rungwe
Member
- Dec 28, 2010
- 19
- 20
[h=3][/h]
Katika kampeni za uchaguzi wa mwaka 2005 Rais Jakaya Kikwete alitoa ahadi kedekede za kuwavutia wananchi. Maisha bora kwa kila mtanzania, kukomesha rushwa na kuondoa kero zote zilizokuwa zikiwasumbua watanzania. Mheshimiwa Kikwete aliahidi kutekeleza hayo yote kwa ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya.
Mara tu baada ya kuingia ikulu, mheshimiwa Rais akaanza kutekeleza ahadi zake kwa vitendo. Waziri mkuu wake Mheshimiwa Edward Lowasa mara moja akaitisha mikutano kadhaa ya viongozi wa bodi za mazao ya pamba, korosho, kahawa na kadhalika. Lengo la mikutano hiyo iliyofanyikia katika ukumbi maarufu wa Karimjee lilikuwa kuchambua matatizo yanayo wakabili wakulima, kuandaa mikakati mpya ya kuboresha uzalishaji wa mazao hayo, na kuandaa mbinu za kuwawezesha wakulima ili waweze kuzalisha katika kiwango cha juu zaidi na kuweza kuuza mazao ya biashara nje ya nchi.
Wakati mheshimiwa Lowasa akishughulika na maswala ya wakulima, Rais Kikwete akafanya ziara maalum katika mkoa wa Dar es salaam ili kujua matatizo yanayo likabili jiji hilo ambalo kwa kiasi kikubwa ndio linawakilisha hali ya miji mingine midogo. Katika ziara hiyo Rais alikagua miundo mbinu ya jiji, maeneo ya biashara na maofisi kadhaa ya serikali ili kupata picha halisi ya mahitaji ya wananchi.
Si hivyo tu, Rais akatembelea magereza ya Keko, Ukonga, na Segelea ambako alikutana na wafungwa na kuzungumza na maafisa wa magereza ili kujua matatizo yanayo wakabili wafungwa na maaskari. Kwa mara ya kwanza katika historia, Rais wa nchi akazungumza mpaka na wafungwa waliohukumiwa kifo na kuwaahidi kuzipitia upya kesi zao ili kuweza kuwasamehe wale ambao wanastahili msamaha. Aidha Rais akaagiza wafungwa hao wapewe chakula kizuri na huduma nyingine bora ambazo binadamu anastahili. Mpaka hapo kila mtanzania akaruka ruka kwa furaha...hatujawahi kupata Rais mwema kama huyu.
Zikafuatia ziala za ghafla katika hospitali, maofisi ya serikali na sehemu nyinginezo ambazo katika utawala uliotangulia watu walisha sahau kwamba Rais wa nchi anapaswa kufika. Lengo ikiwa ni kuwaamsha wananchi ili wawajibike wakati wote wakijua kuwa Rais anaweza kuja wakati wowote.
Mwezi Desemba ulipofika, serikali ya Rais Kikwete ikaandaa sherehe kubwa ya uhuru. Sherehe hiyo tofauti kabisa na nyingine zilizo tangulia ilikuwa na lengo la kurudisha moyo wa uzalendo kwa watanzania, ili wananchi waipende na kujivunia nchi yao. Kwa mara nyingine watanzania wakapiga makofi na vigelele kwa kupata Rais anaefaa.
Ghafla ukasikika uvumi wa ajabu. Kwamba kuna watu waliokuwa wanatoa vitisho kwa Rais Kikwete na kwamba maisha yake yalikuwa hatarini. Baadhi ya raia wakapiga kelele sana na kuwaomba polisi na idara ya usalama wa Taifa kuongeza ulinzi kwa Rais wetu ili mabedui hao wasije wakamdhuru. Hata hivyo, hakuna aliyemgusa Rais na baada ya muda uvumi huo ukatoweka.
Tatizo ni kwamba, uvumi huo uliondoka na Rais Kikwete wetu tuliyekuwa tukijivunia. Ushujaa, wema na mikakati ya Rais kikwete tuliyokuwa tumeanza kuiona ikayeyuka kama samli katika kikaango. Hali mbaya ya maisha ikavamia nchini kama moto wa petroli. Wezi, mafisadi na wahujumuwa mali za umma wakaanza kutamba waziwazi bila kujali kwamba kuna serikali halali na Rais aliye chaguliwa kwa ridhaa ya wananchi. Mikataba ya aibu ikawa inaendelea kufanyika huku serikali ikiwa kimyaa kana kwamba mafisadi hao ni waajiliwa wa serikali. Mpaka ilipofika uchaguzi wa mwaka 2010, watanzania waka wana jiuliza mara mbili kama kweli anastahili kurudishwa ikulu.
Hapo ndipo tunapojiuliza, kubadilika kwa Rais Kikwete kulitokana na vitisho alivyo vipata au ni 'change of heart?' Kama ni vitisho, ni mtu gani anaethubutu kumtisha Rais? ina maana huyo mtu haogopi majeshi yetu yote ya ulinzi na usalama? ana ubavu kiasi gani huyo mtu? Au anajua siri gani za Rais Kikwete kiasi cha kum- blackmail? Rais Jakaya Kikwete tunaemjua ni mwema, mpole, mkarimu, mwingi wa huruma, Rais anaethubu kuwaonea huruma wafungwa walioua na kuagiza watendewe haki. Ndio maana tunajiuliza ni nani aliye mtisha? Tunaomba anaejua, atupatie jawabu.
mwana dikala
Katika kampeni za uchaguzi wa mwaka 2005 Rais Jakaya Kikwete alitoa ahadi kedekede za kuwavutia wananchi. Maisha bora kwa kila mtanzania, kukomesha rushwa na kuondoa kero zote zilizokuwa zikiwasumbua watanzania. Mheshimiwa Kikwete aliahidi kutekeleza hayo yote kwa ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya.
Mara tu baada ya kuingia ikulu, mheshimiwa Rais akaanza kutekeleza ahadi zake kwa vitendo. Waziri mkuu wake Mheshimiwa Edward Lowasa mara moja akaitisha mikutano kadhaa ya viongozi wa bodi za mazao ya pamba, korosho, kahawa na kadhalika. Lengo la mikutano hiyo iliyofanyikia katika ukumbi maarufu wa Karimjee lilikuwa kuchambua matatizo yanayo wakabili wakulima, kuandaa mikakati mpya ya kuboresha uzalishaji wa mazao hayo, na kuandaa mbinu za kuwawezesha wakulima ili waweze kuzalisha katika kiwango cha juu zaidi na kuweza kuuza mazao ya biashara nje ya nchi.
Wakati mheshimiwa Lowasa akishughulika na maswala ya wakulima, Rais Kikwete akafanya ziara maalum katika mkoa wa Dar es salaam ili kujua matatizo yanayo likabili jiji hilo ambalo kwa kiasi kikubwa ndio linawakilisha hali ya miji mingine midogo. Katika ziara hiyo Rais alikagua miundo mbinu ya jiji, maeneo ya biashara na maofisi kadhaa ya serikali ili kupata picha halisi ya mahitaji ya wananchi.
Si hivyo tu, Rais akatembelea magereza ya Keko, Ukonga, na Segelea ambako alikutana na wafungwa na kuzungumza na maafisa wa magereza ili kujua matatizo yanayo wakabili wafungwa na maaskari. Kwa mara ya kwanza katika historia, Rais wa nchi akazungumza mpaka na wafungwa waliohukumiwa kifo na kuwaahidi kuzipitia upya kesi zao ili kuweza kuwasamehe wale ambao wanastahili msamaha. Aidha Rais akaagiza wafungwa hao wapewe chakula kizuri na huduma nyingine bora ambazo binadamu anastahili. Mpaka hapo kila mtanzania akaruka ruka kwa furaha...hatujawahi kupata Rais mwema kama huyu.Zikafuatia ziala za ghafla katika hospitali, maofisi ya serikali na sehemu nyinginezo ambazo katika utawala uliotangulia watu walisha sahau kwamba Rais wa nchi anapaswa kufika. Lengo ikiwa ni kuwaamsha wananchi ili wawajibike wakati wote wakijua kuwa Rais anaweza kuja wakati wowote.
Mwezi Desemba ulipofika, serikali ya Rais Kikwete ikaandaa sherehe kubwa ya uhuru. Sherehe hiyo tofauti kabisa na nyingine zilizo tangulia ilikuwa na lengo la kurudisha moyo wa uzalendo kwa watanzania, ili wananchi waipende na kujivunia nchi yao. Kwa mara nyingine watanzania wakapiga makofi na vigelele kwa kupata Rais anaefaa.
Ghafla ukasikika uvumi wa ajabu. Kwamba kuna watu waliokuwa wanatoa vitisho kwa Rais Kikwete na kwamba maisha yake yalikuwa hatarini. Baadhi ya raia wakapiga kelele sana na kuwaomba polisi na idara ya usalama wa Taifa kuongeza ulinzi kwa Rais wetu ili mabedui hao wasije wakamdhuru. Hata hivyo, hakuna aliyemgusa Rais na baada ya muda uvumi huo ukatoweka.
Tatizo ni kwamba, uvumi huo uliondoka na Rais Kikwete wetu tuliyekuwa tukijivunia. Ushujaa, wema na mikakati ya Rais kikwete tuliyokuwa tumeanza kuiona ikayeyuka kama samli katika kikaango. Hali mbaya ya maisha ikavamia nchini kama moto wa petroli. Wezi, mafisadi na wahujumuwa mali za umma wakaanza kutamba waziwazi bila kujali kwamba kuna serikali halali na Rais aliye chaguliwa kwa ridhaa ya wananchi. Mikataba ya aibu ikawa inaendelea kufanyika huku serikali ikiwa kimyaa kana kwamba mafisadi hao ni waajiliwa wa serikali. Mpaka ilipofika uchaguzi wa mwaka 2010, watanzania waka wana jiuliza mara mbili kama kweli anastahili kurudishwa ikulu.Hapo ndipo tunapojiuliza, kubadilika kwa Rais Kikwete kulitokana na vitisho alivyo vipata au ni 'change of heart?' Kama ni vitisho, ni mtu gani anaethubutu kumtisha Rais? ina maana huyo mtu haogopi majeshi yetu yote ya ulinzi na usalama? ana ubavu kiasi gani huyo mtu? Au anajua siri gani za Rais Kikwete kiasi cha kum- blackmail? Rais Jakaya Kikwete tunaemjua ni mwema, mpole, mkarimu, mwingi wa huruma, Rais anaethubu kuwaonea huruma wafungwa walioua na kuagiza watendewe haki. Ndio maana tunajiuliza ni nani aliye mtisha? Tunaomba anaejua, atupatie jawabu.
mwana dikala