‘Amani ikitoweka tunawapeleka viongozi CCM ICC’

‘Amani ikitoweka tunawapeleka viongozi CCM ICC’

nngu007

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2010
Posts
15,860
Reaction score
5,803
Na Daniel Mjema,Mwananchi

Posted Jumatano,Aprili10 2013 saa 15:1 PM

Chadema inadai wapandaji wa mbegu ya udini ni CCM

Moshi. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema iwapo amani itatoweka kutokana na vurugu za kidini, watawashtaki viongozi wa CCM Mahakama ya Kimataifa ya The Heague.

Kauli hiyo ilitolewa mwishoni mwa wiki iliyopita na Mwenyekiti wa Chadema Manispaa ya Moshi, Jaffar Michael wakati akimkaribisha Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo kuhutubia mkutano wa hadhara.

Michael ambaye pia ni Meya wa Manispaa ya Moshi, alisema baadhi ya viongozi wa Serikali ya CCM ndiyo kiini cha mbegu za chuki za kidini, walipoituhumu Chadema kuwa ni chama cha kidini.

“Nataka niwaambie leo, amani ya Tanzania ikivurugika tunawapeleka viongozi wote wa Serikali ya CCM The Heague, wao ndiyo chanzo cha chuki hizi za udini ambazo zinaligawanya taifa,” alisema Michael.
 

Oh WOW Hii Kali Kweli; Hiyo KESI ITAKUWA PALE ARUSHA au THE HAGUE?

Sababu sisi wengine hatuli NYAMA za MASHINE...
 



Sababu sisi wengine hatuli NYAMA za MASHINE...
Umepost habari nzuri sana inayojieleza lakini hii hapa ni nini, (Nyama za mashine na kesi ya the Hague) na ina lengo na kazi gani katika habari ulipost? inahusianaje na post yako?
 
Umepost habari nzuri sana inayojieleza lakini hii hapa ni nini, (Nyama za mashine na kesi ya the Hague) na ina lengo na kazi gani katika habari ulipost? inahusianaje na post yako?

Oh kwasababu in EUROPE Machine ndio zinachinja wanyama na sio Human; Wanasema watapeleka kesi ICC Makao Makuu yapo THE HAGUE - Uholanzi... Lakini Arusha wanataka iwe Ofisi ndogo ya Mahakama ya DUNIA... Sasa kama issue ni ya Tanzania sijui kama wataruhusu Mahakama kuwa ARUSHA; Sababu Kesi ya akina Uhuru na Ruto Mashahidi waligoma kwenda Arusha kutoa Ushahidi kwa kusema ni Karibu sana na Kenya...
 
hivi hadi sasa Amani haijatoweka? polisi wanaua raia wasio na silaha rejea Arusha, Songea Morogoro, Mwangosi (r.i.p comrade) watu wanatekwa na kuteswa rejea Ulimboka, Kibanda etc?Kama in ICC wanatakiwa sasa hivi tusisubiri hadi vita kamili ianze watu wafe then baada ya vifo ndio tuanze kuwapeleka ICC, the sooner the better!
 
Back
Top Bottom