Goliath mfalamagoha
JF-Expert Member
- Aug 3, 2012
- 602
- 2,505
CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA) JIMBO LA IRINGA MJINI :
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NA UMMA.
YAH: KUFUKUZWA UANACHAMA NDUGU DADY JOHANES IGOGO :
Dady Igogo aliyekuwa Diwani wa CHADEMA kata ya Gangilonga na Naibu Meya Manispaa ya Iringa ; alikisaliti Chama na kujivua nafasi ya Unaibu Meya na baadaye Udiwani kwa kile alichokiita " Sababu zilizoko moyoni mwake "
Katiba ya CHADEMA 2006 , Toleo la 2016 Ibara 5.4. Inaeleza na kufafanua juu ya "kukoma kwa uanachama ".
Vile vile Ibara 5.4. (1 , 2, na 3) inaeleleza kuwa mwanachama atakoma uanachama wake kwa kujiuzulu , kufariki , kuachishwa ama kufukuzwa.
Ndugu Igogo kwa muda mrefu amekuwa na mwenendo usioendana na Itikadi , Falsafa , Madhumuni , Kanuni , Maadili na Sera za Chama .
Kamati tendaji ya Jimbo katika kikao chake cha dharura kilichoketi Tar.24/04/2018 kiliazimia yafuatayo :
1. Dady Igogo avuliwe ujumbe wa kamati tendaji ya Jimbo kwa mujibu wa Ibara 7.4.10 (x) na Ibara 7.7.8 (k) kwa kwenda kinyume na katiba ya chama , kanuni na maadili ya chama.
2. Dady Igogo afukuzwe uanachama kwa mujibu wa Ibara 5.4.3 kwa kuwa amekosa sifa za kuendelea kuwa mwanachama wa CHADEMA.
Hivyo kuanzia leo tar 28/04/2018 Chama kinatoa taarifa kwa wanachama na umma kuwa Dady Igogo sio mwanachama wa CHADEMA tena.
Imetolewa na ;
Suzana Mgonokulima.
Katibu wa CHADEMA.
Jimbo la Iringa Mjini.
27/04/2018.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NA UMMA.
YAH: KUFUKUZWA UANACHAMA NDUGU DADY JOHANES IGOGO :
Dady Igogo aliyekuwa Diwani wa CHADEMA kata ya Gangilonga na Naibu Meya Manispaa ya Iringa ; alikisaliti Chama na kujivua nafasi ya Unaibu Meya na baadaye Udiwani kwa kile alichokiita " Sababu zilizoko moyoni mwake "
Katiba ya CHADEMA 2006 , Toleo la 2016 Ibara 5.4. Inaeleza na kufafanua juu ya "kukoma kwa uanachama ".
Vile vile Ibara 5.4. (1 , 2, na 3) inaeleleza kuwa mwanachama atakoma uanachama wake kwa kujiuzulu , kufariki , kuachishwa ama kufukuzwa.
Ndugu Igogo kwa muda mrefu amekuwa na mwenendo usioendana na Itikadi , Falsafa , Madhumuni , Kanuni , Maadili na Sera za Chama .
Kamati tendaji ya Jimbo katika kikao chake cha dharura kilichoketi Tar.24/04/2018 kiliazimia yafuatayo :
1. Dady Igogo avuliwe ujumbe wa kamati tendaji ya Jimbo kwa mujibu wa Ibara 7.4.10 (x) na Ibara 7.7.8 (k) kwa kwenda kinyume na katiba ya chama , kanuni na maadili ya chama.
2. Dady Igogo afukuzwe uanachama kwa mujibu wa Ibara 5.4.3 kwa kuwa amekosa sifa za kuendelea kuwa mwanachama wa CHADEMA.
Hivyo kuanzia leo tar 28/04/2018 Chama kinatoa taarifa kwa wanachama na umma kuwa Dady Igogo sio mwanachama wa CHADEMA tena.
Imetolewa na ;
Suzana Mgonokulima.
Katibu wa CHADEMA.
Jimbo la Iringa Mjini.
27/04/2018.