Aikimbia CHADEMA baada ya kutapeliwa: Kinana ahutubia maelfu katika kata ya Nyololo Mufindi

MwanaDiwani

JF-Expert Member
Mar 22, 2013
5,536
2,264
Akiwahutubia Maelfu ya wakazi wa jimbo la Iringa mjini katika uwanja wa Mwembetogwa , Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alianza hotuba yake kwa kusema, " Nawaambieni wala hamta nisikia nikishughulika na kumzungumzia mbunge wenu hapa sina Time, mimi nashughulika na mambo ya wananchi kwani mbunge wenu ni kazi yake kutukana kila mmoja na kuhamasisha maandamano yasiyo kwisha "

Akihutubia huku akishangiliwa na maelfu ya wananchi uwanjani hapo, Kinana alisema kuwa amefika jimbo la Iringa mjini kuwaeleza mambo ya kimaendeleo sio kumsema mchungaji Msigwa.

Aliendelea kusema, ''Napenda niwaambie kuwa, kazi zilizofanywa na CCM na serikali yake ni kubwa na kuwa hata miradi ya barabara inayoendelea kujengwa ni jitihada za serikali ya CCM chini ya Rais Jakaya Kikwete hivyo mbunge wenu hana sababu ya kujisifu kwa kazi hizo''.

Katibu mkuu huyo alieleza kusikitishwa kwake na ushuru mbali mbali kwa wananchi wanaojitafutia maisha yao huku viongozi wakijiweka mbinguni na wananchi wao. amewaahidi kukifikisha kilio chao kwenye Kamati Kuu ya CCM na serikalini.

Alisema kuwa ndani ya serikali hii mwananchi anatafuta haki yake hapati hadi atoe rushwa huku viongozi waliopo ndani ya CCM badala ya kushughulika na mambo ya wananchi wanashughulika na mambo yao wenyewe huku wakiendekeza ugomvi usio na mwisho .

" Tunapoteza majimbo na kata kwa ajili ya uroho wa uongozi kwa baadhi yetu na kushindwa kushuka kuwasikiliza wananchi wa chini hali inayozalisha malalamiko ya wananchi na kupelekea kuhamia vyama vya upinzania"

"Ni lazima kujiimarisha kuanzia ngazi ya chini kabisa ili kupata ushindi ikiwa ni pamoja na kuondokana na makundi ambayo yanakigawa chama,"anasema.

Hivyo alisema kuwa iwapo jimbo la Iringa mjini litapata mgombea mgombea mzuri hakuna upinzani katika jimbo hilo ila kama ugomvi wa madaraka utaendelea itakuwa ni kazi kupata mgombea wa CCM .

Alisema kuwa tabia ya baadhi ya wagombea kulazimisha kuendelea kugombea huku wakijua wamechuja ni moja kati ya sababu ya CCM kuendelea kuchokwa na wananchi na hivyo kuamua kuchagua wapinzani.

Kinana alisema kuwa tatizo la CCM kupoteza jimbo hilo ni uroho wa madaraka kwa wale ambao hawakubaliki kwa wananchi kosa ambalo kamwe CCM haitarudia kulifanya.

Kinana alihoji na kusema kuwa, kuna mitaa 150 katika jimbo la Iringa mjini ambapo ni mtaa mmoja pekee ndiyo CHADEMA waliuchukua, wakati huo huo kuna kata zaidi ya 17 ambapo CHADEMA walichukua kata moja kwenye uchaguzi. Sasa ni namna gani CCM ishindwe ubunge jimbo hilo hilo kama si tamaa za uongozi kwa baadhi ya wagombea.

Hivyo aliwataka viongozi hao wa CCM kujaribu kusoma alama za nyakati na iwapo watajua kuingia, basi wajifunze na kutoka kwani kuna wakati wa kuchokwa. Ni lazima wakubali kuondoka badala ya kung'ang'ania kugombea .

Pia katibu huyo aliwataka wana CCM kujifunza kujiuliza kwa wananchi wengine kama wanakubalika ama hawakubaliki badala ya kusimamia maamuzi yao ya kuingia kugombea bila kupendwa na wananchi na kuwa kosa lililofanyika mwaka 2010 kamwe halitajirudia tena.

" Ni mambo ya ovyo yaliyokuwa yakifanyika ndani ya CCM ndio ambayo yamekigharimu chama na kuwa jimbo la Iringa mjini hakuna mpinzani ila wapo wanaotafuta kusikilizwa katika mambo yao na iwapo CCM itatenda mema kwa kusikiliza wananchi jimbo la Iringa mjini hakuna upinzani ila upuuzi ,rushwa ndani ya CCM na serikali yake ndio imekigharimu chama hicho "alisema
=================================================================================
Umati wa wananchi na wanaccm waliofika kumsikiliza Kinana
Aliyewahi kuwa mgombea ubunge Jimbo la Kalenga wa Chadema kura za maoni, Sanga Abubakar akitangaza kuihama Chadema na kujiunga na CCM wakati wa mkutano huo
Umati wa wananchi mjini Iringa


Sehemu ya umati wa watu katika mkutano huo ulihutubiwa na Katibu Mkuu wa CCM, Kinana katika mji wa Nyololo, Mufindi.



Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akionesha kadi 27 za wananchama wa Chadema waliokihama chama hicho na kujiunga na CCM katika mkutano wa hadhara uliofanyika Mjini Nyololo, wakati wa ziara ya kuimarisha uhai wa chama na kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2010. Kulia aliyevaa shati jeupe ni aliyekuwa Katibu wa Kata ya Igowole, Josephat Soda ambapo wengine ni miongoni mwa walio kuwa wafuasi wa Chadema.
Aliyekuwa Katibu wa CHADEMA Kata ya Igowole, Josephat Soda akikabidhi bendera ya chama hicho kwa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana baada ya yeye na wenzie 26 kutangaza kuihama Chadema na kujiunga na CCM wakati wa mkutano huo.
Katibu Mkuu wa CCM, Kinana akimkabidhi kadi ya CCM, Josephat Soda baada ya kutanga kujiunga na CCM katika mkutano huo.
Josephat Soda akielezea jinsi alivyoamua kuondoka Chadema na kujiunga na CCM, ambapo alisema amechoka na chama kilichosheheni uongo na ulaghai, ambapo alidai viongozi wa Chadema walitoa maagizo kuwa akope fedha za kujengea Mnara wa mwandishi wa habari Marehemu David Mwangosi, aliyeuawa wakati wa vurugu za CHADEMA na Polisi katika Mji wa Nyololo, ambapo walimuahidi kumtumia fedha zilizotumika kujenga mnara huo ahadi ambayo hadi sasa hawajaitimiza na anadaiwa na muuza simenti na muuza saruji alikokopa. Kutokana na maelezo yako, CCM imeamua kulipa madeni yote aliyokuwa akidaiwa ili kutunza heshima.
Wanachama wa CCM wakiwemo wale wapya kutoka Chadema, wakiapa kiapo cha utii cha CCM baada ya kukabidhiwa kadi wakati wa mkutano huo
Mfuasi wa CCM, Keneth Mwangosi, akiwa mbele ya gari lake alilolifanyia ukarabati wa kuvutia na mbele yake kuandika jina la Kinana
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (kulia na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye wakichuma majani ya chai katika shamba la Unilver, wakati wa ziara ya kuimarisha uhai wa chama na kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2010, na pia kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi katika Jimbo la Mufindi Kusini, mkoani Iringa.
Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Iringa, Jesca Msambatavangu (katikati) wakisaidia kuchuma majani ya chai katika shamba hilo la Unilve akiwa na viongozi wengine wa chama hicho
Kinana akisaidia kumwagilia maji miche ya miti alipokwenda kukagua bustani ya Vijana mjini, Kigamboni mjini Mafinga
 
Siasa siyo maneno bali ni vitendo vinavyopimwa katika chaguzi za kitaifa na ndogo kwenye sanduku la kura.

CCM haina muda wa kupambana na mashujaa wa maneno na propaganda katika nchi yao ya kufikirika yenye Rais wa kufikirika.

Kazi ya CCM na serikali yake ni kuongoza kwa vitendo na siyo kuongoza kwa maneno.

Kazi ya CCM ni kuibua na kuziweka (set) agenda za kitaifa katika taifa kwa maendeleo ya taifa huku vyama vya upinzani vikifuata.

CCM kwa sasa imezifunga hoja za upatikanaji wa Katiba Inayopendekezwa, kwa sasa iko kwenye hoja ya upigaji wa kura ya maoni. Kwa sasa CCM imewaachia wengine kazi ya kutafuta barabarani hoja za Katiba Inayopendekezwa.

CCM ni Itikadi, Falsafa, Sera na Ilani ya Uchaguzi inayotekelezeka.

Karibu sana katika ulimwengu wa CCM unakubaliwa na wananchi wengi nchini kama matokeo ya chaguzi mbali mbali yanavyobainisha.
 
Eeeh!!!! Mungu wangu msikivu nakuomba uitazame vizuri nchi yako hii ya Tanzania, naomba utuokoe kutoka kwenye mikino ya chama cha kifisadi,
nakuomba Mungu wape busara na hekima watu wote walioajiliwa na mafisadi ya nchi ili kuyapingia propangada na kuyaficha makosa ya mafisadi.,, bele ya wanainchi waliokosea elimu hata ya darasa la saba.

mungu wangu nakuomba fichua maovu yote yaliyofanywa na ccm ili kila wanainchi ayaelewe.
ni katika jina la yesu anatheti aliye hai, wote tuseme amen
 
Siasa siyo maneno bali ni vitendo vinavyopimwa katika chaguzi za kitaifa na ndogo kwenye sanduku la kura.

CCM haina muda wa kupambana na mashujaa wa maneno na propaganda katika nchi yao ya kufikirika yenye Rais wa kufikirika.

Kazi ya CCM na serikali yake ni kuongoza kwa vitendo na siyo kuongoza kwa maneno.

Kazi ya CCM ni kuibua na kuziweka (set) agenda za kitaifa katika taifa kwa maendeleo ya taifa huku vyama vya upinzani vikifuata.

CCM kwa sasa imezifunga hoja za upatikanaji wa Katiba Inayopendekezwa, kwa sasa iko kwenye hoja ya upigaji wa kura ya maoni. Kwa sasa CCM imewaachia wengine kazi ya kutafuta barabarani hoja za Katiba Inayopendekezwa.

CCM ni Itikadi, Falsafa, Sera na Ilani ya Uchaguzi inayotekelezeka.

Karibu sana katika ulimwengu wa CCM unakubaliwa na wananchi wengi nchini kama matokeo ya chaguzi mbali mbali yanavyobainisha.
Kweli ndiyo maana wanasema CCM inajitekenya na kucheka yenyewe...umetoa mada mwenyewe kuchangia wewe ndiyo wa kwanza na ukaanza kujifurahisha mwenyewe na kucheka baada ya kuchangia kwenye mada yako. Kweli mnazidi kuvunja rekodi kama ile ya bunge la katiba la kuchangia,kushangilia kuwa michango yenu mizuri wenyewe,kuanza kujipigia kura wenyewe,kuhesabu kura wenyewe,kujipongeza kwa ushindi wa kushinda baada ya kufanya uchaguzi wenyewe pia mkajipongeza duuuuuuuuuu haya ni maajabu. Ni kama kiongozi mkubwa wa serikali kuwa masharti yake ajue kusoma na kuandika tu maana ndo sifa ya kuwa mbunge wakati Dreva wake masharti awe amemaliza kidato cha Nne.
 
Siasa siyo maneno bali ni vitendo vinavyopimwa katika chaguzi za kitaifa na ndogo kwenye sanduku la kura.

CCM haina muda wa kupambana na mashujaa wa maneno na propaganda katika nchi yao ya kufikirika yenye Rais wa kufikirika.

Kazi ya CCM na serikali yake ni kuongoza kwa vitendo na siyo kuongoza kwa maneno.

Kazi ya CCM ni kuibua na kuziweka (set) agenda za kitaifa katika taifa kwa maendeleo ya taifa huku vyama vya upinzani vikifuata.

CCM kwa sasa imezifunga hoja za upatikanaji wa Katiba Inayopendekezwa, kwa sasa iko kwenye hoja ya upigaji wa kura ya maoni. Kwa sasa CCM imewaachia wengine kazi ya kutafuta barabarani hoja za Katiba Inayopendekezwa.

CCM ni Itikadi, Falsafa, Sera na Ilani ya Uchaguzi inayotekelezeka.

Karibu sana katika ulimwengu wa CCM unakubaliwa na wananchi wengi nchini kama matokeo ya chaguzi mbali mbali yanavyobainisha.

ha ha ha wame bakia watu wesio na akili timamu tu wanao ishabikia ccm.
 
Kweli ndiyo maana wanasema CCM inajitekenya na kucheka yenyewe...umetoa mada mwenyewe kuchangia wewe ndiyo wa kwanza na ukaanza kujifurahisha mwenyewe na kucheka baada ya kuchangia kwenye mada yako. Kweli mnazidi kuvunja rekodi kama ile ya bunge la katiba la kuchangia,kushangilia kuwa michango yenu mizuri wenyewe,kuanza kujipigia kura wenyewe,kuhesabu kura wenyewe,kujipongeza kwa ushindi wa kushinda baada ya kufanya uchaguzi wenyewe pia mkajipongeza duuuuuuuuuu haya ni maajabu. Ni kama kiongozi mkubwa wa serikali kuwa masharti yake ajue kusoma na kuandika tu maana ndo sifa ya kuwa mbunge wakati Dreva wake masharti awe amemaliza kidato cha Nne.
Ndugu,
Nadhani unachokiongea hufahamu hata mantiki yake!

Dreva anateuliwa miongoni mwa walioomba kazi.

Mbunge anachaguliwa kupitia kura kwenye sanduku la kura lenye waomba wabunge wa kujitegemea au kupitia vyama vya siasa.

Taifa liko kwenye mfumo wa vyama vingi na wagombea binafsi.

Kama hoja ni elimu, basi CCM wakituwekea mgombea wao anayefahamu kusoma na kuandika pekee, hatutamchagua kama hoja ni elimu, badala yake tutamchagua mgombea kupitia NLD ambaye ana elimu ya degree ya chuo kikuu au tutamchagua mgombea binafsi mwenye elimu ya degree mbili za chuo kikuu.

Hiki siyo kipindi cha chama kimoja, kwa maana kuwa CCM ikiweka mgombea yoyote bila kujali elimu yake, basi anashinda uchaguzi!. Wananchi ndiyo waamuzi kulingana na mahitaji yao katika sanduku la kura.

Ni upungufu kifikra kushikia bango hoja ambayo haina mantiki katika mfumo wa vyama vingi ndani ya demokrasia.
 
ha ha ha wame bakia watu wesio na akili timamu tu wanao ishabikia ccm.
Ndugu,
Ndiyo watu hao hao wasio na akili timamu wanaoipatia CCM nchi yao kuiongoza.

Ndiyo watu hao hao wasio na akili timamu mnawaomba kura zao ili wawape nchi yao kuitawala.

Hekima na busara zao ambazo mnaziona ni upunguvu wa akili ndizo zimewafanya nyie kutokupatiwa nchi kuiongoza tokea mwaka 1995.

CCM ni chama cha wananchi wote na kwa maana hiyo, kitaendelea kuwakaribisha na kuwashukuru kwa kukipatia nchi kiiongoze hata wale mnaowadhani hawana akili timamu.
 
CCM, pamoja na kwamba inafanya uozo mkubwa sana katika nchi yetu, lakn imeendelea kutumia hela kuhoga wanainchi, na kuwaajili watu kama mwanadiwani kuipiga porojo za uongo kwa wanainchi

ukitembelea sehemu za vijijini kempeni ya ccm inafanywa kwa mngombea wa ccm kutembea na mifuko ya chumvi, viberiti pamoja na kanga.

ccm kiama chake 2015
 
Siasa siyo maneno bali ni vitendo vinavyopimwa katika chaguzi za kitaifa na ndogo kwenye sanduku la kura.

CCM haina muda wa kupambana na mashujaa wa maneno na propaganda katika nchi yao ya kufikirika yenye Rais wa kufikirika.

Kazi ya CCM na serikali yake ni kuongoza kwa vitendo na siyo kuongoza kwa maneno.

Kazi ya CCM ni kuibua na kuziweka (set) agenda za kitaifa katika taifa kwa maendeleo ya taifa huku vyama vya upinzani vikifuata.

CCM kwa sasa imezifunga hoja za upatikanaji wa Katiba Inayopendekezwa, kwa sasa iko kwenye hoja ya upigaji wa kura ya maoni. Kwa sasa CCM imewaachia wengine kazi ya kutafuta barabarani hoja za Katiba Inayopendekezwa.

CCM ni Itikadi, Falsafa, Sera na Ilani ya Uchaguzi inayotekelezeka.

Karibu sana katika ulimwengu wa CCM unakubaliwa na wananchi wengi nchini kama matokeo ya chaguzi mbali mbali yanavyobainisha.

Mbona Hamjapiga picha mkinywa ulanzi na mtakoma mpaka uchaguzi wa serikali za mitaa upite!
 
Ndugu,
Ndiyo watu hao hao wasio na akili timamu wanaoipatia CCM nchi yao kuiongoza.

Ndiyo watu hao hao wasio na akili timamu mnawaomba kura zao ili wawape nchi yao kuitawala.

Hekima na busara zao ambazo mnaziona ni upunguvu wa akili ndizo zimewafanya nyie kutokupatiwa nchi kuiongoza tokea mwaka 1995.

CCM ni chama cha wananchi wote na kwa maana hiyo, kitaendelea kuwakaribisha na kuwashukuru kwa kukipatia nchi kiiongoze hata wale mnaowadhani hawana akili timamu.

mwehu wewe unadhani kila siku ijumaa ccm mwisho wake 2015.
 
Ndugu,
Ndiyo watu hao hao wasio na akili timamu wanaoipatia CCM nchi yao kuiongoza.

Ndiyo watu hao hao wasio na akili timamu mnawaomba kura zao ili wawape nchi yao kuitawala.

Hekima na busara zao ambazo mnaziona ni upunguvu wa akili ndizo zimewafanya nyie kutokupatiwa nchi kuiongoza tokea mwaka 1995.

CCM ni chama cha wananchi wote na kwa maana hiyo, kitaendelea kuwakaribisha na kuwashukuru kwa kukipatia nchi kiiongoze hata wale mnaowadhani hawana akili timamu.
Mnasali usiku na mchana watu wabaki bumbumbu ili muendelee kuwatawala. Kwa bajeti ya trilioni 19 na pointi kwa kodi na vyanzo vingine kwa wawtz mil.45 kila mtu hadi Juni 2015 atachangia 800,000 kwa kijiji wastani wa watu 1500 ni mil 1200 zimelengwa kupatikana kwa kila kijiji. Sasa angalia ni mil ngapi zimepangwa ngazi ya kila kijiji na hiyo kata ya nyololo ikiwemo? Upinzani utawa elemisha maana shule za kata zimesaidia watu kuelimishwa kiurahisi. Laghai na asie laghai atafahamika.
 
Kama kawa,ukiona tshirt na kofia nyingi,tambua hadhira yetu ni ile ile ya kubebwa.
Watu hawaji kwenye mkutano hadi waimbiwe na kuchezewa dance na wasanii; hawaji ng'o hadi kwa ving'ora na mikwara toka kwa wajumbe nyumba 10; hawaji ng'o hadi wavikwe tshirt na kofia kisha wasombwe na malori.

Acha hela ya escrow acc.iendelee kuwanunulilia watu tshirt za rangi ya chama.

Huku mzee wa vipusa na Nape wakizoa posho za kimagumashi. Nape usipojenga mwaka huu, Lowassa atakung'oa tu awamu ijayo SI unaelewa mwenyekiti ajaye sio mtu wa taarabu na vijiwe.Yeye ni mtu wa maamuzi magumu. KAA CHONJO, SAA MBAYA!

KAAZI KWELI KWELI.
 
Mzee kinana kathubutu kaweza sasa anasonga mbele kwa kasi ya ajabu sana mungu amuongoze katika utendaji wake.
 
Ndugu,
Ndiyo watu hao hao wasio na akili timamu wanaoipatia CCM nchi yao kuiongoza.

Ndiyo watu hao hao wasio na akili timamu mnawaomba kura zao ili wawape nchi yao kuitawala.

Hekima na busara zao ambazo mnaziona ni upunguvu wa akili ndizo zimewafanya nyie kutokupatiwa nchi kuiongoza tokea mwaka 1995.

CCM ni chama cha wananchi wote na kwa maana hiyo, kitaendelea kuwakaribisha na kuwashukuru kwa kukipatia nchi kiiongoze hata wale mnaowadhani hawana akili timamu.
Mnasali usiku na mchana watu wabaki bumbumbu ili muendelee kuwatawala. Kwa bajeti ya trilioni 19 na pointi kwa kodi na vyanzo vingine kwa wawtz mil.45 kila mtu hadi Juni 2015 atachangia 800,000 kwa kijiji wastani wa watu 1500 ni mil 1200 zimelengwa kupatikana kwa kila kijiji. Sasa angalia ni mil ngapi zimepangwa ngazi ya kila kijiji na hiyo kata ya nyololo ikiwemo? Upinzani utawa elemisha maana shule za kata zimesaidia watu kuelimishwa kiurahisi. Laghai na asie laghai atafahamika.
 
Mnasali usiku na mchana watu wabaki bumbumbu ili muendelee kuwatawala. Kwa bajeti ya trilioni 19 na pointi kwa kodi na vyanzo vingine kwa wawtz mil.45 kila mtu hadi Juni 2015 atachangia 800,000 kwa kijiji wastani wa watu 1500 ni mil 1200 zimelengwa kupatikana kwa kila kijiji. Sasa angalia ni mil ngapi zimepangwa ngazi ya kila kijiji na hiyo kata ya nyololo ikiwemo? Upinzani utawa elemisha maana shule za kata zimesaidia watu kuelimishwa kiurahisi. Laghai na asie laghai atafahamika.
Hii siyo hoja bali ni shana tu watanzania kwa sasa karibu wote wanaulewa wanajua wanafanya nini pengine wewe ndiyo mburula.
 
Siasa siyo maneno bali ni vitendo vinavyopimwa katika chaguzi za kitaifa na ndogo kwenye sanduku la kura.

CCM haina muda wa kupambana na mashujaa wa maneno na propaganda katika nchi yao ya kufikirika yenye Rais wa kufikirika.

Kazi ya CCM na serikali yake ni kuongoza kwa vitendo na siyo kuongoza kwa maneno.

Kazi ya CCM ni kuibua na kuziweka (set) agenda za kitaifa katika taifa kwa maendeleo ya taifa huku vyama vya upinzani vikifuata.

CCM kwa sasa imezifunga hoja za upatikanaji wa Katiba Inayopendekezwa, kwa sasa iko kwenye hoja ya upigaji wa kura ya maoni. Kwa sasa CCM imewaachia wengine kazi ya kutafuta barabarani hoja za Katiba Inayopendekezwa.

CCM ni Itikadi, Falsafa, Sera na Ilani ya Uchaguzi inayotekelezeka.

Karibu sana katika ulimwengu wa CCM unakubaliwa na wananchi wengi nchini kama matokeo ya chaguzi mbali mbali yanavyobainisha.
naona umeandika porojo tupu, ama kweli siasa ni mchezo mchafu, ulimwengu mzima unafahamu jinsi ccm na mawakala wao wa kifisadi walivyochakachua maoni ya watanzania, na jinsi ilivyotumia mafisadi kama kina chenge kuhalalisha uchakachuaji wa maoni ya wananchi. Mikoa hiyo ya kusini ni moja ya mikoa ambayo ccm inawarubuni watanzania masikini wa huko ili wapate kura za kubaki madarakani kwa blah blah nyingi.
 
Siasa siyo maneno bali ni vitendo vinavyopimwa katika chaguzi za kitaifa na ndogo kwenye sanduku la kura.

CCM haina muda wa kupambana na mashujaa wa maneno na propaganda katika nchi yao ya kufikirika yenye Rais wa kufikirika.

Kazi ya CCM na serikali yake ni kuongoza kwa vitendo na siyo kuongoza kwa maneno.

Kazi ya CCM ni kuibua na kuziweka (set) agenda za kitaifa katika taifa kwa maendeleo ya taifa huku vyama vya upinzani vikifuata.

CCM kwa sasa imezifunga hoja za upatikanaji wa Katiba Inayopendekezwa, kwa sasa iko kwenye hoja ya upigaji wa kura ya maoni. Kwa sasa CCM imewaachia wengine kazi ya kutafuta barabarani hoja za Katiba Inayopendekezwa.

CCM ni Itikadi, Falsafa, Sera na Ilani ya Uchaguzi inayotekelezeka.

Karibu sana katika ulimwengu wa CCM unakubaliwa na wananchi wengi nchini kama matokeo ya chaguzi mbali mbali yanavyobainisha.

Unaweza kunipa idadi ya watanzania walompigia kikwete kura kwa hiyo ilani ya ccm katka uchaguzi wa 2010?
 
Back
Top Bottom