African Albinos become prey

Niliiona hii video kweny CNN jana, for sure hii ni aibu kwa taifa. Kuna hatari hata kiongozi wa nchi siku moja akaenda U.S, CNN au NBC wakam-reffer "this is the president of the country where albinos are hunted"
Mi nafkr hili tatizo llikuwa limeanza siku nyingi sbb enzi hizo za utoto tulikuwa tunaambiwa Albino(Zeruzeru) hawafi ila wanapotea, sasa swali la kujiuliza walikuwa wanaenda wapi??
Kwa mtazamo wangu hakukuwa na haja ya viongozi wa serikali kusimama majukwaani ya kuligeuza swala hili la kisiasa, ninaamini tunayo itelligence ya kutosha ambayo tungeitumia kimyakimya tungefanikiwa kumpata mmoja mjoja, hasa wale wanunuzi wa hiyo biashara.
Siamini kama hii kura ya maoni itafanikiwa sana labda kura hizi zingepigwa kwa njia ya mtandao au kwa SMS ambapo wananchi popote walipo wangetuma majina kwenda namba fulani wakieleza kijiji wilaya na mkoa huyo muhalifu alipo, data zingekusannywa na wauaji wangepatikana kiurahisi. Hii ingewafanya wanachi kuwa huru, kuliko hii system ya sasa ya kwenda kituoni kwani wanachi wanahofia usalama wao, ukichukua mfano rahisi ambapo diwani mmoja dodoma aliamua kuchana karatasi yake baada ya kugundua kuwa vikaratasi vilikuwa vinahidhiwa kwenye ndoo hivyo hakukuwa na usiri wowote hapo.
Ingewezekana tu **** hizo SMS ikawa bure na kila mtu angeweza kupiga kura mara moja au mbili tu, ili kuzuia kupoteza lengo kwani wengine wangejaribu kupiga kura mara nyingi.
Vinginevyo hili jambo litaendelea kututia aibu na kutufanya tuonekane watu wa ajabu, na itafika wakati mtu utakutakuwa ukiona aibu kutaja nchi yako ukiwa abroad sbb ya haibu kubwa kama hii.
 
Back
Top Bottom