musa yasini
Member
- Dec 15, 2020
- 28
- 36
Inasikitisha sana kuona wanasiasa wetu wanaojiita wazalendo, kuwa na malimbikizo na misururu ya marupurupu na posho starehe, kusinzia, kupiga meza na kupongezana kuchaguliwa tena, tena wakiwa hawakatwi kodi na baada tu ya muhula wao kwisha ,bila kuchelewa, wameshachukua chao.
TENA WANACHOTEWA HASWAA, huku kundi lingine la watumishi wa umma ndio limebebeshwa mimba inayosumbua sana yenye mlundikano wa kero, kuonewa,unyanyasaji,kodi, mikopo kandamizi, mishahara duni, kuzuiliwa kuhama na kukosa matumaini juu ya mambo yajayo. Huku ndiko kuna ile sheria ya kwamba ukifa kabla hujatimiza miaka miaka mitano hupewi hata elfu moja japokuwa kiuhalisia unakuwa umefikisha si chini ya milioni 5! Je huu si wizi?
Bado ni katika kundi hilihili ambako wapiga meza wanatamani kuwapangia MAKOKOTOOO! ili kuleta shida zaidi juu yao kana kwamba wao ndio walikuwa wanawatunzia hizo pension zao. AIBUUU! Miaka 60 ndio upewe pension halafu uipeleke wapi au ugawie ndugu na wajukuu? NONSENSE! Je, haya mambo hawayaoniii au wamefumba macho wasisikie? Laiti ingetokea nikawa mfalme Naapa ningewanyoorosha! HUU SI USAWA WALA SI UZALENDO ,TUNADANGANYANA !!
TENA WANACHOTEWA HASWAA, huku kundi lingine la watumishi wa umma ndio limebebeshwa mimba inayosumbua sana yenye mlundikano wa kero, kuonewa,unyanyasaji,kodi, mikopo kandamizi, mishahara duni, kuzuiliwa kuhama na kukosa matumaini juu ya mambo yajayo. Huku ndiko kuna ile sheria ya kwamba ukifa kabla hujatimiza miaka miaka mitano hupewi hata elfu moja japokuwa kiuhalisia unakuwa umefikisha si chini ya milioni 5! Je huu si wizi?
Bado ni katika kundi hilihili ambako wapiga meza wanatamani kuwapangia MAKOKOTOOO! ili kuleta shida zaidi juu yao kana kwamba wao ndio walikuwa wanawatunzia hizo pension zao. AIBUUU! Miaka 60 ndio upewe pension halafu uipeleke wapi au ugawie ndugu na wajukuu? NONSENSE! Je, haya mambo hawayaoniii au wamefumba macho wasisikie? Laiti ingetokea nikawa mfalme Naapa ningewanyoorosha! HUU SI USAWA WALA SI UZALENDO ,TUNADANGANYANA !!