Melki the Storyteller
JF-Expert Member
- May 3, 2022
- 5,701
- 9,779
Hivi ilishawahi kukutana na ile situation umekutana na mwanamke barabarani, kila unapojaribu kuzungumza naye, yeye haoneshi attention yoyote ya kuzungumza ama kuvutiwa na wewe! imani yangu watu wa namna hiyo ni wachache kukuta anapewa details sahihi na mwanamke huyo! just imagine unamwongelesha ilhali yeye amenuna na anaendelea na mawazo ya mishe zake kama kawaida!
Siku ya leo nimeshuhudia kisa cha tofauti kidogo!
Wakati wa asubuhi nikiwa naelekea kwenye shughuli za hapa na pale ili kupata pesa kwa ajili ya mahitaji ya familia na mafuta nilikuwa sambamba na mwanadada ambaye alikuwa mbele yangu. Ghafla bodaboda mmoja tokea nyuma yangu akasogea mpaka mahali mwanadada alipo kisha kumuomba yule mwanadada apande ili ampe lift! mwanadada yule akakataa japo alikuwa akitabasamu!
Bodaboda yule ndo kujipa imani kuwa hakuna mkate mgumu mbele ya chai kwamba mwanadada yule hataki kujionesha kuwa yeye ni maharage ya mbeya ya maji jagi moja.
Waliendelea kujibizana story za hapa na pale huku wakitabasamu! Muda huo mwanadada akiwa anatembea kwa miguu na huyu bodaboda akiwa analazimisha pikipiki yake kwenda taratibu mithili ya mwendo wa kobe mchafu! Wakati wametembea umbali mrefu kidogo, bodaboda kajikuta akiteleza na kiangukia kwenye mtaro ulio pembezoni kufuata ile barabara! tena mtaro wenye matope mazito kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.
Yule mwanadada, alipoteza sura yake ya kutabasamu! na kuweka sura ya kazi! alitazama mbele aendako! hakudiriki kutazama pembezoni kuona kama mwangukaji kaangukia kiuno ama dushe! akatembea mbele kwa mwendo wa jeshi huku akiziseti nywele zake zilizokuwa zikishikwa na yule bodaboda aliyekosa kazi.
Ndipo nilipofika eneo la tukio, pamoja na watu wengine ili kuiopoa pikipiki yake! Hajaumia sana lakini.
Dada wa watu aliishilia na kutokomea kusikojulikana.
Ama kweli, Mapenzi yana wenyewe! Hakuambulia hata namba ya simu!!
Siku ya leo nimeshuhudia kisa cha tofauti kidogo!
Wakati wa asubuhi nikiwa naelekea kwenye shughuli za hapa na pale ili kupata pesa kwa ajili ya mahitaji ya familia na mafuta nilikuwa sambamba na mwanadada ambaye alikuwa mbele yangu. Ghafla bodaboda mmoja tokea nyuma yangu akasogea mpaka mahali mwanadada alipo kisha kumuomba yule mwanadada apande ili ampe lift! mwanadada yule akakataa japo alikuwa akitabasamu!
Bodaboda yule ndo kujipa imani kuwa hakuna mkate mgumu mbele ya chai kwamba mwanadada yule hataki kujionesha kuwa yeye ni maharage ya mbeya ya maji jagi moja.
Waliendelea kujibizana story za hapa na pale huku wakitabasamu! Muda huo mwanadada akiwa anatembea kwa miguu na huyu bodaboda akiwa analazimisha pikipiki yake kwenda taratibu mithili ya mwendo wa kobe mchafu! Wakati wametembea umbali mrefu kidogo, bodaboda kajikuta akiteleza na kiangukia kwenye mtaro ulio pembezoni kufuata ile barabara! tena mtaro wenye matope mazito kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.
Yule mwanadada, alipoteza sura yake ya kutabasamu! na kuweka sura ya kazi! alitazama mbele aendako! hakudiriki kutazama pembezoni kuona kama mwangukaji kaangukia kiuno ama dushe! akatembea mbele kwa mwendo wa jeshi huku akiziseti nywele zake zilizokuwa zikishikwa na yule bodaboda aliyekosa kazi.
Ndipo nilipofika eneo la tukio, pamoja na watu wengine ili kuiopoa pikipiki yake! Hajaumia sana lakini.
Dada wa watu aliishilia na kutokomea kusikojulikana.
Ama kweli, Mapenzi yana wenyewe! Hakuambulia hata namba ya simu!!