Alivyosikia nimeoa kaanza kunitusi.

Alivyosikia nimeoa kaanza kunitusi.

Huwezi fanywa lolote bali ni maumivu ya wewe kuoa.Huyo ni mwepesi kama pamba.Tulia usimfuatilie ikiwa anahoja ataenda mahakamani au ustawi wa jamii ama kwa wazazi wako.
Endelea kumpotezea hivyo hivyo.Huyo kiburudisho wako mpya tulia naye mwelekeze A to Z na umpange vizuri ili naye akusaidie kusolve inshu.Siku akikupigia simu mlengeshee kwa mkeo amchambue sawasawa kama mkeo muoga tafuta lijimama hata la kukodi ulipe namba limbwatukie hadi ajue kuwa wewe uliyemuoa ni zaidi ya MANGE KIMAMBI.
Acha kulegea ukweli sipendi kutishwa maishani najiamini mno hadi najiogopa mwenyewe maana sipendi kumnyanyasa mwanamke wala nami kunyanyasika wala kuona mwingine ananyanyasika.
Nipe sub hiyo kazi mkuu usipate shida.
 
Binafsi ni muumin wa malezi ya wanafamilia wote kwa mtoto, kuna madhara makubwa sana kwa aina ya ndoa kama hiyo, ni vema kuwa makini na kuzaa ovyo, baadae mtoto anakuwa mhanga, pia kumbuka ukiwa unatuma hela ya matumizi utakuwa unamtunza na mama ws mtoto, huo ni mtazamo wangu tu.
 
Kaonane naye muongee maana kukaa kimya haitatatua tatizo ikiwezekana mchukue mtoto au mpange jinsi ya kumlea maana umri wa kuanza masomo umekaribia ni jambo zuri ukaanza kuwa karibu na mtoto mm mzazi mwenzangu alileta matatizo kama ayo mwanzoni kabisa ila nilitumia busara saivi tunalea mtoto kwa amani japo mikwaruzo inakuwa ila naipotezea
 
Yaani huyo mzazi mwenzio ni mjinga na mpumbavu kama alivyokuwa mtalaka wangu, wana kiburi na wamejaa ujinga sana hawa wanawake
 
Kwanza kabisa, kumbuka huyo ni mwanao na unalo jukumu la kumlea na kumtengenezea future hata ikiwa wazazi wake watakuwa wana uwezo kukuzidi wewe.

Pili, Si jambo zuri kuachana na mwanamke mliyejaaliwa kuwa na mtoto kwa shari hata ikiwa hivyo jaribu kumtafuta kisha msuluhishe halafu mwambie kuwa kwasasa kilichobaki ni kumlea mtoto na ikiwa atapata anayehitaji kumuoa wewe upo tayari, nawe ukipata naye awe tayari...athari kubwa hapa ni kuwa mtoto hulelewa kwa chuki hasa kwa baba yake hivyo huwenda akikuwa hatakuwa anathamini uwepo wa baba maishani mwake.

Ila kwa kuwa huko kote pamepita kilichobaki kurekebisha ni hapa.

Hakikisha uliye nae anajuwa ukweli hasa juu ya mtoto wako, na ikiwezekana mfanye amjuwe.
 
Back
Top Bottom