Nyie peke yenu ndio msiojua game.....mimi nimezaliwa na kukulia uswazi.Ukisikia mtu kaenda shamba Pakistan...maana yake ameenda kuchukua mzigo(heroin/Opium),kwenye boda ya Pakistan na Afghanistan.Hii tangu zamani sana(I'm talking about eighties).Ila wanadhani haya mambo yameanza leo.
Agree!....zamani walikuwa wana trffic juu kwa juu,siku hizi wanauza Bongo na Zanzibar.Wameharibu na kuua marafiki zangu wengi sana!!Hakuna asiyoyajuwa hayo ila sasa yamezidi, tumeona mpaka wachungaji wakishikwa kwa kufanya hii biashara haram, tumesikia makanisa na bakwata wakihusika kwa namna moja au nyingine, hiyo pekee inaonesha kuwa hii biashara imeshamiri na inabidi ishikiwe bango ili isambaratishwe hapa kwetu.
Tunaona jinsi vijana, watoto (chini ya miaka 18) na wazee wakiathirika kwa haya maunga. Tushirikiane kwa nguvu zote kupiga vita hii biashara inayoangamiza vizazi.
Do we have any rehab programs for the victims of substance abuse?Agree!....zamani walikuwa wana trffic juu kwa juu,siku hizi wanauza Bongo na Zanzibar.Wameharibu na kuua marafiki zangu wengi sana!!
Rehab??....I don't know man!,sounds too complicated.Do we have any rehab programs for the victims of substance abuse?
Hakuna asiyoyajuwa hayo ila sasa yamezidi, tumeona mpaka wachungaji wakishikwa kwa kufanya hii biashara haram, tumesikia makanisa na bakwata wakihusika kwa namna moja au nyingine, hiyo pekee inaonesha kuwa hii biashara imeshamiri na inabidi ishikiwe bango ili isambaratishwe hapa kwetu.
Tunaona jinsi vijana, watoto (chini ya miaka 18) na wazee wakiathirika kwa haya maunga. Tushirikiane kwa nguvu zote kupiga vita hii biashara inayoangamiza vizazi.
Habari inatoka hapa: http://www.habaritanzania.com/articles/2667/1/Serikali-yaficha-majina-ya-vigogo-wauza-%91unga%92
Serikali yaficha majina ya vigogo wauza ‘unga'
By Habari Tanzania | Published 01/22/2007
Na Charles Mullinda
MAJINA ya vigogo wanaotuhumiwa kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya, yaliyowasilishwa na Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Amina Chifupa katika Wizara ya Usalama wa Raia na kwa Rais Jakaya Kikwete, yataendelea kuwa siri.
Akizungumza na gazeti hili ofisini kwake mwishoni mwa wiki iliyopita, Naibu Waziri wa Usalama wa Raia, Mohammed Aboud, alisema kuwa, wizara yake haina mpango wa kuyatangaza majina yaliyomo katika orodha hiyo.
Aliliambia gazeti hili kuwa, hakuna kiongozi yeyote nje ya wizara hiyo asiyehusika na taasisi za usalama, ambaye ameiona orodha halisi ya majina ya watu waliotajwa katika barua aliyotumiwa Rais Kikwete.
Alisema baada ya kupokea majina hayo, upelelezi ulianza mara moja na wananchi watarajie kuona matokeo ya kazi hiyo, hivi karibuni.
Aboud alisema, baada ya Rais Kikwete kupokea orodha ya majina hayo na kuyawasilisha kwa Waziri wa Usalama wa Raia, Bakari Mwapachu, ambaye pia alikayabidhi kwa viongozi wa juu wa Jeshi la Polisi kwa ajili ya kufanyiwa kazi, uchunguzi ulianza kufanywa kwa tahadhari kubwa na usiri, ili kutoharibu ushahidi.
Alisema baada ya kuanza kwa uchunguzi huo, ilibainika kuwa, kunahitajia usiri wa hali ya juu, ili kufanikisha kazi hiyo kwa ufanisi, kwa sababu wauzaji dawa za kulevya ni wajanja na wenye uwezo mkubwa kipesa, hivyo ni rahisi kuharibu ushahidi.
"Tunachukua hatua kwa uangalifu sana, vinginevyo tutaharibu, tunawaomba wananchi wawe wastahamilivu, vita inaendelea na sisi tunaelekea kushinda, lakini hatutataja mtu miongoni mwa wote waliotajwa.
"Watuhumiwa waliotajwa katika orodha iliyopelekwa kwa Rais Kikwete ni wengi na aliowataja Amina nao ni wengi, lakini watabaki kuwa siri, si kwa sababu yoyote mbaya ila ni kwa mujibu wa taratibu za kufuatilia kesi za aina hii," alisema Aboud.
Alisema vyombo vya usalama vinafuatilia kila mtu aliyetajwa kwa makini na uangalifu na vikithibitisha kuwa anahusika, anakamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria.
Aboud alisema, hatua iliyofikiwa ni kubwa na wengi wa waliotajwa wamekwishachunguzwa. Aliahidi kuwa, mpaka mwishoni mwa mwezi wa Februari, wananchi watashuhudia hatua kubwa zitakazokuwa zimechukuliwa dhidi ya wale watakaokuwa wamethibitika kuhusika na biashara hiyo.
....inaendelea....
Inatoka hapa: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/257-majina-ya-wauza-madawa-ya-kulevya-jk-anayo-4.html
Vigogo dawa za kulevya watajwa
Written by Mwananchi
Monday, 18 September 2006
*Majina yao yapelekwa kwa Rais Kikwete
*Ni orodha ndefu ya majina ya watu 58
*Wamo wafanyabishara, wanasiasa, viongozi wa dini
*Mbinu wanazotumia nazo zaanikwa hadharani
WITO wa Rais Jakaya Kikwete wa kutaka wananchi wajitokeze kutaja majina ya wahalifu nchini, umepata mwitikio mpya, safari hii watu kadhaa wakijitokeza kutaja majina ya vigogo wanaoongoza kwa biashara ya dawa za kulevya nchini.
Majina hayo yako katika barua iliyoandikwa na wananchi 15 kwenda kwa Rais Kikwete, ambamo wanadai kwamba walikuwa wakitumiwa na vigogo hao kufanya biashara hiyo, lakini sasa wameamua kuachana nayo. Barua hiyo iliandikwa Septemba 8, mwaka huu na wahusika wanadai wamekwisha kuiwasilisha Ikulu.
Kwa mujibu wa barua hiyo, majina 58 yameorodheshwa yakiwa katika makundi matatu makubwa, la kwanza likiwa ni waagizaji wakubwa wa dawa hizo; la pili ni wafadhili ambao majina yao hutumika kusafirisha dawa hizo; na la tatu ni wauzaji walioko Dar es Salaam, Tanga, Mwanza, Mbeya na Zanzibar.
Katika orodha ya waandishi wa barua hiyo wanaodai kusukumwa na uzalendo na uchungu kwa nchi yao, yamo majina ya wafanyabiashara maarufu nchini na wanasiasa, wakuu wa taasisi nyeti, baadhi ya viongozi wa dini na maafisa wa juu serikalini.
Kundi la kwanza lina majina 12, miongoni mwao ni wafanyabiashara maarufu katika miji ya Dar es Salaam, Morogoro, Zanzibar, Arusha na Bagamoyo na baadhi ya viongozi wa dini wa madhehebu fulani.
Kundi hili linadaiwa kuwa linaingiza dawa za kulevya kwa njia mbalimbali zikiwamo, kutumia mipira ya kondomu, majokofu, vifaa vya hospitali, meli na marobota ya mitumba.
Katika kundi la pili kuna watu 19, miongoni mwao wamo wanasiasa wakubwa nchini wakiongoza kundi hili, kutoka taasisi ya fedha nchini na wafanyabiashara maarufu wa Dar es Salaam na Zanzibar.
Kundi la tatu lina majina 27, ambao si ya watu wenye majina makubwa, lakini ndio wanaotumika kusambaza mitaani kwa watumiaji wa dawa za kulevya.
Mbali ya kushiriki katika kusambaza dawa za kulevya, kundi hili pia lina baadhi ya majina ya watu waliotajwa kushiriki katika kuingiza silaha nzito zinazotumika kwa ajili ya ujambazi kutoka nchi jirani.
...inaendelea...
Do we have any rehab programs for the victims of substance abuse?
Inabidi Makanisa na Bakwata wachunguzwe kwa kina.