Airtel babalao

Airtel babalao

Sodium 23

JF-Expert Member
Joined
Sep 17, 2013
Posts
484
Reaction score
492
Asalaam aleykum wanajukwaa!
Sina mengi zaidi ya kusema airtel ni baba lao kwa sababu zifuatazo:
1. Huduma za kifedha ni nafuu. Kutuma pesa kwa airtel money ni bure kabisa, pia kutoa ni nafuu kuliko mitandao mingine.
Pia maduka ya airtel money yamejaa kila kona hadi nashindwa kuchagua nitoe pesa wapi.

2. Huduma za intaneti ni za uhakika. Ukiambiwa 1GB ni 1GB kweli. Unatumia hadi unawapigia customer care kwa nini kifurushi hakiishi.

3. Vifurushi vya airtel ni babu kubwa. Mi hua najiunga kifurushi cha mwezi 5000 mitandao yote napata dakika 250. Airtel airtel napata dakika 320 mwezi mzima kwa shilingi 4,000/=.
Vifurushi vya siku hadi shillingi 200 unapata dakika au MB za kuperuzi data.

4. Serikali inamiliki hisa asilimia 49 kwa hiyo ni kampuni ya kizalendo.

5. Airtel inatoa gawio kwa serikali kwa hiyo ukitumia huduma ya airtel unakua umeunga juhudi za JPM.

6. Airtel haidukuliwi ovyo kama mitandao mingine.
Ni hayo tu kwa leo, twende Airtel
 
Nilinunua line ya airtel kwa kumsikiliza mtu kama ww matokeo yake bando nililonunua sijaweza kulitumia! Speed ya kobe na hapa ni dar!

Sent using Redmi Y2
 

Uhamiaji wamezindua mfumo wa malipo ya passport kupitia Airtel Money.
Mambo ni moto
 
Spidi ya mtandao iko chini sana hadi najuta kununua kifurushi Airtel ...au ndio kuibiwa unit huku.
 
Hongera unaweza sana kazi yako ya kupigia promo uko vizur
 
Airtel ilikuwa zamani buana toka walivonyimwa kutumia minara ya ttcl imekuwa majanga
 
Back
Top Bottom