Kumetokea ajali maeneo ya Ruvu baada ya basi lililokuwa linatokea Mbeya linalojulikana kwa jina la Ilasi kugongana uso kwa uso na lorry lililobeba unga la Azam lililokuwa linatokea DSM. Inasemekana ajali hiyo imetokana na lori lililokuwa linajaribu kulipita basi hilo kutaka kugongana uso kwa uso la lori lililobeba unga ndipo lori lililobeba unga likaelekea upande lilipo basi. Mpaka sasa hakuna habari yo yote kuhusu vifo au majeruhi ila abiria wametapakaa unga kiasi cha kushindwa kutambuana.