Ajira za walimu wapya wa Sayansi na Hisabati pamoja na Mafundi sanifu wa maabara

Abuwhythum

JF-Expert Member
Jan 7, 2015
837
494
Serikali kupitia kwa Waziri wa Utumishi wa umma na utawala bora ilitangaza kuwa mwezi ujao inategemea kuajiri walimu wa sayansi na hisabati pamoja na Mafundi sanifu wa maabara ambao kwa ujumla wao ni 4348.

Izingatiwe kuwa hadi tangazo hilo linatoka waziri husika alisema walimu wa sayansi waliotuma maombi (izingatiwe muda ulishaisha) ni 2,100 mafundi sanifu wa maabara wanaendelea kutuma vyeti hadi tarehe 20/02 lakini serikali tayari inajua idadi ya watu itakaowaajiri.

Swali langu ni je huu uhakiki wa vyeti una lengo la uhakiki kweli? Au nikuendelea kuchelewesha muda wa kutoa ajira na stahiki nyingine za walioajiriwa tayari?

Mafundi sanifu ni wachache sana wakilinganishwa na Walimu wa sayansi na hisabati, cha kushangaza wamepewa takriban mwezi mzima kuwasilisha vyeti ika Walimu walipewa siku tano tu! Hapo bado majina ya ajira zao walimu na mafundi sanifu watataka wayatoe kwa pamoja! Kumbukumbu hapo bado hawajawaongezea muda! Kweli hata kama ni mtoto mdogo ukiwa muongo kwa visingizio ambavyo havina msingi atakugundua tu!

Katika suala hili la ajira wanaosubiri wote hakuna kuamini cha nani wala nani! Haoa cha kuamini ni pale tu majina watakapowekwa kwenye tovuti ya TAMISEMI, ukaripoti na ukaona mshahara wako wa kwanza umesoma kwenye akaunti haya mengine yoooote! HAKUNA CHA MSEMA KWELI wala vha nani!
Hata huo mwezi wa tatu uliosemwa tena mbele ya Bunge tukufu usiamini sana kwa sababu hata Jaffo alitamka mbele ya Bunge tukufu kuwa ajira za walimu (tena wote) ni Mei lakini ni miezi 10 sasa hakuna lolote tunaloliona.

Msemaji mwingine akasema ajira zinasitishwa kwa mwezi mmoja na nusu haitazidi miezi miwili, toka amesema hayo ni miezi 8 sasa hakuna lolote.
Hata anayekwambia March Usishangae inapita hivi hivi.

Sema tu hali hairuhusu ika wahusika wote tungefanya maamuzi magumu ya kutofika tutakakopangiwa kwa kisingizio tumeshapata kazi nyingine. Akili ingewasogea na huu ufisadi usingetokea tena. Japo wana kiburi kuwa kuna wahitimu wa wengine wa 2016 wapo mtaani.
 
Porojo nying kila mtu anasema yake, Tanzania imekuwa kama familia zao ktamka watakavyo hafu hakna utekelezaj, mi stak kabsa hata kusikia habra za mawazr na wakuu wa nchi, siasa kila kitu wakat watu wanaumia!

Utumishi,Tamisem, Elimu,wazr mkuu na mkuu wa kaya hakna anaeaminika wote blaa blaa nying, matamko na makanusho yamewajaa, dhambi ya kusema uongo haiepukiki kwao!
 
Porojo nying kila mtu anasema yake, Tanzania imekuwa kama familia zao ktamka watakavyo hafu hakna utekelezaj, mi stak kabsa hata kusikia habra za mawazr na wakuu wa nchi, siasa kila kitu wakat watu wanaumia!

Utumishi,Tamisem, Elimu,wazr mkuu na mkuu wa kaya hakna anaeaminika wote blaa blaa nying, matamko na makanusho yamewajaa, dhambi ya kusema uongo haiepukiki kwao!
Mungu anawaona jamani
 
Porojo nying kila mtu anasema yake, Tanzania imekuwa kama familia zao ktamka watakavyo hafu hakna utekelezaj, mi stak kabsa hata kusikia habra za mawazr na wakuu wa nchi, siasa kila kitu wakat watu wanaumia!

Utumishi,Tamisem, Elimu,wazr mkuu na mkuu wa kaya hakna anaeaminika wote blaa blaa nying, matamko na makanusho yamewajaa, dhambi ya kusema uongo haiepukiki kwao!
hii serikali ni ya watenda dhambi:(
 
Wazalendo wa kweli tukiliongelea Swala hili,kunawatu wanadai Wa-Tanzania ni watu wakulaumu/lawama.

Na Mfumo wetu mbovu wa Elimu wahitimu wamekaa Mtaani wamechoka wengine wamechakaa vilivyo lakini chakushangaza bado Kuna baadhi wanaimani na Serikali hii, viongozi wamekuwa wakipishana kauli na hawasimamii kile wanachokiongea.
UOGA umetujaa na kinachokosekana ni ujasiri tu wakuamua.

"Taifa la kondoo huendeshwa na serekali ya dubu"
 
Wazalendo wa kweli tukiliongelea Swala hili,kunawatu wanadai Wa-Tanzania ni watu wakulaumu/lawama.

Na Mfumo wetu mbovu wa Elimu wahitimu wamekaa Mtaani wamechoka wengine wamechakaa vilivyo lakini chakushangaza bado Kuna baadhi wanaimani na Serikali hii, viongozi wamekuwa wakipishana kauli na hawasimamii kile wanachokiongea.
UOGA umetujaa na kinachokosekana ni ujasiri tu wakuamua.

"Taifa la kondoo huendeshwa na serekali ya dubu"
poleni vijana,kuweni wavumilivu,mungu atawasaidia
 
Ndio nimesoma hapa juu ya ajira za fundi sanifu. Naomba uhakika wa hilo watu waaply
 
Inauma xna hii serikal ya aina yake asee, porojo nyingi sana, cyo mawaziri, cyo sizonje hakuna kitu blabla nyingi sana wao wenyewe wanapishana kauli, kwa kweli hadi ajira zitoke lazima kuna watu watapata magonjwa kutokana na msongo wa mawazo.
 
Ingetokea hukumu ya moto ikawa leo......Mwenyezi Mungu angeanza na kuwaadhibu watawala wa Tz kwa dhambi kubwa ya UONGO. Sio mkulu wala nani,,,,wote ni wale wale,......
Anyway......nipo mbioni kufungua kesi ya madai dhidi ya siri kali, kwa kuwapotezea vijana muda wao mwingi (wa kuwa masomoni & mtaani). Hii haikubaliki kabisa, watawala wanatengeneza taifa la watu waongo tuu,,,,kama viongozi wakuu wa nchi wanakuwa waongo namna hiyo, tena wakiwadanganya raia wao bila kupepesa macho wala kuwa na japo lepe na aibu....then tutegemee nini kwa raia....wao si ndo UONGO ndio utakuwa ni ukweli wao..!!!!

Mubadirike viongozi wa nji hiii...........wacheni uongo.............uongo ni dhambi kubwa saaaana.......na kwa hakika dhambi hii mnayoipanda, itawagharimu sana. Pia italipeleka taifa hili pabaya mno, maana mbegu mliyoipanda/mnayoipanda ni mbegu ya uharibifu, mtajuta........kwani hakuna marefu yasiyokuwa na ncha. Your days are coming.
 
Na wale walimu wa sayansi walioambiwa watume vyeti awamu ya pili (january 12_17) kwa kigezo eti walikosea awali mbona hatupati mrejesho??? au ilikua kiini macho kutuhadaa wahanga wa ajira!!!
 
hakuna ajira mpaka mwaka mpya wa fedha. hata uhakiki wa vyeti tuliouitisha ulikua ni uhakiki wa uongo kwa ajili ya kuwalaghai walimu wa sayansi waliokua wamekata tamaa na kutaka kwenda kuweka mikataba ya kudumu ktk shule za 'private' wasiende kuweka mikataba hiyo na watusubiri mpaka tutapotaka kuajiri.
mtaniamini mimi kama nimewadokezea kweli, pale mtapoona walimu wote wasayansi wameajiriwa huku kukiwa hakuna aliyeenguliwa kwa kukosa sifa kama tulivyosema "tunahakiki ili kutafuta wahitimu wenye sifa za kuajiriwa na serikali", huku tukiwa hatujataja hata sifa tunazozitaka. mfano kama tungekua tunataka wenye sifa fulani, basi tungetaja sifa hizo na tungewaambia wasio na sifa hizo wasijisumbue. kwamfano tungesema wenye GPA ya kuanzia X na wenye ufaulu kuanzia Y ktk shule za vidato ndio watume vyeti.
natumaini mmenielewa.
 
Back
Top Bottom