Rogie
JF-Expert Member
- Nov 22, 2010
- 7,600
- 6,721
Kuna ajali imetokea muda huu njia panda ya Mabibo ikihusisha gari aina ya Toyota Land Cruiser kumgonga mpita njia.
Jinsi Ilivyokuwa
Nimetokea zangu Sinza nikielekea Mabibo, baada ya kupita Shekilango na kuvuka bumps la kwanza maeneo ya Big Brother hiyo gari ilifunga breki za ghafla sana nyuma yangu, dereva akaamia upande wa pili akifuatiwa na pikipiki (boda boda) nyingi sana zikimfukuza coz nilikuwa nimefunga vioo sikuelewa nini wanaongea. Mara ghafla kukatokea foleni hapo njia panda, niliposhusha kioo nikaona kuna gari inatoa moshi mbele hivyo kufanya gari zilizokuwa nyuma yake kuhepa kwa pembeni nami nikahepa, kufika mbele ya hiyo gari nakuta zile pikipiki na madereva boda boda wakisema dereva wa gari alipotoka amegonga mtu, kuangalia vizuri hapo kwenye njia panda pia kamgonga mtu mwingine ambaye inasadikiwa amefariki.
Sikuweza kupata picha nzuri zaidi nilihofia kuweka Flash On kwa maana vijana wa boda boda walikuwa na hasira wakivunja vioo vya hiyo gari mikahofia usalama wangu.
Aliyegongwa hapo njia panda ni mwanaume umri wa makamo . Dah kwa mara ya kwanza nashuhudia pumzi ya binadamu inakatizwa ndani ya sekunde.
Jinsi Ilivyokuwa
Nimetokea zangu Sinza nikielekea Mabibo, baada ya kupita Shekilango na kuvuka bumps la kwanza maeneo ya Big Brother hiyo gari ilifunga breki za ghafla sana nyuma yangu, dereva akaamia upande wa pili akifuatiwa na pikipiki (boda boda) nyingi sana zikimfukuza coz nilikuwa nimefunga vioo sikuelewa nini wanaongea. Mara ghafla kukatokea foleni hapo njia panda, niliposhusha kioo nikaona kuna gari inatoa moshi mbele hivyo kufanya gari zilizokuwa nyuma yake kuhepa kwa pembeni nami nikahepa, kufika mbele ya hiyo gari nakuta zile pikipiki na madereva boda boda wakisema dereva wa gari alipotoka amegonga mtu, kuangalia vizuri hapo kwenye njia panda pia kamgonga mtu mwingine ambaye inasadikiwa amefariki.
Sikuweza kupata picha nzuri zaidi nilihofia kuweka Flash On kwa maana vijana wa boda boda walikuwa na hasira wakivunja vioo vya hiyo gari mikahofia usalama wangu.
Aliyegongwa hapo njia panda ni mwanaume umri wa makamo . Dah kwa mara ya kwanza nashuhudia pumzi ya binadamu inakatizwa ndani ya sekunde.