Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Ally Hapi, leo Septemba 27 katika mahojiano ya Cafe Talk Jijini Dar es salaam, akijibu swali lililoulizwa na Mwaandishi wa Habari Charles William, amesema utekelezaji wa mpango wa Bima ya Afya kwa Wote utasaidia kuondoa changamoto zinazowakabili Wananchi katika kupata huduma za matibabu ikiwemo gharama kubwa za tiba na mapungufu ya vifurushi vya Bima vilivyopo sasa.
Hapi amesema changamoto hizo zitapatiwa suluhisho na kwamba mpango huo unalenga kufanikisha matibabu ya magonjwa makubwa yanayowasumbua Watanzania wengi kama saratani, magonjwa ya moyo, figo na kisukari, ambayo gharama zake za matibabu ni kubwa mno.
“Kwa mara ya kwanza, Serikali itagharamia matibabu ya magonjwa haya makubwa, hivyo changamoto ambazo wananchi wamekuwa wakilalamikia, tutazitatua kwa asilimia mia moja kupitia mpango huu” amesema Ally Hapi.
Aidha, ameeleza kuwa mpango huu utaanza kutekelezwa kwa mageuzi yatakayofanywa ndani ya Siku 100 na Mgombea urais kupitia Chama hicho cha CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan iwapo atapata ridhaa ya kuiongoza Serikali tena baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Ally Hapi, leo Septemba 27 katika mahojiano ya Cafe Talk Jijini Dar es salaam, akijibu swali lililoulizwa na Mwaandishi wa Habari Charles William, amesema utekelezaji wa mpango wa Bima ya Afya kwa Wote utasaidia kuondoa changamoto zinazowakabili Wananchi katika kupata huduma za matibabu ikiwemo gharama kubwa za tiba na mapungufu ya vifurushi vya Bima vilivyopo sasa.
Hapi amesema changamoto hizo zitapatiwa suluhisho na kwamba mpango huo unalenga kufanikisha matibabu ya magonjwa makubwa yanayowasumbua Watanzania wengi kama saratani, magonjwa ya moyo, figo na kisukari, ambayo gharama zake za matibabu ni kubwa mno.
“Kwa mara ya kwanza, Serikali itagharamia matibabu ya magonjwa haya makubwa, hivyo changamoto ambazo wananchi wamekuwa wakilalamikia, tutazitatua kwa asilimia mia moja kupitia mpango huu” amesema Ally Hapi.
Aidha, ameeleza kuwa mpango huu utaanza kutekelezwa kwa mageuzi yatakayofanywa ndani ya Siku 100 na Mgombea urais kupitia Chama hicho cha CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan iwapo atapata ridhaa ya kuiongoza Serikali tena baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Ally Hapi, leo Septemba 27 katika mahojiano ya Cafe Talk Jijini Dar es salaam, akijibu swali lililoulizwa na Mwaandishi wa Habari Charles William, amesema utekelezaji wa mpango wa Bima ya Afya kwa Wote utasaidia kuondoa changamoto zinazowakabili Wananchi katika kupata huduma za matibabu ikiwemo gharama kubwa za tiba na mapungufu ya vifurushi vya Bima vilivyopo sasa.
Hapi amesema changamoto hizo zitapatiwa suluhisho na kwamba mpango huo unalenga kufanikisha matibabu ya magonjwa makubwa yanayowasumbua Watanzania wengi kama saratani, magonjwa ya moyo, figo na kisukari, ambayo gharama zake za matibabu ni kubwa mno.
“Kwa mara ya kwanza, Serikali itagharamia matibabu ya magonjwa haya makubwa, hivyo changamoto ambazo wananchi wamekuwa wakilalamikia, tutazitatua kwa asilimia mia moja kupitia mpango huu” amesema Ally Hapi.
Aidha, ameeleza kuwa mpango huu utaanza kutekelezwa kwa mageuzi yatakayofanywa ndani ya Siku 100 na Mgombea urais kupitia Chama hicho cha CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan iwapo atapata ridhaa ya kuiongoza Serikali tena baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025