johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 83,968
- 141,977
Akihutubia kama mgeni rasmi katika ufunguzi wa shule ya Range Primary & Sec school mjini Ilula RC mstaafu Albert Chalamila amesema yeye amesoma UDSM kwa miaka 7 na ana degree, post graduate diploma na Masters za kutosha hivyo hana njaa.
Chalamila amesema viongozi wengi wakiteuliwa wanaendekeza wizi wa mali za umma ili wasistaafu wakiwa maskini lakini yeye hakuwa mmoja wao kwa sababu elimu yake ni mtaji.
Chalamila amewataka wanafunzi kuzingatia masomo wawapo shuleni na wasiendekeze makundi, ndio maana hata yeye alipokuwa RC wa Mbeya aliwachapa viboko wanafunzi waliochoma mabweni
Jumaa kareem!
Chalamila amesema viongozi wengi wakiteuliwa wanaendekeza wizi wa mali za umma ili wasistaafu wakiwa maskini lakini yeye hakuwa mmoja wao kwa sababu elimu yake ni mtaji.
Chalamila amewataka wanafunzi kuzingatia masomo wawapo shuleni na wasiendekeze makundi, ndio maana hata yeye alipokuwa RC wa Mbeya aliwachapa viboko wanafunzi waliochoma mabweni
Jumaa kareem!