AKA KABINTI SPECIAL VIPI TENa

AKA KABINTI SPECIAL VIPI TENa

BABU KIZEE

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2013
Posts
452
Reaction score
72
Nina mpenzi wangu tumekuwa nae muda mrefu bila kupeana wet kiss leo nikataka kujaribu kumkiss nikakutana na harufu fulani ambayo sikuipenda na nikazuga nimesahau kitu fulana ili kuepukana na hali hiyo, naomba kuuliza wakuu hivi hii hali husababishwa na nini na anaweza tibika huyu. Kwa mtazamo wake tu yuko smart lakini hali yake hiko hivyo, natanguliza shukrani kwa ushauri mtakanipa.
 
Asipotibika ndio itakuwa mwisho wenu...........

Hapo ni usafi wa kinywa pia wahitajika
 
Mmmmh simple issue afanye Usafi wa kinywa kwa kujua jinsi ya kusukutua meno pia mswaki abadili mara kwa mara within 3 month,kwa siku asubuh na jioni aswaki pia akiweza kila baada ya kula kwa kutumia dawa za alovera au synsodne pia kuna ya kusukutua/ spray ya mdomo

Au mpeleke kwa docta aangaliwe
 
Kabla ya kukujibu imebidi nipigwe na butwaa

Kwa kweli inatibika bila ya wasi muhimu kuswaki japo mara tatu kwa siku, kusugua ulimi hadi ndani kwa chini karibu na kolomelo, tena ajitahidi sana kuuzungusha mswaki kila kona ya mdomo kwa ndani, bila ya kusahau mashavuni, ikiwezekana kila baada ya mlo, asipokuwa karibu na mswaki, ajitahidi kusukutua mara kwa mara

Anaweza tumia mouthwash pia kabla au baada ya kuswaki, lakini akumbuke mouthwash haitomsaidia kwa kutwa nzima inaweza kusaidia kuzuia kaharufu kwa muda wa nusu saa baada ya hapo hali ya kawaida inarudi

Kama ujuavyo mdomo una bacteria wengi sana

Hebu jaribu haya machache halafu uje kutupa maendeleo yakoje

Kama hakuna mabadiliko inaweza kuwa hako kaharufu kanatokea tumboni hapo anahitaji kwenda kumuona daktari haraka iwezekanavyo
 
mpeleke kwa madaktar wa meno watamsaidia inatibika kabisa hiyo.
 
na wewe mtoa mada unahitaji:help::help😛ia
 
Dawa ni ni mswaki kutwa mara tatu kama doz na umwambie ili ajijue inawezekana akawa hajui
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom