Alichosema Ismail Jussa

Well said Jussa, ukweli utabaki milele lakini chadema watajua kwamba hilo dude ni bovu baada ya uchaguzi...yaani ...nimecheka comment ya aina mkumbo ndio aina viongozi wa chadema tunaotegemea kuwapa nchi..waziri mkumbo ndio anaongea hivyo what a joke!

Chadema bado sana!
 

Ni vizuri tukaweka sawa rekodi hapa. Uchaguzi wa serikali za mitaa uliopita (mwaka jana tu ) Chadema ilishirika kikamilifu swa na CUF. Matokeo (Bara) CUF wameshika nafasi ya pili. Hapa Dar Es Salaam Chadema imeambulia viti vya mitaa 4 (vinne ) tu wakati CUF wamelamba zaidi ya viti 60 (sitini)

Kusema Lipumba kapata kura nyingi zanzibar ndio maana kawa wa pili sio sahihi pia. Uchaguzi wa mwaka 2005 Lipumba kapata kura 1.3m kati ya hizo za zanzibar hazifika hata laki 2 kwani waliopiga kura zanzibar ni watu 460,000 tu assuming more than half walimpa Kikwete then Lipumba abaki chini ya laki 2

Nilitaka kuweka sawa hilo tu......
 
dah, yaani slaaa amuunge mkono lipumba?

mnaleta mzaha?!!

sla yuko juu ya huyu lipumba , na hili ndilo tatizo la cuf, wanategema mtu mmoja kama ulimi
 
Jusa anaweza kusema yote lakini it's a known fact that the mainland has never been their priority. Wanaona kuwa hawapotezi kitu huku bara, ndiyo sababu pamoja na kuwa zaidi ya nusu ya kura za urais alizopata Lipumba 2005 zilipatikana bara, kiasi cha ruzuku wanachopewa bara ni kichekesho ukilinganisha na kile kinachobaki visiwani.
Hofu yao kubwa ni kuwa chama kikipata nguvu bara kuna hatari ya wapemba kukosa sauti ndani ya chama hicho na msimamo wa Prof Safari katika hilo ndio uliomkosesha uenyekiti na si kama Jusa anavyotaka tuamini. Jusa ni kiongozi wa ngazi ya juu CUF, anayoandika wengine tunayachukulia kama msimamo rasmi wa chama chake, hivyo CHADEMA wasipuuzie mashambulizi haya. Ni vema kupitia wanachama wao wanaoifahamu vizuri CUF kama Lwakatare wakatueleza ni kwa nini tupuuze madai kama haya kwa kueleza ukweli ulivyo ndani ya chama hicho.

Si siri tena kuwa kwa sasa kuna mkakati baina ya CCM na vyama hivi vingine kuhakikisha kuwa CHADEMA haifanikiwi. Rejea kauli ya Mrema na waraka wa Vatican kuhusu Dr Slaa!
 
Hii makala imenikumbusha wale wote ambao huwa na tabia ya kudharau watoto. Eti hana ozoefu, kichekesho na maneno yaliyopitwa na wakati.

Kuna jamaa alishasema kuwa alipokuja Wayne Rooney, kijana mdogo kabisa na wala hakuhitaji afundishwe miaka kibao kufunga magoli. Au una kipaji cha kufunga au huna. Lipumba miaka yote hiyo, zaidi ya kugombea Urais, kafanya nini?

Kikwete alikuwa na uzoefu sana mambo ya nje na hasa kuomba misaada, kazi ambayo kaendelea kuifanya hata baada ya kuwa Rais.

Dr. Slaa ni mtu makini na mtu anayetaka mambo/nchi yaende kwa kuongozwa na siyo kuweka Autopilot.

Tunahitaji mtu atakayetimiza na kuturudisha kwenye maneno ya wimbo wa Babyface:

YouTube - Babyface - Simple Days

Bring back those simple times of yesterday
When a man was a man
And a friend was a friend
Bring back those simple times of yesterday
When you said what you meant
And you meant what you said ................


 
Jusa anaweza asiwe sahihi sana, lakini na wengi wanaomshambulia nao wanakwenda siko na ni kwa kigezo hicho CCM itaendelea kupeta.

Kama kungekuwa hakuna kudharauliana na kuna strategy ya upinzani ya pamoja, suala la Urais wangekubaliana kuliacha kwanza, kila chama kiende kivyake, wajikita zaidi na Ubunge na kila chama kusimika wabunge maeneo yenye ushawishi mkubwa. Jiji kama Dsm wapinzani wanaweza kupata viti alau vinne. CUF watumie nguvu nyingi Temeke na Kigamboni na Chadema Ubungo na Kawe/Segerea. CCM haiwezi kukubali Ikulu (Ilala) iende upinzani piga ua.

Lakini ni kwa dharau kama hizi ndio NCCR na Chadema mwaka 1995 walikataa kushirikiana na CUF kutengeneza kambi ya upinzani bungeni kwa madai kuwa NCCR ndio walistahili kutengeneza kambi ya upinzani kwa kuwa na wabunge 17 wa Bara. Kambi ikaundwa na CUF na UDP. Tazama kilichofuatia 2000 na 2005 kwa wabunge wa vyama hivyo na still Chadema (ya sasa) wanakiona CUF kama chama dhaifu.

Kwangu mimi neither Lipumba nor Slaa ninaamini atatoa upinzani mkali kwa JK. Pengine tujikumbushe upinzania alioutoa Mrema na wapi alipoishia.

Mazingira na wananchi wa Tanzania hawaonyeshi kwamba upinzani strong utatoka CUF pekee au Chadema pekee bali coordinated strategy/efforts. Mkakati wa kwanzani uwe Ubunge. Chadema iwekeze vya kutosha (kwa pesa, zana na nguvu kazi) kanda ya kaskazini na Nyanda za Juu Kusini. CUF iwekeze ukanda wa pwani na Zanzibar. Kanda ya ziwa na Dsm waachiane majimbo. Magharibi: Tabora iwe CUF, Kigoma iwe Chadema; Kanda ya Kati pia waachiane majimbo. Sio lazima kuachiana kuwe sawa kwa sawa bali kulingana na nguvu ya chama mahala hapo.

Mkakati wa pili ni Urais: Baada ya kujenga nguvu bungeni, wapinzani wanatafuta mtu anayekubalika kwa wananchi na pande zote kisha hao viongozi wawe nyuma yake. Asimame chini ya chama gani itategemea na chama kinachokubalika zaidi wakati huo.

Haya yatawezekana endapo kuna nia njema kwa wahusika.
 
Hujajibu hoja mkuu. Ungefanya jambo la busara sana kama ungejibu hoja kwa vigezo vinavyofanana na jinsi jamaa alivyoandika na si majungu. Mfano, jamaa kasema uchguzi wa serikali za mitaa CUF ndo ilikuwa ya pili bara baada ya CCM, sasa na wewe labda sema CHADEMA ilikuwa hivi na vile...... CUF ni chama cha kileberali na chadema hawaeleweki na wewe sema chadema ni mlengo fulani, si masuala ya kuleta porojo humu mara kajiunge na hizbula, mara nini. Yo wrote non sense man, I'm sorry
 


Asante niliyokupa ni ya content pamoja na mpangilio mzima wa majibu yako mkuu!

Posts nyingine zaweza kuwa nzuri lakini mtu akashindwa kuzisoma kwa jinsi zilivyokosa mpangilio; big up bro!
 
Onother UMBEYA/MAJUNGU. unajua ruzuku wanayopata CUF?
 
Sasa mlimtegemea huyu Mheshimiwa Jussa aseme nini? Yeye ni mwanachama wa CUF na anataka chama chake kishinde. Mpingeni hoja zake kama alivyofanya Mkandara na si kuingiza mambo ya kutupiana matope.

Amandla.....

Yaani ingekuwa watu wengi humu JF ni kama wewe, nafikiri ingekuwa raha saana. Nakupa 5 mkuu..
 
..lakini Jussa anamchukulia Maalim Seif kama Mungu mtu.

..sitegemei kiongozi yeyote yule wa upinzani aeneze kampeni chafu namna hii dhidi ya chama kingine cha upinzani.

..kama hawakubaliani, that is fine, lakini siyo waanze kupakaziana masuala ya ukabila,udini, etc etc.

..jambo lingine la ajabu sana ni kwamba Jussa anadharau uzoefu wa miaka 15 wa Dr.Slaa kama mwakilishi wa Karatu ktk wa bunge la Muungano.
 

Penye rangi: Yeah, angetaja kwa mfano CUF ilitoka kapa kabisa katika viti vya Ubunge huku Bara mwaka 2005 na kwamba hiyo 'ndoa' yao na CCM imekiweka chama hicho ktk hali ngumu kwani kinaonekana kuelekea kwenye u-CCM-B na huenda kikapoteza kura nyingi pamoja na madiwani.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…