Ally Kamwe: Mashabiki wa Yanga Sc watasimama kwenye dakika ya 5 na kupongeza wachezaji kwa ushindi dhidi ya mtani

NALIA NGWENA

JF-Expert Member
Oct 6, 2016
10,299
12,796
Wakati Yanga ikiwa ugenini kesho kuikabili Coastal Union katika mechi ya Ligi Kuu Bara, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga, Ally Kamwe amewataka mashabiki kusimama dakika ya 5 kwa ajili ya kuwapongeza wachezaji kwa ushindi wa mabao 5-1 walioupata dhidi ya Simba Novemba 5

“Mashabiki wa Yanga tutakaoingia Mkwakwani kesho, tunaombwa ikifika dakika ya 5 kwenye mchezo wetu Vs Coastal Union, tusimame wote na kuinua mkono mmoja juu tukionyesha ishara ya vidole vitano . Hii ni kwa ajili ya kuwapongeza wachezaji wetu kwa kazi nzuri waliyoifanya,” ameandika Kamwe
 
Wamepata content
1699246194307.jpg
 
Meneja wa habari na mawasiliano wa klabu ya Yanga SC Ally Kamwe amewataka Mashabiki wa klabu hiyo kusimama na kuinua mkono mmoja juu ikifika dakika ya kuonyesha ishara ya vidole vitano katika mchezo wa kesho dhidi ya Coastal ikiwa ni ishara ya kuwapongeza Wachezaji wa klabu hiyo kwa kazi nzuri waliyoifanya kwenye ushindi wa 5-1 dhidi ya Watani wao Simba SC.

“Mashabiki wa @YoungAfricansSC tutakaoingia Mkwakwani kesho, Tunaombwa ikifika DAKIKA YA 5 kwenye mchezo wetu Vs Coastal Union Tusimame wote na kuinua mkono mmoja juu tukionyesha ishara ya vidole vitano Hii ni kwa ajili ya kuwapongeza Wachezaji wetu kwa kazi nzuri waliyoifanya” ameandika Ally Kamwe kwenye ukurasa wake wa mitandao ya kijamii.

Una maoni gani kuhusu hatua hiyo ya Kamwe?

#KitengeSports
1699427658767.jpg
 
Back
Top Bottom