Environmental Security
Senior Member
- May 21, 2020
- 181
- 261
Hello
Mwaka 2010 aliyekuwa Rais wa Nigeria wakati huo hayati Umaru Musa Yar'Adua alifariki akiwa madarakani baada ya kuugua kwa muda mrefu, na kupelekea makamu wake mheshimiwa Goodluck Jonathan, kuongoza nchi hadi ulipofika uchaguzi mkuu ambapo yeye na chama chake tawala waliangushwa na mheshimiwa Buhari, hivyo upinzani ukachukua nchi.
Mwaka 2012, alifariki aliyekuwa Rais wa Ghana mheshimiwa Atta Mills, akiwa madarakani, hivyo kupelekea makamu wake mheshimiwa John Mahama kuongoza nchi hadi ulipofika uchaguzi mkuu ambapo yeye na chama chake tawala waliangushwa na mheshimiwa Nana Akufo Ado ambaye ndiye rais wa sasa wa Ghana hivyo upinzani ukachukua nchi
Mwaka 2012, alifariki aliyekuwa Rais wa Malawi, mheshimiwa Bingu Wamutharika, akiwa madarakani hivyo kupelekea makamu wake mheshimiwa Joyce Banda kuongoza nchi hadi ulipofika uchaguzi mkuu ambapo yeye na chama chake tawala waliangushwa na mheshimiwa Profesa Peter Mutharika, hivyo upinzani ukachukua nchi
Mwaka 2008 , alifariki aliyekuwa Rais wa Zambia mheshimiwa Levy Mwanawasa akiwa madarakani, hivyo kupelekea makamu wake mheshimiwa Rupia Banda kuongoza nchi hadi ulipofika uchaguzi mkuu ambapo yeye na chama chake tawala waliangushwa na mheshimiwa Michael Sata (king cobra), hivyo upinzani ukachukua nchi
Mheshimiwa Michael Sata, naye alifariki akiwa madarakani hivyo kupelekea makamu wake mheshimiwa Guy Scot, kwa kipindi kifupi sana kutokana na changamoto za kikatiba ambazo hazikumruhusu kubakia kama Rais wa nchi, hivyo kupelekea nchi kuingia mikononi mwa mheshimiwa Edgar Lungu akiwa mrithi rasmi wa Michael Sata, lakini naye kama tunavyojua, mara tu baada ya uchaguzi ameangushwa vibaya sana na mheshimiwa Rais Haikande Hichilema hivyo upinzani ukachukua nchi.
Tanzania pia, Rais aliyekuwepo alifariki akiwa madarakani, hivyo kupelekea makamu wake kuongoza nchi akiwa ndiye Rais kwa mujibu wa katiba.
Swali ni he! Historia itaendelea kuandikwa Africa kama ilivyokwisha tokea kwa mataifa wenzetu au context ya Tanzania ni tofauti kabisa na hao, au tusubiri wakati ufike..!!??
Karibuni.
Mwaka 2010 aliyekuwa Rais wa Nigeria wakati huo hayati Umaru Musa Yar'Adua alifariki akiwa madarakani baada ya kuugua kwa muda mrefu, na kupelekea makamu wake mheshimiwa Goodluck Jonathan, kuongoza nchi hadi ulipofika uchaguzi mkuu ambapo yeye na chama chake tawala waliangushwa na mheshimiwa Buhari, hivyo upinzani ukachukua nchi.
Mwaka 2012, alifariki aliyekuwa Rais wa Ghana mheshimiwa Atta Mills, akiwa madarakani, hivyo kupelekea makamu wake mheshimiwa John Mahama kuongoza nchi hadi ulipofika uchaguzi mkuu ambapo yeye na chama chake tawala waliangushwa na mheshimiwa Nana Akufo Ado ambaye ndiye rais wa sasa wa Ghana hivyo upinzani ukachukua nchi
Mwaka 2012, alifariki aliyekuwa Rais wa Malawi, mheshimiwa Bingu Wamutharika, akiwa madarakani hivyo kupelekea makamu wake mheshimiwa Joyce Banda kuongoza nchi hadi ulipofika uchaguzi mkuu ambapo yeye na chama chake tawala waliangushwa na mheshimiwa Profesa Peter Mutharika, hivyo upinzani ukachukua nchi
Mwaka 2008 , alifariki aliyekuwa Rais wa Zambia mheshimiwa Levy Mwanawasa akiwa madarakani, hivyo kupelekea makamu wake mheshimiwa Rupia Banda kuongoza nchi hadi ulipofika uchaguzi mkuu ambapo yeye na chama chake tawala waliangushwa na mheshimiwa Michael Sata (king cobra), hivyo upinzani ukachukua nchi
Mheshimiwa Michael Sata, naye alifariki akiwa madarakani hivyo kupelekea makamu wake mheshimiwa Guy Scot, kwa kipindi kifupi sana kutokana na changamoto za kikatiba ambazo hazikumruhusu kubakia kama Rais wa nchi, hivyo kupelekea nchi kuingia mikononi mwa mheshimiwa Edgar Lungu akiwa mrithi rasmi wa Michael Sata, lakini naye kama tunavyojua, mara tu baada ya uchaguzi ameangushwa vibaya sana na mheshimiwa Rais Haikande Hichilema hivyo upinzani ukachukua nchi.
Tanzania pia, Rais aliyekuwepo alifariki akiwa madarakani, hivyo kupelekea makamu wake kuongoza nchi akiwa ndiye Rais kwa mujibu wa katiba.
Swali ni he! Historia itaendelea kuandikwa Africa kama ilivyokwisha tokea kwa mataifa wenzetu au context ya Tanzania ni tofauti kabisa na hao, au tusubiri wakati ufike..!!??
Karibuni.