beevenom
JF-Expert Member
- May 1, 2017
- 313
- 428
Wandugu habari zenyu! Niende moja kwa moja katika mkasa huu, nina Dada yangu wa damu kabisa miaka hiyo akajichanganya kwa dume la kutoka Iringa sasa kasheshe jamaa ni mtata haswaa,hakuhitaji ndugu yeyote nyumbani kwake kutoka kiumeni hiyo haikuwa shida sana. Sasa mama yetu alienda kumuuguza binti yake baada ya kujifungua daaaah naamini mpaka anaingia shimoni hatomsahau mkwewe maana si kwa matusi aliyotukanwa. Tukasema so shida hatutafika kwake.
Sasa Dada yetu ilikuwa haambiwi kuhusu huyo kamanda wake. From no where miaka kama sita imepita Dada akaja kasi mno kutaka talaka kunusuru maisha yake kwani aliomba sana support kutoka kwa ndugu zake. Mie nikawaambia huyu ndugu yetu mna uhakika kuwa anamainisha akaapa miungu yote haya ya majini kuwa yeye na jamaa basi. Mahakamani mambo yakaiva Mara talaka paaah! mezani dada huyo kwa wazazi. Familia ikamshauri apewe mtaji aingie katika kilimo,akaanza fresh kabisa na akapata mavuno mazuri.
Acheni mapenzi yaitwe mapenzi,tunashangaa ghafla bini vuuu binti kaenda kwa x mumewe kinyemela akiulizwa anasingizia watoto,tukasema sio kesi cha kufanya aende mahakamani kwa taratibu zaidi akaona tunamzingua akaendelea na mmewe kibishi. Sasa kumbe jamaa yake anavuta bangi sana na kibaya zaidi kagombana na majirani zake wote. Sijui shetani au Mungu jamaa alijichanganya akapanda mmea nyuma ya nyumba yake na majirani kwa hasira wakawatonya vijana wa lugola mara paap Dada yetu akapigwa bangili za chuma lupango na mmewe akasakwa naye ndani. Akiulizwa Mara ooh mi sikujua kuwa no bange. Kituko zaidi katika kumsechi mmewe akakutwa na pesa kama laki mbili na nusu. Jamaa wakamwambia ajichange kama mia tatu hivi wawatoe kabla mambo hayajavunda mmewe kwa mbwembwe akasema sitoi pesa kama vipi waende kwa pilato.
Kama mzaha kesi ikaanza kuunguruma Mara kooooooti Dada mwaka mmoja ndani au faini na jamaa anangojea kusomewa next week. Kituko sasa jamaa lake haya kujichanga au liuze hata nyumba hamna. Sasa wadau ushauri unahitajika hapa na ikumbwike wiki moja iliyopita jamaa alituma mwseji ya matusi mazito kwa familia yetu,yaani inatia kichefuchefu kabisa. Jamani nyie wanawake nani kawaroga wandugu yaani hata kutumia robo tu ya ubongo ni ngumu? Ukizingatia kipindi chenyewe hiki cha herode sijui
Sasa Dada yetu ilikuwa haambiwi kuhusu huyo kamanda wake. From no where miaka kama sita imepita Dada akaja kasi mno kutaka talaka kunusuru maisha yake kwani aliomba sana support kutoka kwa ndugu zake. Mie nikawaambia huyu ndugu yetu mna uhakika kuwa anamainisha akaapa miungu yote haya ya majini kuwa yeye na jamaa basi. Mahakamani mambo yakaiva Mara talaka paaah! mezani dada huyo kwa wazazi. Familia ikamshauri apewe mtaji aingie katika kilimo,akaanza fresh kabisa na akapata mavuno mazuri.
Acheni mapenzi yaitwe mapenzi,tunashangaa ghafla bini vuuu binti kaenda kwa x mumewe kinyemela akiulizwa anasingizia watoto,tukasema sio kesi cha kufanya aende mahakamani kwa taratibu zaidi akaona tunamzingua akaendelea na mmewe kibishi. Sasa kumbe jamaa yake anavuta bangi sana na kibaya zaidi kagombana na majirani zake wote. Sijui shetani au Mungu jamaa alijichanganya akapanda mmea nyuma ya nyumba yake na majirani kwa hasira wakawatonya vijana wa lugola mara paap Dada yetu akapigwa bangili za chuma lupango na mmewe akasakwa naye ndani. Akiulizwa Mara ooh mi sikujua kuwa no bange. Kituko zaidi katika kumsechi mmewe akakutwa na pesa kama laki mbili na nusu. Jamaa wakamwambia ajichange kama mia tatu hivi wawatoe kabla mambo hayajavunda mmewe kwa mbwembwe akasema sitoi pesa kama vipi waende kwa pilato.
Kama mzaha kesi ikaanza kuunguruma Mara kooooooti Dada mwaka mmoja ndani au faini na jamaa anangojea kusomewa next week. Kituko sasa jamaa lake haya kujichanga au liuze hata nyumba hamna. Sasa wadau ushauri unahitajika hapa na ikumbwike wiki moja iliyopita jamaa alituma mwseji ya matusi mazito kwa familia yetu,yaani inatia kichefuchefu kabisa. Jamani nyie wanawake nani kawaroga wandugu yaani hata kutumia robo tu ya ubongo ni ngumu? Ukizingatia kipindi chenyewe hiki cha herode sijui