AIRTEL MONEY wamenitapeli Tsh 90,000/- yangu

AIRTEL MONEY wamenitapeli Tsh 90,000/- yangu

IKWETE

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2012
Posts
4,057
Reaction score
696
Wanabodi,
Hii ni kweli kabisa usiku wa Tarehe 21 na 22 nilituma pesa sh 10,000/- na 80,000/- kwa nyakati mbili tofauti ndani ya nusu saa nikiwa Bukoba kwenda kwenye namba 0719125715 kutoka kwenye namba 0688-01..18 nikapata kitambulisho rejea namba PN140221.2122.A.01459 na Kitambulisho rejea namba PN140222.0832.A00465.

Kesho yake yule niliyemtumia alipokwenda kuzitoa akashindwa, hakufanikiwa.
Aliponieleza nikafika ofisi za Airtel pale Bukoba ili wazireverse pesa zangu zirudi kwenye akaunti yangu kwakuwa nilishamtumia kupitia tigo pesa.

Mfanyakazi wa Airtel anayeitwa Simba wa pale Bukoba akaniambia nisubiri nusu saa, ikazaa saa moja, mbili na hatimaye hadi wanafunga ofisi pesa zangu hazikuwa zimerudi.

Nikapiga simu customer care, huko nikaambulia kuzodolewa na kujibiwa majibu yasiyo na staha na baadhi ya wasichana niliobahatika kuongea nao. Kwa hakika Customet care yao haikujishughulisha na mimi hata kidogo zaidi ya wale mabinti kunijibu hovyo na kunikatia simu.

Nikaenda kwenye mtandao wao, nikapata email yao ya kupeleka malalamiko, nikaandika malalamiko yangu. Aliyenijibu email yangu akakiri kuwa kuna tatizo kwenye airtel money kwenda offnet, na eti watazirudisha pesa zangu very soon. Nikasubiri kwa siku mbili hola!

Jana nikaenda ofisi zao pale Mwanza, nikapeleka tatizo hilohilo, mhudumu akaliverify akaona ni genuine aka escalate kwa wakubwa zake kwa ahadi kuwa very soon litakuwa solved. Hadi sasa hiyo very soon haijafika!

Leo nimefika hapa makao makuu yao, nimeleta tena hilo tatizo, nikajibiwa kuwa eti hizo pesa zilirudishwa kwangu usiku ule ule miliozituma na kwamba wao airtel hawahusiki kunirudishia hata shilingi kumi

Wiki nzima nimekuwa nikihangaikia pesa nilizozitafuta kwa jasho langu wahuni hawa wa airtel wameziiba tena bila hata haya wala soni!

Walivyo na dharau hata kumsikiliza mteja hawataki, majibu yao ya hovyo kumbe wanajua kuwa michezo yao ni wizi tu.

Ninaapa kwa jina la Mungu hizi pesa zilizobaki nikishazitoa sitakuja kutumia Airtel money milele yote

Asanteni Airtel kwa UTAPELI mlionifanyia.
 
Pole sana kiongozi wenye pesa wameshika mpini.
 
Nami walinizungusha kutoa pesa kila nnkiweka password wanakataa,
nkafata utaratibu wao wa kubadili Pin wap,
mwisho ikakubali katika kununua salio,
lakini kutoa pesa ikagoma,
kamwe situmii airtel money,
zaidi anzeni kukata na sio kuiba.
 
Nami walinizungusha kutoa pesa kila nnkiweka password wanakataa,
nkafata utaratibu wao wa kubadili Pin wap,
mwisho ikakubali katika kununua salio,
lakini kutoa pesa ikagoma,
kamwe situmii airtel money,
zaidi anzeni kukata na sio kuiba.
Mkuu inatia hasira sana
 
Just imagine wakifanya huo wizi kwa watu elfu kumi tu kwa siku, em' tupige hesabu sasa.
90,000 X 10,000 = 900,000,000, hii ni almost bilioni 1 kwa siku. Hatari sana.., ingekuwa mi naua mtu aisee..!!
 
Hawa jamaa hawafai hata kidogo kwenye fedha, inabidi sijui twende wapi maana mitandao yote ina tabia hii ya utapeli, sijui labda tigo sijawahi kuwatumia..Pole sana kiongozi tunaelewa uchungu ulio nao.lakini wajue ndio wanajiloga
 
Aisee usifute hizo msg,me imeshawahi nitokea hiyo kitu zaidi ya mara 2 na nilienda airtel makao makuu na nikarudishiwa pesa zangu fasta tu.Mara ya mwisho ilikuwa mwezi huu,nilituma pesa kutoka airtel kwenda tigo na nilienda kuzirejesha.Fuatilia mkuu,huku dar hiyo kitu ni simple tu.
 
Usifute izo sms kumbuka haki haiombwi nenda T C R A wakishindwa nenda mahakamani
 
ghalama ya kufuatilia tatzo ni zaid ya kumaliza tatizo. Sasa mala naul mwanza 2 bk na utaambiwa nenda dar ukpga esabu ume2mia lak 2 kwa kufuatlia 90. Ila kazana 2.
 
Kawaida yao aise.,mi walishafanya hvyo bt baada ya wiki kupita walinirudishia fedha yangu
 
Pole sna ila Airtel wanazingua sana, me nimeacha kabsa kutumia airtel money coz mambo kama hayo.

Sent from my BlackBerry 9790 using JamiiForums
 
Niliwahi kuibiwa 35000 kutoka kwa wakala mmoja yupo ipinda kyela nilikuwa namtumia mamangu kijijini.
sina hamu nao tena.
 
Na nyie hamkomi tu kutumia mitandao ya hovyo? Haipiti wiki hapa JF watu wanaanzisha thread za Wizi wa Airtel lakini hamjifunzi!! Ona mtu Ulikuwa BKB, Ukaenda Mwanza, Umefika hadi Dar bado watu hawana hata punje ya huruma. Na bado kuna wapuuzi wataendelea kuitumia Airtel money! Watanzania sijui tumerogwa na nani haki ya mungu!
 
Back
Top Bottom