Aina za ndoa 2023

Aina za ndoa 2023

Anak
Ni ndoa ambazo zimejaa usanii na maigizo

Kislay queen kitakuugizia kinakupenda kinyama kitakupost sana kwenye mitandao mkiwa maeneo mazuri au mkiwa mnakula bata

Ukifilisika vijembe vinaanza hawachelewi kufuta post zake zote enzi hizo mkiwa mnakula bata mpunga ukiwepo
Anakutosa vibaya mno
 
Nilishuhudia ndoa ya mimba ilivunjika mtoto akiwa na miezi 9
 
Of all ndoa namba #10 ndio ndoa inayoongoza kwa kufungwa na vijana na maslay queen wa mjini.

Haidumugi sababu msingi wa ndoa ni huduma. Mwanaume anakuwa ameielewa shape na muonekano wa demu ila demu anakuwa amependa lifestyle ya mwanaume huyo. Pesa ya kula bata na magari ya kufanyia starehe za town.

Ikitokea tu mwanaume hela zimekata ndio mgogoro unapoanzia tena vijembe na kejeli za mwanamke hutajua zilipotokea. 😀😀😀 Kumbe alikuwa anakudanga tu kabla hujatumbuliwa.
Hiyo namba 10 tena binti ndiye anainitiate mahusiano kwa kujilengesha, ukinasa umekwisha wanakuwaga na hesabu kali.
 
1. NDOA YA MKEKA
Inatokana na kufumaniwa na Binti wa watu. Ndoa hii huwa Haina mahari. Hii huvunjika mwaka mmoja tu baada ya wanandoa kugundua hawakuwa wakipendana!

2. NDOA YA MIHEMKO (NYEGE)
Hufungwa na vijana wenye umri wa miaka kati mume18 mke 16. Huvunjika baada ya miaka 3 au 4 ya ndoa.

4. NDOA YA MAONYESHO
Wenye ndoa Hii hupenda kujionyesha barabarani. Ila ndani hazina utii. Hupigana kila wanaporudi kutoka kwenye mizunguko. Cha kushangaza huwa hazivunjiki lakini ndiyo ndoa zinazoongoza kwa kuchepuka!

5. NDOA YA UHAMISHO.
Hufungwa na watumishi wa vijijini na mjini. Ili wa kijijini ahamie mjini. Mahari hutoa anayetaka kuhamia mjini. Hata kama mahari atatoa mume lakini hii ndiyo ndoa yenye ukakasi zaidi.Huvunjika mara tu wanapoanza kuishi wote mjini. Salama ya hii ndoa ni kuhama kutoka mjini kwenda kijijini.

6. NDOA YA MIMBA.
Hufungwa kwa sababu wanaoowana hawataki kuonekana makwao kuwa wamezaa nje. Au muolewaji alikuwa hampendi muoaji kwa dhati.Muoaji hutumia mimba kama mtego wa kuingia ndoani. Hii huvunjika mtoto akizaliwa na kufikisha mwaka 1.

7. NDOA YA MALI (UTAJIRI)
Muolewaji miaka 18 au 28 Muoaji 65 au 70.Ndoa hii pia huitwa ndoa ya babu na mjuukuu. Ndoa ya aina hii hudumu, kwasababu mwenye kauli ni mwenye mali. Asilimia kubwa ya waume wa ndoa hizi hulea watoto wasio wao.

8. NDOA YA KWA SABABU.
Hufungwa ili mradi muoaji au muolewaji aonekane tu kwa jamii kuwa naye kaoa au kaolewa. Huwa hazina utii wala upendo dhati. Ndoa ya aina hii ikifikisha miaka 4 huwa hazivunjiki wahusika huishi kwa mazoea.

9. NDOA YA UPENDO.
Ndoa hizi ziliishia mwaka 1978 kabla ya vita vya Kagera. Muoaji na muolewaji hawakuangalia vitu ila utu tu ambao uliwaunganisha na kutengeneza upendo wa kudumu. Hii ilidumu miaka yote.

10. NDOA KUCHUMA
Ndoa hii ufungwa ili mradi muoaji au muolewaji akapate kitu au vitu fulani kutoka kwa upande mmoja wapo. Hii hudumu miaka kadhaa kutegemea na malengo ya mhusika. Wengine husubiri mpaka mhusika afe,lkn hujikuta wanakufa wao kwanza

11. NDOA ZA HUDUMA
Hii hufungwa baada ya binti au kijana kuona anaweza jipatia matunzo kiulaini kama kula bure, kulala kuvishwa, kupewa gari na vingine kama hivyo kutoka kwa mwenza, hudumu sana mpaka pale mtunzaji atakapo shindwa au kuchoka kumhudumia mhusika hapo ndo mhudumiwaji atahamia kwingine. Hizi ndo nyingi kwa sasa na ndo zinaongoza kutrend instagram.
Ndoa No. 1 inafungwa na waislamu pekee, zilizobaki zote wote tunahusika kwa namna moja au nyingine
 
Hamna ndoa Kama hiyo katika uislamu labda uipeleke kwenye mila
Ushawahi kuta Padre au mchungaji anafungisha ndoa ya watu waliofumaniwa? Lakini mashehe walishawahi fanya hayo..!! Labda kama umeamua kubisha
 
ukiwa mwanaume na ndoa yako ni aina ya namba 5, ikiwa mna watoto si ajabu wengine si wako. Ni ndoa zinazoongoza wanandoa kuchepuka. Na wanandoa wengi katika ndoa hii huwa hawalali chumba kimoja. Kila mmoja anajua anavyoingia na kutoka. sterling wa nyumba ni housemaid
Hahahaaa housegirl ndo ana control mchezo
 
kuna NDOA NDOIGE
hii ndowa hipo kwa ndugu zetu waislamu sana sana.imebeba yote uliyoeleza
 
Ushawahi kuta Padre au mchungaji anafungisha ndoa ya watu waliofumaniwa? Lakini mashehe walishawahi fanya hayo..!! Labda kama umeamua kubisha
Mkuu Shekh akifanya hivyo Haina maana kuwa Jambo Hilo limeamrishwa,,,

Hivyo Shekh akifanya hivyo wakati uislam haujaamrisha hivyo hiyo Ni haramu yake
 
Mkuu Shekh akifanya hivyo Haina maana kuwa Jambo Hilo limeamrishwa,,,

Hivyo Shekh akifanya hivyo wakati uislam haujaamrisha hivyo hiyo Ni haramu yake
At least you got my point.
Lakini nyie kukana ndiyo zenu. NASISITIZA, NDOA YA MKEKA INAFUNGWA NA WAISLAMU PEKEE
 
10. NDOA KUCHUMA
Ndoa hii ufungwa ili mradi muoaji au muolewaji akapate kitu au vitu fulani kutoka kwa upande mmoja wapo. Hii hudumu miaka kadhaa kutegemea na malengo ya mhusika. Wengine husubiri mpaka mhusika afe,lkn hujikuta wanakufa wao kwanza
Hahahahaha mkeka unakuchanikia
 
1. NDOA YA MKEKA
Inatokana na kufumaniwa na Binti wa watu. Ndoa hii huwa Haina mahari. Hii huvunjika mwaka mmoja tu baada ya wanandoa kugundua hawakuwa wakipendana!

2. NDOA YA MIHEMKO (NYEGE)
Hufungwa na vijana wenye umri wa miaka kati mume18 mke 16. Huvunjika baada ya miaka 3 au 4 ya ndoa.

4. NDOA YA MAONYESHO
Wenye ndoa Hii hupenda kujionyesha barabarani. Ila ndani hazina utii. Hupigana kila wanaporudi kutoka kwenye mizunguko. Cha kushangaza huwa hazivunjiki lakini ndiyo ndoa zinazoongoza kwa kuchepuka!

5. NDOA YA UHAMISHO.
Hufungwa na watumishi wa vijijini na mjini. Ili wa kijijini ahamie mjini. Mahari hutoa anayetaka kuhamia mjini. Hata kama mahari atatoa mume lakini hii ndiyo ndoa yenye ukakasi zaidi.Huvunjika mara tu wanapoanza kuishi wote mjini. Salama ya hii ndoa ni kuhama kutoka mjini kwenda kijijini.

6. NDOA YA MIMBA.
Hufungwa kwa sababu wanaoowana hawataki kuonekana makwao kuwa wamezaa nje. Au muolewaji alikuwa hampendi muoaji kwa dhati.Muoaji hutumia mimba kama mtego wa kuingia ndoani. Hii huvunjika mtoto akizaliwa na kufikisha mwaka 1.

7. NDOA YA MALI (UTAJIRI)
Muolewaji miaka 18 au 28 Muoaji 65 au 70.Ndoa hii pia huitwa ndoa ya babu na mjuukuu. Ndoa ya aina hii hudumu, kwasababu mwenye kauli ni mwenye mali. Asilimia kubwa ya waume wa ndoa hizi hulea watoto wasio wao.

8. NDOA YA KWA SABABU.
Hufungwa ili mradi muoaji au muolewaji aonekane tu kwa jamii kuwa naye kaoa au kaolewa. Huwa hazina utii wala upendo dhati. Ndoa ya aina hii ikifikisha miaka 4 huwa hazivunjiki wahusika huishi kwa mazoea.

9. NDOA YA UPENDO.
Ndoa hizi ziliishia mwaka 1978 kabla ya vita vya Kagera. Muoaji na muolewaji hawakuangalia vitu ila utu tu ambao uliwaunganisha na kutengeneza upendo wa kudumu. Hii ilidumu miaka yote.

10. NDOA KUCHUMA
Ndoa hii ufungwa ili mradi muoaji au muolewaji akapate kitu au vitu fulani kutoka kwa upande mmoja wapo. Hii hudumu miaka kadhaa kutegemea na malengo ya mhusika. Wengine husubiri mpaka mhusika afe,lkn hujikuta wanakufa wao kwanza

11. NDOA ZA HUDUMA
Hii hufungwa baada ya binti au kijana kuona anaweza jipatia matunzo kiulaini kama kula bure, kulala kuvishwa, kupewa gari na vingine kama hivyo kutoka kwa mwenza, hudumu sana mpaka pale mtunzaji atakapo shindwa au kuchoka kumhudumia mhusika hapo ndo mhudumiwaji atahamia kwingine. Hizi ndo nyingi kwa sasa na ndo zinaongoza kutrend instagram.

12. NDOA ZA KUSOGEZANA
Hizi vijana ambao hawajajipanga huamua kuanza kuishi pamoja huku wakikusanya mahari na hela ya harusi, hizi changamoto yake ni jambo la kufunga ndoa ambalo lingeweza kufanyika ndani ya mwaka basi laweza fanyika baada ya miaka kumi. Hizi pia hudumu sana na binti huzaa chap chap ili kujimilikisha nafasi asije achwa
Mbona ndoa za "Ramadhani" haujazitaja?

Zile nyingi nyingi zinazofungwa kwa mihemko ya mwezi mtukufu!

Yote kwa yote, umeonesha udhaifu katika utafiti wako kwa kuweka hitimisho kwa kila aina ya ndoa, ambapo siyo sahihi na siyo kweli!

Chanzo chochote cha ndoa chaweza kuhitimishwa kwa upendo.

Na pia chanzo chochote cha ndoa chaweza kuhitimishwa kwa kusambaratika.

Natolea mfano kwangu mwenyewe;
Mke niliyenaye nimeishi naye zaidi ya miaka 30 sasa bila ya tatizo lolote, lakini nilivyompata sasa!

Nilipomuonesha nia akawa hanitaki, tena kwa kashifa zake za kishenzi, eti "tena nimkome kama nilivyokoma kunyonya ziwa la mamangu mzazi!"

Kunikataa kwa mdomo mdomo ndipo alipo nitibua na kukazia nia yangu na kumuonesha kwamba mi zaidi.

Nikaweka mamluki kwenda kumjaza vitisho kwamba mimi ni mchawi hamnepo na kwa matusi aliyonitukana ninaweza kumaliza ukoo wao mzima kama hataangalia😆😆😆!

Vitisho vikamwingia binti, akatuma wajumbe kuja kumuombea msamaha nikakataa.

Nikaongeza masharti kwamba akiniona awe ananikwepa tusionane na ikitokea tumekutana basi asinisalimie vinginevyo kifo kinamhusu!

Nikaona kama anapuuza, nikaweka mazingira ya kesi.

Akashitukia namshitaki kwa mwenyekiti, mashahidi ni wale alokuwa anawaeleza zile kashifa kunihusu!

Mwenyekiti kutaka kutusuluhisha nikakataa nikaomba kwenda mbele.

Mamluki wangu nikawapanga kwenda kumzidishia vitisho, "kachezea pabaya na safari hii anafungwa" sitaki ujinga mie.

Akajiongeza akaomba tukutane naye.

Tulipo kutana naye, alijiandaa kisaikolojia kunipatia "rushwa" ili yaishe!

Nikakubali kupokea hiyo "rushwa", kweli yakaisha, mahari ikatolewa, ndoa ikafungwa na mpaka sasa ndiye mke.

Ndiyo kusema chanzo chaweza kuwa ni cha vurugu, ama sura yoyote lakini baadaye upendo na maelewano yakatengenezwa juu kwa juu na watu wakaishi daima dumu!
 
13.Ndoa Ndoige ndoa za mke mmoja, kwa wenzetu wakristu, hapo ukijichanganya umekwisha, ukipigwa kama umepigwa na ukipiga kama umepigwa tu, mwanamke ana relax mana hamna competition wala kipengele cha kuvunja ndoa hakipo,kwenye ndoa hizi mara nyingi wanawake ni mabonge na matumbo makubwa sababu ya ku relax na wanaume hukonda sana, wanaume huishia kujinyonga au kuwa na michepuko ya kutosha.
 
Back
Top Bottom