AFCON ni mashindano ya nguvu, kujituma, utimamu wa mwili na akili kiasi

Kamgomoli

JF-Expert Member
May 3, 2018
1,865
3,802
Nimefatilia vizuri mashindano ya AFCON yanayoendelea kule Ivory cost, nikagundua kama huna wachezaji ambao wako fiti kwa maana ya nguvu, utimamu wa mwili,wenye maumbo makubwa na waonajituma ni ngumu kushinda mechi. Lazima uwe na wachezaji ambao wako fiti kweli kweli na wenye "spirit" ya kulazimisha mambo yatokee bila kujali zimebaki dk ngapi. Ndio maana tumeshuhudia matokeo ya kushangaza.

Timu yetu inawacheza wengi ambao hawawezi kupambania "dual balls".Pia wengi ni wafupi na hawana utimamu wa mwili wa kutosha kumudu kucheza dk 90 zenye mbilinge mbilinge. Fikiria unamtoa Kibu Denis halafu unamuingiza Charles Mmombwa, halafu mechi imechafuka Zambia wanalitaka goli wapi na wapi!!:oops:. Kwenye timu yetu tuna wachezaji wachache sana wenye nguvu na spirit ya kupambana mfano Kibu Denis, Ibrahimu Baka, Mzamiru, Novatus na Himidi Mao. Wengine na wazuri tukiwa na mpira basi "the likes of Feitoto"

Wapo wachezaji ambao huwa tunawachukulia poa lakini kwenye haya mashindano ya mechi 3 muhimu wangeweza kutusaidia. Mfano Laurent Lusajo, Tariq Seif, Masawe( japo umri umeenda), Charles Ilafya na Kelvin Kijili. Hawa ni baadhi ya wachezaji wachache tulionao ambao wana maumbo na makubwa na roho ya upambanaji, japo wanaweza wasiwe wazuri wa kuuchezea mpira. Ndio Ditramu Chimbi katika ubora wake aliwahi kuwa mchezaji muhimu sana kwenye timu yetu.

Kutokana kukosa wachezaji wa aina hii ndio maana inakuwa vigumu Taifa Stars kufunga magoli ya kona au faulo ila ni rahisi sana sisi kufungwa magoli ya aina hiyo. Ni kweli wenzetu wametuacha ila tumeshuhudia timu za viwango vyetu zikifanya maajabu ya kuwapiga vigogo kutokana na kutumia wachezaji wenye hizo sifa nilizozieleza. Nadhani somo limetuingia. Next time viongozi na benchi la ufundi wawe makini kwenye "selection" ya wachezaji. Kwenye timu ya Taifa ufundi na kipaji cha kuuchezea mpira havitoshi kupata matokeo. Ni zaidi ya hivyo. Nawasilisha.

Sent from my SM-G955U using JamiiForums mobile app
 
Pamoja na kwamba una hoja ya msingi kwenye suala zima la kujituma ila Senegal hawana wachezaji wenye maumbile makubwa na hawana historia ya kuwa na wachezaji hao ila ni top rated timu ya Afrika. Ghana pia hivyo hivyo ila wanaangushwaga na mapuuza yao. Wakati timu zenye wachezaji wenye maumbile makubwa kama Cameroon na Nigeria hawana maajabu yoyote siku hizi.

Kuna uzi nilifikiria kuja kuuleta kuhusu suala hili ila ngoja niseme hapa hapa. Vijana wenye nguvu na maumbile yanayofaa kwa michezo ambao wangeweza kuisaidia Tanzania kwenye michezo wote wanakimbilia jeshini maana mifumo yetu ya michezo haitoi taswira nzuri ya kuwepo fursa nzuri za kujenga maisha ya uhakika. Ndiyo maana tunaishia na hao wachezaji unaosema. Nikitulia siku nyingine nitalielezea hili vizuri zaidi.
 
Pamoja na kwamba una hoja ya msingi kwenye suala zima la kujituma ila Senegal hawana wachezaji wenye maumbile makubwa na hawana historia ya kuwa na wachezaji hao ila ni top rated timu ya Afrika. Ghana pia hivyo hivyo ila wanaangushwaga na mapuuza yao. Wakati timu zenye wachezaji wenye maumbile makubwa kama Cameroon na Nigeria hawana maajabu yoyote siku hizi.

Kuna uzi nilifikiria kuja kuuleta kuhusu suala hili ila ngoja niseme hapa hapa. Vijana wenye nguvu na maumbile yanayofaa kwa michezo ambao wangeweza kuisaidia Tanzania kwenye michezo wote wanakimbilia jeshini maana mifumo yetu ya michezo haitoi taswira nzuri ya kuwepo fursa nzuri za kujenga maisha ya uhakika. Ndiyo maana tunaishia na hao wachezaji unaosema. Nikitulia siku nyingine nitalielezea hili vizuri zaidi.
Colibary.koyate.mendy.sarr ile team ya Senegal magaint ni mengi mno sijui unasemea Senegal ipi
 
Pamoja na kwamba una hoja ya msingi kwenye suala zima la kujituma ila Senegal hawana wachezaji wenye maumbile makubwa na hawana historia ya kuwa na wachezaji hao ila ni top rated timu ya Afrika. Ghana pia hivyo hivyo ila wanaangushwaga na mapuuza yao. Wakati timu zenye wachezaji wenye maumbile makubwa kama Cameroon na Nigeria hawana maajabu yoyote siku hizi.

Kuna uzi nilifikiria kuja kuuleta kuhusu suala hili ila ngoja niseme hapa hapa. Vijana wenye nguvu na maumbile yanayofaa kwa michezo ambao wangeweza kuisaidia Tanzania kwenye michezo wote wanakimbilia jeshini maana mifumo yetu ya michezo haitoi taswira nzuri ya kuwepo fursa nzuri za kujenga maisha ya uhakika. Ndiyo maana tunaishia na hao wachezaji unaosema. Nikitulia siku nyingine nitalielezea hili vizuri zaidi.
Senegal hawana wachezaji wenye maumbile makubwa na hawana historia ya kuwa na wachezaji hao ila ni top

Chief futa hii kauli wachezaji wa senegal asilimia 80 wana miili mikubwa na hii tokea zamani enzi za akina papa bouba diop

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Colibary.koyate.mendy.sarr ile team ya Senegal magaint ni mengi mno sijui unasemea Senegal ipi

Senegal hawana wachezaji wenye maumbile makubwa na hawana historia ya kuwa na wachezaji hao ila ni top

Chief futa hii kauli wachezaji wa senegal asilimia 80 wana miili mikubwa na hii tokea zamani enzi za akina papa bouba diop

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
Hapa nadhani tunaongelea wastani wa maumbile ya wachezaji na haimaanishi kuwa hizo timu hazina kabisa wachezaji wenye vimo au maumbile makubwa.

Ukijikita kwenye wastani, ni wazi wachezaji wa Senegal na Ghana wana maumbile ya kawaida kulinganisha na wa Cameroon, Ivory Coast au hata Nigeria. Njia nyingine ya haraka ni kuangalia vimo na maumbile ya best players wa timu hizo katika miaka yote.

Nafikiri tunadharau maana nzima ya "kuujua mpira". Hata hawa wachezaji wetu tunaowasifiaga wana vipaji baadae tunakuja kugundua hawaujui mpira na hawana msingi ule basic kabisa wa kuujua mpira wenyewe ukilinganisha na madogo wa Senegal, Ghana au Brazil. Kuna kitu hatuwapi wachezaji wetu wanapokuwa bado wanacheza soka la mtaani.
 
Tatizo la Taifa Stars ni backpass hata Yanga tuna huu upuuzi pia. Tatizo jingine tumeenda kuokoteza wachezaji diaspora wanaocheza ligi daraja la nne. Kwani ni lazima timu iwe na wachezaji ambao hatuna uhakika kama kweli ni raia wa Tz?? Mara mia tungewachukua hata kina Chasambi na Shekhan.
 
Tatizo la Taifa Stars ni backpass hata Yanga tuna huu upuuzi pia. Tatizo jingine tumeenda kuokoteza wachezaji diaspora wanaocheza ligi daraja la nne. Kwani ni lazima timu iwe na wachezaji ambao hatuna uhakika kama kweli ni raia wa Tz?? Mara mia tungewachukua hata kina Chasambi na Shekhan.
Kuchukua wachezaji wazuri nje siyo jambo baya hasa wale wanaoonekana wana potential kweli. Ukiniuliza mimi hao ndiyo wanacheza kwa kupambana zaidi maana wanajua impact kwenye career zao kama watafanya vizuri iko wazi tofauti na hawa wa Simba, Yanga au Azam ambao ni kama wameridhika na hawana mpango wa kwenda zaidi ya walipofikia. Ila cha msingi tungezingatia quality ule mchujo tuliokuwa tunafanya tumekuja kuutelekeza dakika za mwisho kwa sababu za kiswahili.

Ila nakubaliana na wewe kwenye suala la kuwapa exposure madogo ambao ndiyo kizazi kipya tutakachotakiwa kukitegemea baada tu AFCON hii. Hili niliwahi kulishauri wakati fulani. Cha kushangaza AFCON ijayo na qualification ya kombe la dunia utaona tunawategemea hawa hawa kina Msuva, Zimbwe na Samatta.
 
Nimefatilia vizuri mashindano ya AFCON yanayoendelea kule Ivory cost, nikagundua kama huna wachezaji ambao wako fiti kwa maana ya nguvu, utimamu wa mwili,wenye maumbo makubwa na waonajituma ni ngumu kushinda mechi. Lazima uwe na wachezaji ambao wako fiti kweli kweli na wenye "spirit" ya kulazimisha mambo yatokee bila kujali zimebaki dk ngapi. Ndio maana tumeshuhudia matokeo ya kushangaza.

Timu yetu inawacheza wengi ambao hawawezi kupambania "dual balls".Pia wengi ni wafupi na hawana utimamu wa mwili wa kutosha kumudu kucheza dk 90 zenye mbilinge mbilinge. Fikiria unamtoa Kibu Denis halafu unamuingiza Charles Mmombwa, halafu mechi imechafuka Zambia wanalitaka goli wapi na wapi!!:oops:. Kwenye timu yetu tuna wachezaji wachache sana wenye nguvu na spirit ya kupambana mfano Kibu Denis, Ibrahimu Baka, Mzamiru, Novatus na Himidi Mao. Wengine na wazuri tukiwa na mpira basi "the likes of Feitoto"

Wapo wachezaji ambao huwa tunawachukulia poa lakini kwenye haya mashindano ya mechi 3 muhimu wangeweza kutusaidia. Mfano Laurent Lusajo, Tariq Seif, Masawe( japo umri umeenda), Charles Ilafya na Kelvin Kijili. Hawa ni baadhi ya wachezaji wachache tulionao ambao wana maumbo na makubwa na roho ya upambanaji, japo wanaweza wasiwe wazuri wa kuuchezea mpira. Ndio Ditramu Chimbi katika ubora wake aliwahi kuwa mchezaji muhimu sana kwenye timu yetu.

Kutokana kukosa wachezaji wa aina hii ndio maana inakuwa vigumu Taifa Stars kufunga magoli ya kona au faulo ila ni rahisi sana sisi kufungwa magoli ya aina hiyo. Ni kweli wenzetu wametuacha ila tumeshuhudia timu za viwango vyetu zikifanya maajabu ya kuwapiga vigogo kutokana na kutumia wachezaji wenye hizo sifa nilizozieleza. Nadhani somo limetuingia. Next time viongozi na benchi la ufundi wawe makini kwenye "selection" ya wachezaji. Kwenye timu ya Taifa ufundi na kipaji cha kuuchezea mpira havitoshi kupata matokeo. Ni zaidi ya hivyo. Nawasilisha.

Sent from my SM-G955U using JamiiForums mobile app

Tena Kijili kwenye ile mbavu ya kulia na ule mwendo angetufaa saana
 
Back
Top Bottom