FYATU
JF-Expert Member
- Dec 7, 2011
- 5,867
- 5,064
Waafrika ni jamii tuliyokwisha ithibitishia Dunia na hata kujithibitishia wenyewe kuwa kuna tija ndogo sana kutoka Viongozi wao.
Chaguzi zimekuwa vichaka tu, ndio maana leo utashangaa nchi iliyotawaliwa na Kiongozi mmoja miaka 40 siku anapinduliwa ndio utawasikia wananchi wanashukuru kwamba walishachoka,na chaguzi zilikuwepo na huyo Raisi alikuwa anashinda tu kwa kishindo.
Na si kwamba eti anayeingia ataleta unafuu,la hasha mambo yanaweza kuwa yaleyale au hata kuharibika zaidi.
Uongozi umekuwa mali ya kundi fulani tu, ikitokea wanahitilafiana na Wenzao basi nchi itatumbukia kwenye vikundi vya uasi.
Ni bora Afrika kuajiri Mameneja kwa taaluma zao bila kujali wanatokea nchi au bara gani,wasimamie rasilimali na raia wagawane kwa haki.
Chaguzi zimekuwa vichaka tu, ndio maana leo utashangaa nchi iliyotawaliwa na Kiongozi mmoja miaka 40 siku anapinduliwa ndio utawasikia wananchi wanashukuru kwamba walishachoka,na chaguzi zilikuwepo na huyo Raisi alikuwa anashinda tu kwa kishindo.
Na si kwamba eti anayeingia ataleta unafuu,la hasha mambo yanaweza kuwa yaleyale au hata kuharibika zaidi.
Uongozi umekuwa mali ya kundi fulani tu, ikitokea wanahitilafiana na Wenzao basi nchi itatumbukia kwenye vikundi vya uasi.
Ni bora Afrika kuajiri Mameneja kwa taaluma zao bila kujali wanatokea nchi au bara gani,wasimamie rasilimali na raia wagawane kwa haki.