Niko kwenye kipindi kigumu sana wana MMU, nahitaji msaada wenu kwa ushauri na mengine.
Iko hivi;
Nilitokea kumpenda binti mmoja ambaye pia alinipenda, mahusiano yetu yalianza kama urafiki ambao ulitokana na familia zetu kuwa karibu (family friend), kwa muda mrefu tulidumu katika urafiki wa kawaida, nilipofika kidato cha nne (nilimtangulia darasa) tulianzisha mahusihano rasmi ya kimapenzi, bahati mbaya baada ya mtihan yeye hakupata ufahulu mzuri, mimi kwa kipindi hicho nilikuwa advance level.
Kutokana na familia yake kutokuwa na uwezo waliamua kumpeleka jeshini (JKT) alpomaliza akakaa two years (mkataba) kipindi chote hicho tulikuwa tunawasiliana ingawa kwa shida kutoka na yeye kutokuwa na simu alafu mimi nilikuwa boarding so mawasiliano yalikuwa likizo ingawa kwa shida sana (wakati mwingine likizo iliisha bila kuwasiliana)
Baada ya mimi kuingia chuo kikuu, yeye alipata mkataba mwingine (baada ya wa awali kumalizika bila kupata ajira) kipindi chote tulishirikiana na kupeana moyo tukikumbushana ahadi na mipango tuliyowekeana, tuligawana bum kutokana na maisha magumu ya Jeshini hasa swala la hela ya matumizi( 50000 kwa mwezi)
Mwaka wa pili wa mkataba akapata nafasi ya kujiunga JWTZ akapiga depo na kumalizia makutopola Dodoma, alinialika kwenye gwaride la kufunga mafunzo kipindi icho nlikuwa Dar es salaam, kutokana na kushindwa kufika (nilikuwa kwenye maandalizi ya UE) nikamuomba mdogo wangu aliyekuwa UDOM akaniwakilishe kule.Baada ya kuhitimu chuo na kuanza kusugua gaga kutafuta kazi na yeye akiwa mwajiriwa wa Jeshi matatizo yalianzia hapo.
Alianza visa vingi vya ajabu, kutopokea simu, text hazijibiwi, hapigi simu mpaka mimi nimtafute kuna kipindi alikuja likizo nyumbani nikaongea nae kwa kirefu kuhusu mahusiano yetu aliahidi kurekebisha kasoro hizo.
Kipindi chote kuna mambo mengi yalinihuzunisha sana, nakumbuka kipindi anaanza kidato cha kwanza aliniandkia barua (mpaka leo ninayo) barua ilisisitiza tuendlee kutunzana ikiwemo kutomtaka kimapenzi mpaka amalize masomo yake, cha kushangaza alipofika form three akaniandikia barua ya kuniomba msamaha kwamba ameshawishiwa na tayari alikuwa kwenye mahusiano na mwalimu na tayari wameshiriki ngono, nliumia sana (alimtoa bikra yule ticha).
Aliniomba msamaha kupitia dada yake nilimsamehe, kipindi ameanza kazi jeshini alikuwa kambi Morogoro alikuja Dar kikazi nikaonana nae tuliongea mengi akapewa ruhusa tukalala nae usiku ule akaniambia kule jeshini alishapata boyfrend ambaye walianza mahusiano baada ya mimi kuonekana simjali, na usiku ule alikuwa anasaliti, niilimwambia sawa kwa sababu now wewe ni mtu mzima unaamua unachokitaka.
Kwa ufupi alibadilika sana baada ya kupata kazi na mimi nikiwa mtaani nasugua gaga, aliwaambia ndugu zake mimi hanipendi tena so wasiniite shemeji, ingawa nilivyomuuliza alikataa na kunihakikishia tuko pamoja, kilichokuwa kinanipa wasiwasi muda wote niko chuo nlijitahidi kumsaidia bum likitoka na hata before kishule shule tuligawana hela nilizokuwa napewa nyumbani but alivyopata kazi kila nikimuomba msaada kidogo alinijibu ana majukumu mengi hivyo hawezi nisaidia nisubiri muda utafika.
Bahati nzuri mwaka jana nikapata kazi, sikutaka kumwambia sijui alipata wapi habari akaanza kunimiminia text za pongezi, mwezi uliopita alipata likizo nilimuomba sana apite kwangu alishtuka aliponiona nimebadirika, umbile, status na hata alipofika ndani kwangu aliendelea kushangaa.
Tangu hapo kila siku ananipigia, akinituhumu mimi ndo chanzo cha penzi letu kuyumba so anaomba tukae tuweke mambo sawa coz hataki kuolewa na mwanajeshi mwenzio ambae yuko nae now.
Najiuliza kweli nastahili lawama hizi je, nifanye nini?
Iko hivi;
Nilitokea kumpenda binti mmoja ambaye pia alinipenda, mahusiano yetu yalianza kama urafiki ambao ulitokana na familia zetu kuwa karibu (family friend), kwa muda mrefu tulidumu katika urafiki wa kawaida, nilipofika kidato cha nne (nilimtangulia darasa) tulianzisha mahusihano rasmi ya kimapenzi, bahati mbaya baada ya mtihan yeye hakupata ufahulu mzuri, mimi kwa kipindi hicho nilikuwa advance level.
Kutokana na familia yake kutokuwa na uwezo waliamua kumpeleka jeshini (JKT) alpomaliza akakaa two years (mkataba) kipindi chote hicho tulikuwa tunawasiliana ingawa kwa shida kutoka na yeye kutokuwa na simu alafu mimi nilikuwa boarding so mawasiliano yalikuwa likizo ingawa kwa shida sana (wakati mwingine likizo iliisha bila kuwasiliana)
Baada ya mimi kuingia chuo kikuu, yeye alipata mkataba mwingine (baada ya wa awali kumalizika bila kupata ajira) kipindi chote tulishirikiana na kupeana moyo tukikumbushana ahadi na mipango tuliyowekeana, tuligawana bum kutokana na maisha magumu ya Jeshini hasa swala la hela ya matumizi( 50000 kwa mwezi)
Mwaka wa pili wa mkataba akapata nafasi ya kujiunga JWTZ akapiga depo na kumalizia makutopola Dodoma, alinialika kwenye gwaride la kufunga mafunzo kipindi icho nlikuwa Dar es salaam, kutokana na kushindwa kufika (nilikuwa kwenye maandalizi ya UE) nikamuomba mdogo wangu aliyekuwa UDOM akaniwakilishe kule.Baada ya kuhitimu chuo na kuanza kusugua gaga kutafuta kazi na yeye akiwa mwajiriwa wa Jeshi matatizo yalianzia hapo.
Alianza visa vingi vya ajabu, kutopokea simu, text hazijibiwi, hapigi simu mpaka mimi nimtafute kuna kipindi alikuja likizo nyumbani nikaongea nae kwa kirefu kuhusu mahusiano yetu aliahidi kurekebisha kasoro hizo.
Kipindi chote kuna mambo mengi yalinihuzunisha sana, nakumbuka kipindi anaanza kidato cha kwanza aliniandkia barua (mpaka leo ninayo) barua ilisisitiza tuendlee kutunzana ikiwemo kutomtaka kimapenzi mpaka amalize masomo yake, cha kushangaza alipofika form three akaniandikia barua ya kuniomba msamaha kwamba ameshawishiwa na tayari alikuwa kwenye mahusiano na mwalimu na tayari wameshiriki ngono, nliumia sana (alimtoa bikra yule ticha).
Aliniomba msamaha kupitia dada yake nilimsamehe, kipindi ameanza kazi jeshini alikuwa kambi Morogoro alikuja Dar kikazi nikaonana nae tuliongea mengi akapewa ruhusa tukalala nae usiku ule akaniambia kule jeshini alishapata boyfrend ambaye walianza mahusiano baada ya mimi kuonekana simjali, na usiku ule alikuwa anasaliti, niilimwambia sawa kwa sababu now wewe ni mtu mzima unaamua unachokitaka.
Kwa ufupi alibadilika sana baada ya kupata kazi na mimi nikiwa mtaani nasugua gaga, aliwaambia ndugu zake mimi hanipendi tena so wasiniite shemeji, ingawa nilivyomuuliza alikataa na kunihakikishia tuko pamoja, kilichokuwa kinanipa wasiwasi muda wote niko chuo nlijitahidi kumsaidia bum likitoka na hata before kishule shule tuligawana hela nilizokuwa napewa nyumbani but alivyopata kazi kila nikimuomba msaada kidogo alinijibu ana majukumu mengi hivyo hawezi nisaidia nisubiri muda utafika.
Bahati nzuri mwaka jana nikapata kazi, sikutaka kumwambia sijui alipata wapi habari akaanza kunimiminia text za pongezi, mwezi uliopita alipata likizo nilimuomba sana apite kwangu alishtuka aliponiona nimebadirika, umbile, status na hata alipofika ndani kwangu aliendelea kushangaa.
Tangu hapo kila siku ananipigia, akinituhumu mimi ndo chanzo cha penzi letu kuyumba so anaomba tukae tuweke mambo sawa coz hataki kuolewa na mwanajeshi mwenzio ambae yuko nae now.
Najiuliza kweli nastahili lawama hizi je, nifanye nini?