NALIA NGWENA
JF-Expert Member
- Oct 6, 2016
- 10,299
- 12,796
Wakati Yanga ikiwa ugenini kesho kuikabili Coastal Union katika mechi ya Ligi Kuu Bara, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga, Ally Kamwe amewataka mashabiki kusimama dakika ya 5 kwa ajili ya kuwapongeza wachezaji kwa ushindi wa mabao 5-1 walioupata dhidi ya Simba Novemba 5
“Mashabiki wa Yanga tutakaoingia Mkwakwani kesho, tunaombwa ikifika dakika ya 5 kwenye mchezo wetu Vs Coastal Union, tusimame wote na kuinua mkono mmoja juu tukionyesha ishara ya vidole vitano . Hii ni kwa ajili ya kuwapongeza wachezaji wetu kwa kazi nzuri waliyoifanya,” ameandika Kamwe
“Mashabiki wa Yanga tutakaoingia Mkwakwani kesho, tunaombwa ikifika dakika ya 5 kwenye mchezo wetu Vs Coastal Union, tusimame wote na kuinua mkono mmoja juu tukionyesha ishara ya vidole vitano . Hii ni kwa ajili ya kuwapongeza wachezaji wetu kwa kazi nzuri waliyoifanya,” ameandika Kamwe