Ada shule binafsi imezidi kupaa, mpango wa Ada elekezi ya Serikali umeyeyuka?

sirluta

JF-Expert Member
Nov 28, 2012
6,325
2,491
Serikali ilitangaza kutoa ada elekezi kwa shule za watu binafsi ili kupunguza gharama kubwa wanazotozwa wazazi wanaosomesha watoto wao katika shule hizo.

Zamani ilikuwa watoto wanaofaulu kwenda sekondari, walisoma sekondari za serikali na zile za binafsi walienda kusoma wale waliokosa alama za juu za kujiunga na shule hizo. Uvurugaji ulipokuja, ikawa kinyume chake kuwa wanaopata alama za juu husoma sekondari za binafsi na wenye alama za chini na wazazi wao kuwa na kipato kidogo ndio husoma za serikali. Ni vema hadhi ya shule za serikali ikarudi kwa kuzibana shule binafsi maana wameifanya elimu kuwa biashara na siyo huduma.

Zipo shule za awali na sekondari katika mhula huu licha ya shule za serikali kufuta ada na michango, wao wamepandisha ada na michango zaidi. Hali ya utoaji elimu katika baadhi ya shule siyo nzuri.

Mfano kuna shule moja hapa Arusha mtoto wa darasa la tatu mbali na ada kupanda, anahitaji kwenda na kaunta book 19 ambapo ana masomo 12, na hayo 6 ni ya majaribio na mazoezi na moja ni la akiba. Sijui shule zingine ila je mtoto huyu ambaye hata miaka 10 hana ataweza kumudu masomo yote hayo? Mfumo wa utoji elimu ni rafiki kwa watoto?

**Raisi wetu ada elekezi tafadhali.
**Waziri wa Elimu mitaala rafiki ya Elimu tafadhali

Nawasilisha
 
Hili utekelezaji wake mgumu mkuu, waboreshe tu shule za serikali mambo mengine yote yatajiseti yenyewe bila shurti. Halafu ujue wamiliki wa hizi shule ndo hao hao viongozi wa serikali unaowapelekea hiki kilio.
 
Mkuu unataka kunambia ilikuwa nguvu ya soda .
Umeona jipya lipi katika hizi harakati?

Hakuna jipu wala kipele hapo wamebaki kufukuza kazi watu bila kufuata taratibu za ajira, mi naona hili ndilo jipu kutofuata sheria za ajira ni uonevu na mawaziri hawa wangewajibishwa, kugusa shule za watu hawathubutu, wameshindwa za serikali wakae kimya, walisema biashara huria ndio haya sasa.
 
Dawa ni kupiga marufuku watoto wa viongozi wa serikali kusoma shule binafsi au kuwapeleka nje kusoma na kutibiwa, hapo utaona huduma zitakavyoboreshwa mashuleni na hospitali za umma.

Tuanzie hapo kwanza kwa kujaribu.
 
Shule binafsi ni mali binafsi kama shughuli nyingine binafsi. Ukiweza nenda, ukishindwa acha. Unataka vitu vya chee?

Unategemea FEZA,nk ziwe laki nane?
Hakuna serikali inaweza fanya hayo makosa.
Huko ni kuielewa vibaya serikali.
 
Yaani shule za binafsi wanapandisha ovyo ovyo ada na michango kila Siku, kila wanapojisikia, utafikiri nchi hii haina serikali.

Elimu ya sekondari millioni 4 na zaidi kwa mwaka. serikali lazima iingilie kati. Kwa kuwatumia wataalam kufanya utafiti kubaini kiasi gani ni ada halali name shule itakayokiuka ifungiwe.

Name sisi wazazi tutatoa taarifa wakikaidi.
 
Acha kujifrastrate. Option ziko nyingi. Ziko shule kuanzia milioni kwa mwaka mpaka m8.

Lakini mtoto akija akakugongea sigara usilalalamike. Usagaji/ushoga/kunguni ni mambo ya kawaida kwenye hizi shule za urojo.

Jamani kama uwezo unaruhusu punguza matumizi somesha mtoto shule nzuri.
 
Dawa ni kupiga marufuku watoto wa viongozi wa serikali kusoma shule binafsi au kuwapeleka nje kusoma na kutibiwa, hapo utaona huduma zitakavyoboreshwa mashuleni na hospitali za umma.
Tuanzie hapo kwanza kwa kujaribu.
Hii ndio dawa mulua kabisa, kama walivyopigwa marufuku kupanda ndege kwenda ulaya hivyo hivyo we hata kwenye elimu.

Leo nimepeleka mtoto shule naamabiwa hakuna cha magufuli walala babake na magufuli ada ya mtoto iko pale pale kama hutaki kampeleke mwanao ikulu mama Magu si mwalimu akaufundishie.
 
Hauwezi kueka bei elekezi katika kitu ambacho sio commodity!

Yaani unaweza kuweka bei elekezi kwenye petroli kwa vile ni ile ile kila pump.
Elimu ni tofauti kila shule jinjsi inavyokuwa delivered hata kama syllabus ni ile ile, kama pale IST kuna indoor basketball court, 2 swimming pools, kiwanja kamili cha mpira, studio za muziki etc sasa bei yao itakuwaje sawa na shule zengine? IST ni extreme case ila shule zote binafsi zinajitofautisha kwa quality na mazingira ya elimu yao na mteja yupo huru kuchagua ni shule ipi inamfaa.

Serikali iboresha shule zake ili kumpeleka mtoto private iwe ni kutafuta huduma za ziada tu.
 
Walipotangaza bei elekezi mlipiga kelele serikali inaingilia mashule bila kuangalia hali halisi. Wamewaacha mpigwe hizo ada napo mnalalamika hivi watanzania nani aliwaroga mbona mnakuwa wanafiki hivi?

Kama ada imekuwa kubwa mrudishe serikalini ada bure
 
Ili upate kazi kwa Tanzania,ukiondoa magumashi mengine ni lazima uwe na cheti,tunaajiliwa kwa kuwa na ufaulu wa alama ktk cheti.

Mimi au mzaz mwingine anataka mtoto wake afaulu apate cheti ili aweze kupata kazi ukitaka ada elekez ujue mwanao anafeli,utakuta hiyo shule haina hata walimu na vifaa vingine vya kujifunzia.Labda useme serikali itoe ruzuku kwenye shule binafs,halafu utoe ada elekez.

Mbona serikal inatoa elimu bure,mpeleke huko akapate bora elimu.
 
Serikali ilitangaza kutoa ada elekezi kwa shule za watu binafsi ili kupunguza gharama kubwa wanazotozwa wazazi wanaosomesha watoto wao katika shule hizo.

Zamani ilikuwa watoto wanaofaulu kwenda sekondari, walisoma sekondari za serikali na zile za binafsi walienda kusoma wale waliokosa alama za juu za kujiunga na shule hizo. Uvurugaji ulipokuja, ikawa kinyume chake kuwa wanaopata alama za juu husoma sekondari za binafsi na wenye alama za chini na wazazi wao kuwa na kipato kidogo ndio husoma za serikali. Ni vema hadhi ya shule za serikali ikarudi kwa kuzibana shule binafsi maana wameifanya elimu kuwa biashara na siyo huduma.

Zipo shule za awali na sekondari katika mhula huu licha ya shule za serikali kufuta ada na michango, wao wamepandisha ada na michango zaidi. Hali ya utoaji elimu katika baadhi ya shule siyo nzuri.

Mfano kuna shule moja hapa Arusha mtoto wa darasa la tatu mbali na ada kupanda, anahitaji kwenda na kaunta book 19 ambapo ana masomo 12, na hayo 6 ni ya majaribio na mazoezi na moja ni la akiba. Sijui shule zingine ila je mtoto huyu ambaye hata miaka 10 hana ataweza kumudu masomo yote hayo? Mfumo wa utoji elimu ni rafiki kwa watoto?

**Raisi wetu ada elekezi tafadhali.
**Waziri wa Elimu mitaala rafiki ya Elimu tafadhali

Nawasilisha
Mliozaa watoto vichwa maji mtakoma, sisi tuliozaa vipanga tumewapeleka shule za bure na bado wanapasua mitihani
 
L
Serikali ilitangaza kutoa ada elekezi kwa shule za watu binafsi ili kupunguza gharama kubwa wanazotozwa wazazi wanaosomesha watoto wao katika shule hizo.

Zamani ilikuwa watoto wanaofaulu kwenda sekondari, walisoma sekondari za serikali na zile za binafsi walienda kusoma wale waliokosa alama za juu za kujiunga na shule hizo. Uvurugaji ulipokuja, ikawa kinyume chake kuwa wanaopata alama za juu husoma sekondari za binafsi na wenye alama za chini na wazazi wao kuwa na kipato kidogo ndio husoma za serikali. Ni vema hadhi ya shule za serikali ikarudi kwa kuzibana shule binafsi maana wameifanya elimu kuwa biashara na siyo huduma.

Zipo shule za awali na sekondari katika mhula huu licha ya shule za serikali kufuta ada na michango, wao wamepandisha ada na michango zaidi. Hali ya utoaji elimu katika baadhi ya shule siyo nzuri.

Mfano kuna shule moja hapa Arusha mtoto wa darasa la tatu mbali na ada kupanda, anahitaji kwenda na kaunta book 19 ambapo ana masomo 12, na hayo 6 ni ya majaribio na mazoezi na moja ni la akiba. Sijui shule zingine ila je mtoto huyu ambaye hata miaka 10 hana ataweza kumudu masomo yote hayo? Mfumo wa utoji elimu ni rafiki kwa watoto?

**Raisi wetu ada elekezi tafadhali.
**Waziri wa Elimu mitaala rafiki ya Elimu tafadhali

Nawasilisha
ni vizuri tukamshukuru Rais wetu Magufuli kwa kuhakikisha elimu bure kwa shule za Serikali kuanzia msingi hadi Sekondari.

Nina hakika atasimamia kuhakikisha elimu ya shule za Serikali ambazo zina wanafunzi wengi sana ina kuwa bora kuliko elimu inayotolewa kwenye shule za binafsi kama fedha.

Hii itawasaidia wazazi kupunguza gharama za elimu kwa shule za private kwa kuwa watoto wengi watasoma shule hizo za Serikali kama ilivyokuwa miaka ya 1980 kushuka chini ambapo shule za Serikali kama eru wetu, Jangwani, loleza, kilakala, tabora girls, nganza, zanaki, kibasila, kisutu , tambaza etc zilikuwa zimejaa watoto wenye akili nyingi waliofaulu. Kufaulu darasa la Saba haikuwa rahisi na kwendakusoma shule tajwa Hapo JUU ilikuwa sifa kwa wazazi na watoto.

Zilikuwepo shule za private kama kibosho, mzizima, shaaban Robert etc walikwenda watoto ambao hawakufaulu. Kwa sasa hali imegeuka imekuwa Ni sifa kwa wazazi kusomesha shule bora zenye quality education kama feza, Marian, rosmini, kifungilo, mazinde JUU, st joseph , Msolwa etc. bei ya shule hizi zitapungua tu automatically pale hali ya elimu ya shule za Serikali itakaporudi kama ile ya miaka ya 1980 kurudi nyuma. Kwa sasa chaguo ni la mzazi ni free market economy.

Ukitakakumpeleka mwanao Jangwani ni elimu bure. Ukitaka aende feza shurti utoe fedha.
 
Back
Top Bottom