwa wheel chair
 
Putin anakagua gwaride akiwa kwenye jeep,hata kibaki ajili ya umri nilishamuona anakagua gwaride akiwa juu ya gari la wazi.
 
wetu huyu anaanguka anguka sana majukwaani
 
Back
Top Bottom