Ajali ubungo terminal

Ajali ubungo terminal

cr9

Senior Member
Joined
Oct 13, 2010
Posts
185
Reaction score
103
Leo asubuhi kumetokea ajali Ubungo Terminal ndani ukuta umeangukia magari yaliyokuwa parking. Bado haijafahamika magari mangapi yamehusika na ajali na kama kuna watu wamejeruhiwa vibaya au kifo. Polisi ndiyo wanaingia sasa hivi.

attachment.php
 

Attachments

  • ubung.jpg
    ubung.jpg
    14.7 KB · Views: 1,778
Pole wahanga, yaani lijiukuta limejiporomokea tu
 
Ni dhahiri ujenzi ulikuwa umechakachuliwa! Na faida yake ndiyo hivyo.

Poleni wahanga wote wa tukio hilo!
 
Zaidi ya magari 20 yameangukiwa na huo ukuta.. Source..Choice FM..
 
Magari 24 ndiyo yamekuwa chapati kwa mujibu wa Kamanda Charles Kenyela
 
Pole sana waliojeruhiwa na kuharibikiwa na magari. Uzembe huu katika ujenzi CRB na ERB muufanyie kazi
 
Katika hili ni busara kama wakimalizana mahakamani maana haya magari yapo kwenye parking iliyo salama..!
 
Leo asubuhi kumetokea ajali ubungo terminal ndani ukuta umeangukia magari yaliyokuwa parking. Bado haijafahamika magari mangapi yamehusika na ajali na kama Kuna watu wamejeruhiwa vibaya au kifo. Polisi ndiyo wanaingia sasa hivi

kwa wenzetu kama uchina hapo mkandarasi na vibarua walio jenga wangekuwa tayari wapo nyuma ya nondo wanasikilizia hatima yao aidha kunyongwa au jela
 
kazi ya Mungu haina makosa

Kwa wenzetu waliondelea na wenye demokrasia hawana kipengele hicho kwenye man made disasters.. Hapo kuna uzembe umefanyika na ni lazima watu wawajibike.. Sheria ichukue mkondo wake..
 
Zaidi ya magari 20 yameangukiwa na ukuta huo, source: ITV BREAKING NEWS.
 
Back
Top Bottom