Trust None
JF-Expert Member
- Feb 12, 2018
- 1,260
- 4,421
Nauliza,
•Hivi zile za push-ups jukwaani ziliishia wapi? Bado zinaendelea? Tutumie nguvu hizo kulegeza vyuma vilivyokaza.
•Milioni 50 kila kijiji ziko wapi? Zimehamia miundombinu? Kupanga ni kuchagua.
•Wakulima wasipangiwe bei, je, wanapangiwa au hawapangiwi? Korosho hoyeeee? Nadhani sasa hivi mbuzi wanakunywa champagne badala ya bia.
•Watumishi wataboreshewa maslahi, nadhani wanasherekea, au siyo? Wakishindwa kupanda madaraja wapande ndege!
•Mahakama ya mafisadi imewahukum kina nani? Kina Mbowe? Akram? Vipi waliouza nyumba za NHC? Escrow? Richmond? Iptl?
•Mikopo vyuo vikuu, neno lenyewe mkopo? Wanachuo, hali ikoje huko?
•Tumbua, teua, zimeleta tija?
•Kauli yetu ya Hapa Kazi Tu, bado inavuma majukwaani? Vipi serikali ya viwanda?
•Wafanyabiashara sasa nadhani mna mazingira mazuri ya kufanyia biashara, mtatuangusha 2020? Wamachinga hoyee! Mmeshapata kipande?
•Elimu bure safiii, na nyie dada zetu, kwanini mnakuwa wazazi kabla ya F4? Msitulaumu.
•Huduma za afya vijijini safi, lakini na nyie wananchi kwanini mnakataa kukata bima CHIF kwa sh.15,000/=?
Tunawatakia sikukuu njema.
•Hivi zile za push-ups jukwaani ziliishia wapi? Bado zinaendelea? Tutumie nguvu hizo kulegeza vyuma vilivyokaza.
•Milioni 50 kila kijiji ziko wapi? Zimehamia miundombinu? Kupanga ni kuchagua.
•Wakulima wasipangiwe bei, je, wanapangiwa au hawapangiwi? Korosho hoyeeee? Nadhani sasa hivi mbuzi wanakunywa champagne badala ya bia.
•Watumishi wataboreshewa maslahi, nadhani wanasherekea, au siyo? Wakishindwa kupanda madaraja wapande ndege!
•Mahakama ya mafisadi imewahukum kina nani? Kina Mbowe? Akram? Vipi waliouza nyumba za NHC? Escrow? Richmond? Iptl?
•Mikopo vyuo vikuu, neno lenyewe mkopo? Wanachuo, hali ikoje huko?
•Tumbua, teua, zimeleta tija?
•Kauli yetu ya Hapa Kazi Tu, bado inavuma majukwaani? Vipi serikali ya viwanda?
•Wafanyabiashara sasa nadhani mna mazingira mazuri ya kufanyia biashara, mtatuangusha 2020? Wamachinga hoyee! Mmeshapata kipande?
•Elimu bure safiii, na nyie dada zetu, kwanini mnakuwa wazazi kabla ya F4? Msitulaumu.
•Huduma za afya vijijini safi, lakini na nyie wananchi kwanini mnakataa kukata bima CHIF kwa sh.15,000/=?
Tunawatakia sikukuu njema.