Ama kweli "IVUMAYO HAIDUMU"

Ama kweli "IVUMAYO HAIDUMU"

Ile mikono kuizungusha tena ni ngumu nasikia imenasia

Jiwe hajiamini, anajua kilichompata 2015 ndiyo maana alizuia mikutano ya kisiasa.

Wapinzani wanakamatwa wanapofanya mikutano na vikao vya ndani wakati Polepole na Bashiru wakizunguka nchi nzima kufanya kampeni.

Maendeleo hayana vyama, unaanzaje kuwa nyutro? Nikuteue mimi, mshahara nikulipe, posho nikupe, Gari nikupe, halafu umtangaze mpinzani.... Hiiiiiiiiiii!!!!!

"Kukiwa na uchaguzi huru na wa haki, CCM ijiandae kukabidhi nchi" Polepole akiongea kabla ya kuwekwa tonge domoni.
 
Mkuu umekata tamaa hata haueleweki nini umeandika.
Mkuu, rudia kusoma utaielewa tu. Vipi huko kwenu viwanda vingapi vimeshajengwa?, na wafanyabiashara wanasemaje juu ya uchumi wao?
 
Hili la kutatua shida ya maji kwa Dar es Salaam (nasikia kila mahali yanapatikana) ni jambo ambalo sisiti kuipa sifa serikali hii maana shida ya maji kwa Dar ilikuwa ni jambo la aibu sana. Sijui sustainability yake itakuwaje lakini sitegemei shida ijirudie tena.
 
Hili la kutatua shida ya maji kwa Dar es Salaam (nasikia kila mahali yanapatikana) ni jambo ambalo sisiti kuipa sifa serikali hii maana shida ya maji kwa Dar ilikuwa ni jambo la aibu sana. Sijui sustainability yake itakuwaje lakini sitegemei shida ijirudie tena.
Uwenauhakika! Usisikie tu.
 
Mkuu, rudia kusoma utaielewa tu. Vipi huko kwenu viwanda vingapi vimeshajengwa?, na wafanyabiashara wanasemaje juu ya uchumi wao?

Wafanyabiashara wanaendelea na biashara kama kawa??vipi huko kwenu wamrudi ndani kulala???

Viwanda naona serikali kila kukicha inahangaika kuweka mazingira safi,inaongeza vyanzo vya nishati na mawasiliano kuwa rahisi ili isiwe tabu kwa wenye uwezo kama kina mengi nk kuanzisha viwanda vyao.
 
Nauliza,
•Hivi zile za push-ups jukwaani ziliishia wapi? Bado zinaendelea? Tutumie nguvu hizo kulegeza vyuma vilivyokaza.
View attachment 977550
View attachment 977551
•Milioni 50 kila kijiji ziko wapi? Zimehamia miundombinu? Kupanga ni kuchagua.
View attachment 977548
•Wakulima wasipangiwe bei, je, wanapangiwa au hawapangiwi? Korosho hoyeeee? Nadhani sasa hivi mbuzi wanakunywa champagne badala ya bia.
View attachment 977559


•Watumishi wataboreshewa maslahi, nadhani wanasherekea, au siyo? Wakishindwa kupanda madaraja wapande ndege!
View attachment 977566

View attachment 977564
•Mahakama ya mafisadi imewahukum kina nani? Kina Mbowe? Akram? Vipi waliouza nyumba za NHC? Escrow? Richmond? Iptl?

Mikopo vyuo vikuu, neno lenyewe mkopo? Wanachuo, hali ikoje huko?

Tumbua, teua, zimeleta tija?

•Kauli yetu ya Hapa Kazi Tu, bado inavuma majukwaani? Vipi serikali ya viwanda?

•Wafanyabiashara sasa nadhani mna mazingira mazuri ya kufanyia biashara, mtatuangusha 2020? Wamachinga hoyee! Mmeshapata kipande?

Elimu bure safiii, na nyie dada zetu, kwanini mnakuwa wazazi kabla ya F4? Msitulaumu.

•Huduma za afya vijijini safi, lakini na nyie wananchi kwanini mnakataa kukata bima CHIF kwa sh.15,000/=?

Tunawatakia sikukuu njema.
View attachment 977570
Picha ya mwisho ndiyo iliyonifurahisha kuliko zote. Haina vitisho ina bashasha kwa mara ya kwanza. Kumbe akiacha ukatili ansura ya kawaida!!!! Mhe. Kassimu Majaliwa Majaliwa anayo kila sababu ya kutokuwa na woga maana si ameshikwa mkono na rais!!!!
 
Hivi ile "wacha waisome namba eeeh..."

Wanaisoma wapinzani tu?
Mkuu hivi watu bado wanasoma namba? Mimi naona giza linatanda haraka hata namba zenyewe kuzisoma sasa ni shida na sisi wenye macho mabovu ndio hatuzioni kabisa.
 
Back
Top Bottom