Wakuu,
Hizi ajali ni za kujitakia. Zinaweza kuzuilika watendaji wetu serikalini wakiamua. Ukiangalia kwa hesabu za haraka haraka hilo basi lilikuwa limebeba zaidi ya abiria 80 wakati uwezo wake hauapashwi kuwa zaidi ya abiria 60.
Je ni kwa nini askari wa usalama barabarani wanaruhusu magari ya safari ndefu kubeba abiria zaidi ya idadi inayokubalika?
Kamanda Mwema upo hapo. You need to act before any more tragedy is added to the list.
Tiba angalia hiyo alama nyekundu hapo juu, Tatizo sio askari wa uslama barabarani kwani kuna vitu vingi vinachangia.kama ifuatavyo
- Ubovu wa gari yenyewe hii inasabisha ajali sana
- Mwendo kasi hii ndio usiseme kwani inachangia kwa kasi kuteketeza ndugu zetu kwani mwendo wa kasi na huku gari bovu matokeo yake ajali.
- Abiria.abiri anashabikia mwendo wa kasi wa gari hata bila kumkanya dereva
- Hii ndio muhimu sana Expire Tyres matairi yanakuwa yameisha muda wake wa matumzi hata kama ni jipya hii ingekuwa inaangaliwa sana ajali nyingi za kupasuka matairi zisinge kuwepo kabisa kwani tairi likiwa limeexpire basi ujua halina muda litapasuka hata kama ni jipya hii sheria hapa inatakiwa iangaliwe kama unahitaji notice zaidi nenda google search expire tyre utaona maelezo
- Dereva anachangia pia kwa kuna mtu anamambo yake kichwa sasa anakuwa confused.
- Hii ni TBS walitakiwa waweke utaratibu wa kukagua magari mara kwa mara Pia hawa wanasababisha kwa uzembe
- Mwisho sasa ndio Traffic wanasabisha kwa interest zake tu.
Kwahiyo sio traffic anasababisha ok wandugu ni pamoja na vitu hapo juu
Jamani poleni sana