Aliens & extraterrestrials

Jun 17, 2022
4
16
UTANGULIZI

Kuna tofauti kati ya Aliens na Extraterrestrials.
Extraterrestrials inatokana na maneno "Extra" na "Terra". Terra inamaanisha Dunia Extra ni Zaidi kwa hiyo extraterrestrials ni viumbe wa angani (Celestrial beings) kutoka kwenye dunia nyingine wanaokuja kutokea kwenye dunia ya ziada yaani extra terraa.

Neno Alien kwasasa nitalielezea kwa mapana zaidi tofauti na awali ambapo kwenye mada hii neno alien linamaanisha kitu ambacho hakifahamiki, ni viumbe wanaokwenda kinyume na asili yaani "nature" na wanakwenda kinyume na utaratibu wa ulimwengu (Order of Cosmos) kwa kua wanyonyaji yaani parasaiti wa viumbe hai wengine ambao wanashikilia mwanga na nishati. Kwa hiyo hapa tunaendelea kupata tofauti kati ya aliens na Anunnaki kwamba, ANUNNAKI ni Extraterrestrials na ni viumbe wema wakati viumbe wengine wa sayari ya nje ya dunia ambao wanaishi chini ya ardhi hapa hapa duniani mfano Draco - zetas ambao tumewaona kwa uchache kwenye nakala zilizo pita wao ni Aliens kwa kua wana athari hasi kwa wanadamu. Hilo sio somo letu kwa sasa kwani somo hilo kwa hakika tumekwisha lijadili kwa kina kwenye nakala zilizo pita. Kwenye nakala hii tutazungumzia utekaji wa aliens ambao wanateka wanadamu kwa kushirikiana na Serikali wao wakiwapa serikali zawadi ya Teknolojia. Hili linawezekanaje? ngoja tuone.

Kuanzia miaka ya awali ya mwaka 1900 hadi karibia 1930 Teknolojia ilibadilika kutoka kusukuma Wagon (Gari) kwa kutumia farasi (Horses) na kupiga bunduki kwa unga wa bunduki (Gun Powder) hadi kuanza kurusha roketi ya kwanza angani kwenye mwaka 1938 hivi. Katika muda wa kipindi cha miaka 30, Serikali ya Marekani, au serikali za dunia zimapitia kwenye hatua kubwa za mabadiliko ya teknolojia kutoka kusukuma wagon kwa kutumia Farasi hadi kurusha roketi kwenye anga ya nje (Outer space).

Sasa mtu mfikiriaji wa kawaida kabisa ukimwambia taarifa hiyo na kuiweka katika mtizamo itakua ni ngumu sana kwake kuelewa. Kwamba ni sababu ipi haswa iliyopelekea Serikali ya Markani kupiga hatua kubwa ya Teknolojia. Sababu haswa ya kupiga hatua kubwa ya mabadiliko ya teknolojia huko marekani imetokana na serikali hiyo kukutana na viumbe walio kua wakiishi ndani ya Dunia hii na Si nje ya dunia hii. Viumbe hao walitokea juu lakini wamekua wakikutana na serikali chini ya dunia na waliipa serikali ya marekani teknolojia ya hali ya juu kwa kubadilishana na miili ya wanadamu. Naam hivyo ndivyo serikali za dunia zinavyopata maendeleo makubwa ya teknolojia na ufahamu mwingi kwa ujumla katika muda mfupi tu wa takribani miaka 30.

HII UNAWEZA KUJIULIZA, Pamoja na Watu weusi/Wa Afrika kuishi na Anunaki uso kwa uso zama hizo, na kufundishwa maarifa mengi, mfano;- Unajimu, kilimo, Sayansi ya anga na aina zote za sayansi Lakini leo hii Mataifa ya Afrika yapo Chini kiteknolojia ikilinganishwa na mataifa ya Ulaya ya watu weupe, kumbe siri ni kwamba Wenzetu Wanasaidiwa na viumbe wasio wanadamu (ALIENS) Ambao wanaishi hapa hapa Duniani Chini Ya Ardhi. Teknolojia imekua kwa kasi mno katika kipindi cha miaka 30 ya nyuma, ambapo unaweza kuzungumzia ugunduzi namna unavyotaka lakini huwezi kutoka katika kuvuta gari na Farasi huko Wild Wild West hadi kurusha roketi angani bila msaada wa teknolojia. Msaada wenyewe ambao serikali iliyoupata ni kutoka mji wa ROSSWELL, uliopo huko kusini mashariki mwa New Mexico. Kuna nini huko RossWell?

Mji huo unafahamika zaidi kama eneo ambalo vifaa vya anga vya viumbe wa sayari ya nje, UFOs kugongana mwaka 1940. Sasa tukiangalia asili ya majina yaani Etymology, ya jina Rosswell, Well ni kisima kilichokua huko New Mexico ambacho kilichimbwa. Na Walivyo chimna walikutaba na viumbe wanaoitwa GREYS. Na hao Greys walikua aina ya viumbe ambao walitokea kwenye mfumo nyota unaoitwa ZETA RETICULI. Hii ndio sababu viumbe hao wanaitwa DRACO-ZETAS Kutokana na mfum nyota ZETA RETICULI. Sasa kwa kua sayari hiyo ya Zeta Reticuli inazinguka nyota yake pasipo kujisokota (Spin) na hivyo inakua katika sehemu ile ile lakini haizunguki nyota husika, hiyo inapelekea sehemu ya giza ya sayari hiyo kua na giza moja kwa moja na halikadhalika ile sehemu ya mwanga inakua na mwanga moja kwa moja. Ni kama mwezi kwenye dunia hivyo ndivyo sayari inavyo zunguka Zeta Reticuli kwa hiyo viumbe hao wanatokea kwenye sehemu ya Giza ya sayari inayo zunguka Zeta Reticuli. Sasa Greys ndio Jamii ya Draco lakii wao wanatokea mfumo nyota ZetacReticuli wakati Draco wanatokea mfumo nyota Draco Constellation ama Alpha draconis.

Mifumo hiyo nyota ndipo viumbe wote wa sayari ya nje ya dunia wanatokea mfano NOMMOS Miungu ya DOGON Wanaotokea mfumo nyota Sirius, kwenye kundi nyota CANIS MAJOR. Mifumo hiyo nyota mfano ORION na PLEIADES ama KILIMIA Kwa kiswahili pia imeongelewa kwenye Biblia.

AYUBU 38:31

Je, waweza kuufunga mnyororo wa kilimia, au kuvilegeza vifungo vya Orioni?.

AYUBU 9:8-9

Yeye afanyaye hizo nyota za Dubu na Orioni na hicho Kilimia, na makundi ya Nyota ya kusini.

.Soma pia AMOSI 5:8

Nimekuletea dondoo hiyo ya kwenye Biblia ili kukuthibitishia kwamba makazi ya viumbe hao pia yamejadiliwa kwenye Biblia. Lakini hii ni dondoo tu kwani makundi nyota hayo na matumizi yake kwenye Ukiroho wa Afrika (African Spirituality) na Kwenye nakala za Theolojia ya Unajimu.

Kuhusu ZETA RETICULI, mtaalamu wa mambo ya UFO, Bob Lazer, alielezea pia kwamba alikutana na kugusa UFO Inayosadikiwa kutoea kwenye mfumo nyota huo huku kukiwa pia na baadhi ya nyaraka ambazo zinaonyesha kwamba UFO hiyo ilitokea mfumo nyota huo, yaani Zeta Reticuli Sta System. Ambayo ilikua ni Sayari ya tatu katika mfumo nyota huo ambayo pia iliitwa ZB3.

ZETA RETICULI inaweza kua inafahamika zaidi kwani imekua sehemu ya mapokeo ya kileo ya UFO karibia tangu mwanzo, ikianzia na tukio la kwanza lililoripotiwa la utekaji unaohusu Alien (Alien Abduction). Inaelezwa kwamba, Barney na Bety Hill walidai kwamba,bwalitekwa na Aliens kwenye Vuli ya mwaka 1961 na Betty, akiwa katika hali kama ya kiini mach (Hypnosis), alichora Ramani ya sehemu wanayodaiwa kupelekwa.

(Picha ya Mfumo nyota Zeta Reticuli wanapotokea viumbe aina ya Greys nitaiweka Instagram)

Mnajimu mwanaridhaa aliyeitwa Marijorie Fish, alitumia miaka kadhaa akichambua ramani hiyo na kuhitimisha kwamba ilikua ni Ramani ya mfumo nyota wa zeta Reticuli (Zeta Reticuli System). kama jambo hilo ni kweli ama sio imekua ni mdahalo, huku Carl Sagan, akipinga jambo hilo kwenye kipindi cha Cosmos mwaka 1980. Lakini imekua ni kawaida kabisa kwa serikali kupitia vibaraka wake kukataa uwepo wa viumbe hao.

(Gazeti la kila siku Rosswell Daily Record likiwa na kichwa cha habari kinacho husu kukamatwa kwa kifaa cha angani (Flying saucer) kinacho tumiwa na Aliens huko Rosdwell, Unaweza kutafuta Google)

Tukiendelea na somo letu ambapo tuliona kwamba, viumbe hao wanaotokea gizani kutokana na nyota yao kuzunguka sehemu ya giza ya sayari inayozunguka Zeta reticuli.

Wametokea gizani ndio maana macho yao ni Makubwa sana kwa kua ilibidi wachkue kila mwanga wanaopata kama macho ya chura ambae muda wote hukaa mazingira ya gizani na unyevunyevu. Hivyo ndivyo namna umbo lao lilivyo na ndio maana hawawezi kustahimili kwenye mwanga wa Nyota.

Tukirudi Nyuma kidogo, Viumbe hawa wanaotokea chini ya Ardhi wao ndio ambao hufahamika kama Aliens. Kwa hiyo Greys ni Aliens ambao awali walitokea kwenye mifumo nyota ya sayari za nje ya dunia na sasa wanaishi Chini ya Ardhi na kutambulika kama Aliens. Sasa maswali yote ya kwanini alien hawaonekani hadharani kwenye uso wa Dunia mara kwa mara majibu yake ni kwa sababu wakikaa kwenye mwanga mkali watakufa, Fikiri tu kwamba Jicho lao moja Ni kubwa kuliko Sura zetu.

Macho yao yanakua kwenye hatari mno (Sensitive) kwenye mwanga na kwenye Joto kali.

Kwahiyo kama parasaiti wengine wanaokaa mazingira ya Gizani, Greys nao ni wanyonyaji asilia (Natural Parasites).. Fikiria kuhusu kupe, Kunguni na hata minyoo hawawezi kustahimili Joto na Mwanga. Mdudu yeyote mnyonyaji hawezi kustahimili vitu hivyo viwili.

Greys wanapo safiri kwenye sayari hii, wanaposafiri kwenda Maldek na Tiamat inabidi waende chini ya Ardhi. Inabidi waende chini ya Ardhi haraka kwasababu hawawezi kustahimili mwanga wa jua wa moja kwa moja. Mwanga wa jua badala ya kuwapa nishati unawaondolea nishati kwasababu ni viumbe wa Ulimwengu wa 5(5th Dimension) walioanguka kwenye Ulimwengu wa 3 (3th Dimension) yaani sayari ya Duna, muda uleule kama ilivyo tokea kwa Draconians.Greys ni wanyonyaji Asilia wa kuzaliwa. Ndio maana masuala mengi ya utekaji yanaongezeka Ulimwenguni kote kwasababu wanawatumia mateka kama sampuli za kuchanganya DNA zao na DNA za Caucasoids (Wazungu) na kutengeneza kitu Fulani Kinacho Itwa Black Eye Children.

TO BE CONTINUED
 
Back
Top Bottom