Ama kweli majuto ni mjukuu..

Ama kweli majuto ni mjukuu..

Hakuna nidhamu kwenye laki 3 mkuu, nidhamu ya hiyo senti ni kula tu. Ukiipa nidhamu senti yako hiyo utakufa na njaa.

Nidhamu inayojadiliwa hapa ni fedha (siyo senti), yaani kipato cha mamilioni kwa mwezi (mil 2, 3, .....).
Mkuu hiyo ni ishara kwamba nidhamu yako ni ndogo sana, unadharau laki 300000? wewe kweli hamnazo
 
Pesa huwa zinatufanya tunajisahau sana.. hasa hela za dili za chap chap! Wewe sio wa kwanza ukija kuzipata tena utarudia ujinga uliokuwa unafanya...

Mi kuna kipindi nilikuwa sikosi mil 3 mpaka 5 kwa mwezi.. nikaona maisha si ndo haya.. nikaanza kuwaza magari na simu za bei kali, saiz nataman hata ningenunua viwanja kila mwezi au ningesimamisha hata kajumba kadogo...

Lakini si mbaya baada ya msoto wa miezi kadhaa saiz nimeanza kurudi kwenye form!!
Kwahiyo hata kajumba hukubahatika kupata mkuu?
 
Bila nidhamu ya pesa kwenye haya maisha,lazima kuna siku lazima utakuja kujutia.
Hiyo ndo hali niliyonayo saivi

Vijana wenzangu hasa ambao bado hatujawa na source ya kudumu ya kupata kipato,tuheshimu sana hela.

Nakosa hata hela ya kula kweli!,majuto kweli ni mjukuu.
hakika ni kweli
 
Miaka 4 nmeishi kama shetani nisie na mbele wala nyuma , hiyo ni baada ya uko nyuma kuchezea hela . Nilizani sifa walizokuwa wananipa walimaanisha nikajiona napendwa kila kona napopita yeyote akiniomba buku Nampa buku mbili, wa elfu tano Nampa bila kujiuliza mara mbili , kumbe ilikuwa inapendwa pesa tu sikujua ilo , nilivoishiwa sikumuona yeyote kati yao sio ndugu , sio rafiki, walaa wale mademu waliokuwa kutwa kuniita beb... Kwenye simu yangu walibakia watu wawili tu waliobaki kunitafuta na kunijulia hali , Mama yangu na mke wangu pekee ndo walibakia kuwa wafariji wangu.... Leo Mambo yamerudi kuwa sawa baada ya msoto mkali , kiukweli nmejifunza vitu vingi sana ... Pesa yangu kuja mtu kuila kizembe sio rahisi aisee , pesa yangu saiv inaenda kwenye vitu muhimu pekee ....
 
Bila nidhamu ya pesa kwenye haya maisha,lazima kuna siku lazima utakuja kujutia.
Hiyo ndo hali niliyonayo saivi

Vijana wenzangu hasa ambao bado hatujawa na source ya kudumu ya kupata kipato,tuheshimu sana hela.

Nakosa hata hela ya kula kweli!,majuto kweli ni mjukuu.
Nadhani nimemkosea Mungu, ndugu zangu na mtoto wangu sana nimejikuta ndani ya miezi 7 nimeonga zaidi ya 10M kweli kama kurongwa kupo sasa baada yakutafakari zaidi demu anapigwa machine na mtu mwingine nimebidi ni shut down kila kitu nijipange upya tena.

Sent from my 601SO using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom