Prof_Adventure_guide
JF-Expert Member
- Dec 21, 2023
- 519
- 1,463
Katika wakati ambapo wananchi walioamka wanapaza sauti kwa umoja na msimamo thabiti wakisema NO REFORMS NO ELECTION – yaani bila mabadiliko ya kweli ya mfumo wa uchaguzi hakuna sababu ya kushiriki uchaguzi wa maigizo – chama cha ACT-Wazalendo kinakuja na kauli isiyokubalika ya "Linda kura".
Swali la msingi ni hili: unalinda nini kwenye mfumo wa kisiasa uliojengwa juu ya udanganyifu, uonevu, na ukandamizaji wa demokrasia?
Unalinda kura zipi ambazo hata kabla hazijapigwa tayari zimeandaliwa kuibiwa kupitia tume isiyo huru, daftari lililochakachuliwa, na sheria kandamizi zisizotoa haki sawa kwa vyama vyote?
ACT-Wazalendo, kwa kauli zao hizi, wanazidi kujidhihirisha kuwa si chombo cha ukombozi wa kisiasa bali ni "controlled opposition" – chama kidogo kinachoishi kwa makombo ya mfumo wa CCM kwa kisingizio cha realism. Huu ni usaliti wa kisiasa kwa wananchi wanaotafuta mabadiliko ya kweli.
Katika mazingira ambapo uchaguzi ni predetermined, tume ya uchaguzi ni state-captured, na vyombo vya dola ni biased tools of repression, hoja ya "Linda kura" ni kichekesho cha kisiasa kilichojaa political naivety au complicit intent. Ni sawa na mtu anayelinda mzoga ukifikiri bado una uhai.
Wananchi wanaelewa, na historia inashuhudia: hakuna mabadiliko yanayopatikana kwa kulinda udanganyifu. Mabadiliko ya kweli huanzia kwenye kusimama kidete na kudai REFORMS kabla ya chaguzi yoyote kufanyika.
Kwa hiyo tunarudia kwa msisitizo:
NO REFORMS, NO ELECTION.
Sio Linda Kura bali Linda Demokrasia kwanza.
ACT-Wazalendo wasituchanganye na siasa za kulinda maslahi yao ya kisiasa kwa mgongo wa wananchi w
aliodhulumiwa.
Swali la msingi ni hili: unalinda nini kwenye mfumo wa kisiasa uliojengwa juu ya udanganyifu, uonevu, na ukandamizaji wa demokrasia?
Unalinda kura zipi ambazo hata kabla hazijapigwa tayari zimeandaliwa kuibiwa kupitia tume isiyo huru, daftari lililochakachuliwa, na sheria kandamizi zisizotoa haki sawa kwa vyama vyote?
ACT-Wazalendo, kwa kauli zao hizi, wanazidi kujidhihirisha kuwa si chombo cha ukombozi wa kisiasa bali ni "controlled opposition" – chama kidogo kinachoishi kwa makombo ya mfumo wa CCM kwa kisingizio cha realism. Huu ni usaliti wa kisiasa kwa wananchi wanaotafuta mabadiliko ya kweli.
Katika mazingira ambapo uchaguzi ni predetermined, tume ya uchaguzi ni state-captured, na vyombo vya dola ni biased tools of repression, hoja ya "Linda kura" ni kichekesho cha kisiasa kilichojaa political naivety au complicit intent. Ni sawa na mtu anayelinda mzoga ukifikiri bado una uhai.
Wananchi wanaelewa, na historia inashuhudia: hakuna mabadiliko yanayopatikana kwa kulinda udanganyifu. Mabadiliko ya kweli huanzia kwenye kusimama kidete na kudai REFORMS kabla ya chaguzi yoyote kufanyika.
Kwa hiyo tunarudia kwa msisitizo:
NO REFORMS, NO ELECTION.
Sio Linda Kura bali Linda Demokrasia kwanza.
ACT-Wazalendo wasituchanganye na siasa za kulinda maslahi yao ya kisiasa kwa mgongo wa wananchi w
aliodhulumiwa.