Umesoma vzr.. Umepata kazi nzuri.. Ila unataka kuaribu mwishoni kabisa. Haijalishi umesoma vzr kiasi gan au una Kazi nzuri kiasi gani lakini ukikosea ktk kuchagua mpenzi, hivyo vyote ulivyonavyo havina maana yoyote. Ndoa ni mtihani wa mwisho ktk maisha. Na unapaswa kufaulu vzr ili usipate Bashite (Zero) ktk Maisha yako ya Baadae. Huyo binti sio kwamba alilazimishwa kuolewa, ila aliona ww wakati ule ulikuwa bado mwanafunzi kwa hiyo ungempotezea sana muda. Na amerudi tena kwako kwa sababu alivyovitegemea kwa mume wake amevikosa. Anatagemea kupata vitu hivyo kwako na ikiwa hatavikosa tena kwako bhasi ataendelea kuvitafuta kwa wengine. Na ushajiuliza.. Kuwa ndoa yake ingekua yenye mafanikio unafikiri angerud kwako tena? Asingerudi my young brother. Huyo anatafuta Hifadhi kwako wala hakupendi, kama kweli alikuwa anakupenda asingekubali kuolewa na mtu mwengine. Mdogo wangu ww n kijana mdogo, ndoa sio kitu cha mchezo mchezo.. Tuliza akiri fanya maamuzi sahihi. Huyo mpumbavu achana nae