Ajali mbaya hapa Bwawani Mkoa wa Pwani

Ajali mbaya hapa Bwawani Mkoa wa Pwani

Magu

Senior Member
Joined
Jun 13, 2011
Posts
156
Reaction score
56
Kuna ajali mbaya iliyohusisha malori mawili moja likiwa tanker ya mafuta na lori la mizigo.

Katika ajali hii njia imejifunga mana lori la mizigo limekata barabara kabisa, kuna magari zaidi ya mia na hamsini yako katika foleni, ni vurugu tu ambapo mabasi yanapita porini. Nashukuru mimi nimepita porini naendelea na safari ya kwenda Dar.

Sijapata kama kuna mtu kapoteza maisha lakini cabin za magari yote zinashawishi kufikiria hivyo.

Nasikitika sijapata picha nzuri sana ya magari yaliyohusika katika ajari.
 

Attachments

  • uploadfromtaptalk1364553670475.jpg
    uploadfromtaptalk1364553670475.jpg
    26.5 KB · Views: 625
Very sad; Mpaka sasa ni ajali tatu kwa siku, hiyo, ile ya Tazara na ghorofa la city centre Dar
 
Damu inavyo zidi kumwagika za watanzania wasio kuwa na hatia ni dalili nzuri kwa maccm.
 
Wacheni ushabiki wa siasa kwanza tuwaombee walioiaga pasaka siku ya leo
 
Maadili yanapokiukwa tutarajie majanga zaidi na zaidi.Hakuna uwajibikaji kabisa,mfumo wa vyama vingi pia umechangia kuporomosha maadili.Vinapinga uwajibikaji,insha allah vitakaposhika dola sijui kama vita acha nchi iende kiholela kama ilivyo sasa.Sasa hivi kila mtu anafanya atakalo bila kujali kuwa anavunja sheria,madereva ndio usiseme,serikali ilipoweka fine kubwa kuwabana wajirekebishe,vyama pinzani vilikuja juu na fine zikashushwa.Kwa hali hii tutarajie nini? ndio hayo sasa!
 
Hakuna ajali mbona...au hiyo picha umeweka ni urembo tu
 
inaelekea saa 12 jion sasa folen ni kubwa na hata magari yaliyokuwa yanapita porini yameshafungamana maana hakuna wa kuyaongoza. tooo sad
 
Umenishtua sana ulipoandika ajali mbaya, kumbe hata haijulikani kama kuna mtu amefariki? Poleni sana kwa kadhia ya foleni ndefu!
 
Maadili yanapokiukwa tutarajie majanga zaidi na zaidi.Hakuna uwajibikaji kabisa,mfumo wa vyama vingi pia umechangia kuporomosha maadili.Vinapinga uwajibikaji,insha allah vitakaposhika dola sijui kama vita acha nchi iende kiholela kama ilivyo sasa.Sasa hivi kila mtu anafanya atakalo bila kujali kuwa anavunja sheria,madereva ndio usiseme,serikali ilipoweka fine kubwa kuwabana wajirekebishe,vyama pinzani vilikuja juu na fine zikashushwa.Kwa hali hii tutarajie nini? ndio hayo sasa!

Mkuu hapo nilipoweka rangi nyekundu sio sahihi sana (ungesema kwa mtazamo wako, ambao sio lazima uwe sahihi). Kuna maovu mengi ya kimaadili yameibuliwa na uwepo wa vyama vya upinzani na bila kuwapo yangebaki hivyo hivyo (Mifano ni mingi sina haja ya kukuwekea hapa, kama huijui huna haja ya kujiita mtanzania). Hapo kwenye Blue, umenishangaza sana tena sana!! Yaani vyama vya upinzani ndo vinapinga uwajibikaji? Are you really serious???!!! Tell us you are kidding!!
 
Mbona watanzania tumekuwa wabishi hata vitu ambavyo haviitaji kubishana? Kama hujaiona basi yawezekana ulilala wakati mnafika bwawani, it is not a big deal, kama wengine wanasema saa 12 pana foleni ya ajabu wewe unasema huoni, tukusaidiaje?
 
Back
Top Bottom