KIBURUDISHO swali lako ni muhimu saana!
Japo watu wasio jua jibu wanaleta mzaha na kejeli kwako!
Jibu ni kuwa
Ramani ya dunia imechorwa kutoka na jitihada ya
wavumbuzi mbalimbali ambao wametembea kuzunguka dunia.
Na wakusanyaji mbalimbali wa ramani za nchi tofauti na mipaka yake.
Ilichukua miaka miiingi sana kuipata ramani tulionayo leo.
Kama utarejea kwenya geographic maps za awali kabla ya ugunduzi wa kamera na upaaji wa angani! Basi ramani zile zilikuwa na ulakini mwingi! Na kasoro nyingi mno,
Na zimefanyiwa maregebisho mengi sana!
Baada ya uvumbuzi wa kamera na uwezo wa mwanadamu kupaa angani kwa kutumia vyombo mbalimbali
Hapo ndipo tulipoweza kupiga picha ya mkoa kwa mkoa. Nchi kwa nchi. Bara kwa bara.
Na hatimae kuziweka pamoja na kupata ramani tulionayo leo.
Asante kwa kuuliza
Na kama kuna lingine uliza usione aibu!