Alhamisi nitakuwa Lusaka Jumapili Windhoek

Alhamisi nitakuwa Lusaka Jumapili Windhoek

Emma Simbo

Member
Joined
Jan 28, 2018
Posts
44
Reaction score
15
Wakuu kwema humu ndani? wale diaspora wa nchi za kusini mwa Tanzania hasa Namibia, Botswana na South Africa nawasalimu saana na siishii kuwasalimu ila naombeni mtupe mawili matatu watanzania wenzenu tunaohitaji kuja humo.

Mimi kiukweli kesho kutwa nitakuwa huko Windhoek labda bahati iso njema kwangu itokee nisifike. Siji kutembea nakuja kutafuta. watanzania waliopo huko mtakuwepo tu humu ndani kwa nchi ya botswana Namibia na South Africa.

Vipi nchi gani inaunafuu kuizidi nyingine kifursa kwa kijana kuhangaika. Madili ya ngada msinipe sitaki hata kuyasikia. Ukimwi nao nimeambiwa upo sina ulevi wa wanawake nitajilinda.

Sasa wapi pana unafuu? Namibia?botswana au SA? tusibaniane wakuu tupeane nyeusi nyeupe.

1. Yellow card ninayo
2. Pass kubwa ipo

Kilichobaki ambacho mtanisaidia ni sababu ya safari nisije rudisha mpakani.asanteni.
 
Watakuja mkuu pia jaribu kupitia uzi zinazolandana na hizi humu jukwaani
 
ukifika botswana niite na mm mkuu!tutafute wote aisee !hali hii sio jaman!
 
Hizo Nchi hasa Botswana,SA na Namibia wanataka watu wenye ujuzi kidogo hasa ufundi Magari, umeme ,kupaka rangi au kutengeneza matatizo ya engine...kwa hii SA ndio ukitilia Magari ya ajali mengi yanataka kunyoshwa yauzwe maana wengi wananunua katika mnada na kuuza likishapona ili maisha yaende hasa Pretoria na Johannesburg huko kwingine unaweza kufanya ila kipato na idadi ya Magari sio mengi ya kutengeneza kama kwa kaburu...Usijihusishe na kuvunja sheria unga,bangi na madudu mengine au kuvunja na kuiba utapotea jela maana hawacheleweshi kufunga huko na pia usideal kabisa na gari za wizi wana mtandao mmoja wa kukamata...
 
Hizo Nchi hasa Botswana,SA na Namibia wanataka watu wenye ujuzi kidogo hasa ufundi Magari, umeme ,kupaka rangi au kutengeneza matatizo ya engine...kwa hii SA ndio ukitilia Magari ya ajali mengi yanataka kunyoshwa yauzwe maana wengi wananunua katika mnada na kuuza likishapona ili maisha yaende hasa Pretoria na Johannesburg huko kwingine unaweza kufanya ila kipato na idadi ya Magari sio mengi ya kutengeneza kama kwa kaburu...Usijihusishe na kuvunja sheria unga,bangi na madudu mengine au kuvunja na kuiba utapotea jela maana hawacheleweshi kufunga huko na pia usideal kabisa na gari za wizi wana mtandao mmoja wa kukamata...
Asante saana Mkuu isanga nitayazingatia yote uliyonieleza.
 
Mkuu nauli kutoka Lusaka mpaka Windhoek ni sh.ngapi
 
Hizo Nchi hasa Botswana,SA na Namibia wanataka watu wenye ujuzi kidogo hasa ufundi Magari, umeme ,kupaka rangi au kutengeneza matatizo ya engine...kwa hii SA ndio ukitilia Magari ya ajali mengi yanataka kunyoshwa yauzwe maana wengi wananunua katika mnada na kuuza likishapona ili maisha yaende hasa Pretoria na Johannesburg huko kwingine unaweza kufanya ila kipato na idadi ya Magari sio mengi ya kutengeneza kama kwa kaburu...Usijihusishe na kuvunja sheria unga,bangi na madudu mengine au kuvunja na kuiba utapotea jela maana hawacheleweshi kufunga huko na pia usideal kabisa na gari za wizi wana mtandao mmoja wa kukamata...
Shida SA makaratasi ya kazi wanabana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom