Ameacha kutumia supplements za ujauzito

Ameacha kutumia supplements za ujauzito

BABA TUPAC

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2015
Posts
1,533
Reaction score
3,837
Wakuu,

Mchumba wangu ni mjamzito, ujauzito wake wa una umri wa miezi minne. Yeye yupo Mwanza, mimi nipo Arusha.

Alipoanza kwenda clinic alipewa dawa za kuanza kutumia kwaajili ya madini na madini, ambazo zinakuwa 30 (ambao wameshakuwa wajawazito nadhani wanazifahamu) jina lake limenitoka kidogo.

Sasa leo nimemuuliza hivi zile dawa ulizimaliza? akanijibu kuwa kuna mwenzake wa ofisini alimshauri aache kutumia dawa maana dawa si nzuri, kwahyo alikuwa nusu na nusu aliacha. Niliumia sana kitendo cha yeye kufanya maamuzi yanayohusu mtoto wetu peke yake bila kunishirikisha.

Huyo mwenzake amemshauri kuwa aache dawa na awe anakula samaki au dagaa na mchicha au matembele. Naombeni mnisaidie mambo yafuatayo:

1. Kuna athari zipi mama au mtoto anaweza kuzipata endapo hizo dawa hazitanywewa au kumaliziwa dozi?
2. Kwa amekatisha hiyo dozi karibia mwezi mmoja uliopita, je anaweza kumalizia zile dawa zilizobaki kwasasahivi au kwakuwa alishakatisha dozi inatakiwa aanze upya?
3. Mna lipi na kulishauri zaidi kuhusiana na swala hili?

MWISHO, kina mama msifanye maamuzi yoyote yale kuhusu ujauzito au mtoto peke yako, fanya na mwenzio, msipende sana kusikiliza tu maneno ya saloon na maofisini bila ushauri. Mtoto ni wenu wote, likitokea tatizo lolote wote mnawajibika. Inauma sana, namuonea huruma sana mwanangu na yeye pia mchumba wangu kama kuna athari zozote wanaweza pata

Naombeni sana mnishauri wakuu
 
Jaribu kuongea nae na umshauri asikilize ushauri wa wataalam na sio maneno ya nje..

Hawezi kujua hizo dawa zitamsaidia vipi yeye na hicho kiumbe kilichopo tumboni mwake.. Hivyo vyakula alivyoshauriwa kula sio vibaya ndio ila Na hizo dawa pia azitumie...labda tu kama zinamletea maudhi ya pembeni (side effects)
 
Nilikuwa sivimezi sababu ya harufu yake mbaya ilinipelekea kuzidi kutapika, lkn mbadala wake ni ivyo vyakula rafiki alivyomwambia
 
Inategemea hizo dawa amepewa kwaajili ya nini... but nachokumbuka huwa wanapewa dawa za kuzuia mama mjamzito kupata malaria (SP), minyoo (mebendazole) pamoja na za kuzuia upungufu wa damu (folic na ferrous)

kila dawa hutolewa kwa malengo yake na maana zake...
Mwambie afuate ushauri na matibabu ya wataalamu
 
Kumbe wanameza dawa?kazi kweli kweli

Ila huo ushauri wa chini mzuri
 
Sema aina ya dawa alizopewa upate ushauri mzuri zaidi ya hapo tutakuwa tunakudanganya tuu.
 
A
Jaribu kuongea nae na umshauri asikilize ushauri wa wataalam na sio maneno ya nje..

Hawezi kujua hizo dawa zitamsaidia vipi yeye na hicho kiumbe kilichopo tumboni mwake.. Hivyo vyakula alivyoshauriwa kula sio vibaya ndio ila Na hizo dawa pia azitumie...labda tu kama zinamletea maudhi ya pembeni (side effects)
Asante mkuu
 
Nilikuwa sivimezi sababu ya harufu yake mbaya ilinipelekea kuzidi kutapika, lkn mbadala wake ni ivyo vyakula rafiki alivyomwambia
Mtoto alipozaliwa hakuwa na tatizo lolote linahusiana na kutokutumia hizo dawa? uliacha baada ya kutumia kwa mda gani?
 
Mtoto alipozaliwa hakuwa na tatizo lolote linahusiana na kutokutumia hizo dawa? uliacha baada ya kutumia kwa mda gani?
Nina watoto watatu na nilikuwaga nameza km siku tatu tu naacha nilijitahidi kula mboga za majani samaki dagaa na kubywa maji kwa wingi, bila kusahau juice ya matunda yan natural sio ya kwenye makopo, na watoto niliwazaa fureshi kabisa
 
Hizo dawa ni folic acid kwa ajiri ya kuzui Neuro tube defects ( vichwa vikubwa, mgongo wazi etc) mara nyingi zinatakiwa zitumike miez mi3 ya mwanzo japo si lazima sana kama mama atakuwa hana upungufu wa hayo madini....nchi za walioendelea huwa wanatumia kabla hata ya kushika ujauzito pindi mama anapotaka kushika mimba...hivo cha msingi wee subiria tu mtoto azaliwe atakuwa fresh tu
 
Kama hushirikishwi kuhusu mtoto jua kuna mwingine anapewa updates daily. Hao ndo wanawake wa kibongo. Ukikana ujauzito wanalia lia ukikubali kuna baba kijacho mwingine nae analea. Yamenikuta, chunguza tena.
 
Wakuu,

Mchumba wangu ni mjamzito, ujauzito wake wa una umri wa miezi minne. Yeye yupo Mwanza, mimi nipo Arusha.

Alipoanza kwenda clinic alipewa dawa za kuanza kutumia kwaajili ya madini na madini, ambazo zinakuwa 30 (ambao wameshakuwa wajawazito nadhani wanazifahamu) jina lake limenitoka kidogo.

Sasa leo nimemuuliza hivi zile dawa ulizimaliza? akanijibu kuwa kuna mwenzake wa ofisini alimshauri aache kutumia dawa maana dawa si nzuri, kwahyo alikuwa nusu na nusu aliacha. Niliumia sana kitendo cha yeye kufanya maamuzi yanayohusu mtoto wetu peke yake bila kunishirikisha.

Huyo mwenzake amemshauri kuwa aache dawa na awe anakula samaki au dagaa na mchicha au matembele. Naombeni mnisaidie mambo yafuatayo:

1. Kuna athari zipi mama au mtoto anaweza kuzipata endapo hizo dawa hazitanywewa au kumaliziwa dozi?
2. Kwa amekatisha hiyo dozi karibia mwezi mmoja uliopita, je anaweza kumalizia zile dawa zilizobaki kwasasahivi au kwakuwa alishakatisha dozi inatakiwa aanze upya?
3. Mna lipi na kulishauri zaidi kuhusiana na swala hili?

MWISHO, kina mama msifanye maamuzi yoyote yale kuhusu ujauzito au mtoto peke yako, fanya na mwenzio, msipende sana kusikiliza tu maneno ya saloon na maofisini bila ushauri. Mtoto ni wenu wote, likitokea tatizo lolote wote mnawajibika. Inauma sana, namuonea huruma sana mwanangu na yeye pia mchumba wangu kama kuna athari zozote wanaweza pata

Naombeni sana mnishauri wakuu
Mm binafsi sikuwahi kutumia dawa yoyote zaidi ya SP ambazo unapewa na unatakiwa uzimeze papo kwa papo kama huna maji utaambiwa ukanunue ila kuna rafiki yangu alikuwa mjamzito akanambia kapewa hizo dawa nikamuuliza za nn? Akasema kama ww ulivyosema nikamshangaa coz mm binafsi sijawahi tumia dawa hizo na nilijifungua salama na mtoto yuko salama tu ila baadae ya kufuatilia nikagundua mama mjamzito anayehudhuria clinic private hospital ndio huwa wanapewa dawa hizo sasa cjui huwa zinasaidia nn
 
Dawa dawa dawa...ale vzr na mtoto atatoka vizuri...nani kakwambia dawa zinasaidia zaidi ya kuongeza matatizo tu
 
Dawa dawa dawa...ale vzr na mtoto atatoka vizuri...nani kakwambia dawa zinasaidia zaidi ya kuongeza matatizo tu
nawasikitikia watu kama wewe, ndio huwa mnawashauri wenzenu vibaya.
Btw mjamzito anaweza asitumie hayo madawa na asipate tatizo lolote akajigungua vizuri kabisa tena mtoto mwenye afya.
Ila akitumia hizo dawa, zinaongeza ukakika wa mtoto kuwa salama na afya nzuri.
Msidharau ushauri wanaotoa wataalamu, sio wajinga kuamua kutoa hizo dawa, tena dawa zenyewe zinatolewa bure sijui zingeuzwa ingekuwaje
 
Ni vizuri mama mjamzito kutumia dawa kadri anavoelekezwa clinic maana watu hawafanani kama wewe hukupata tatizo ulivoacha kumeza haimaniishi na mama k unayemshauri asitumie itakua hivo tusaidiane kupunguzza vifo vya akina mama tusipotoshane
 
N kweli kila mama anatofauti zake kipindi cha ujauzito, na pia kama hatumii hizo dawa basi ajitahidi kila mwez kupima pressure na wingi wa damu, mengine muombe Mungu amuepushie
 
Dawa zinachosha nilipewa folic acid na ferrous kwa ajili ya damu nilizitupia huko baada ya kutumia mwezi.... nikakazania kunywa maji ya matembele na rozella so haikuleta shida.

Muambie ajitahidi tu kula mboga za kuongeza damu
 
Back
Top Bottom