ACT na kushindwa kwa Kafulila

ACT na kushindwa kwa Kafulila

Dotto C. Rangimoto

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2012
Posts
1,985
Reaction score
1,286
ACT NA KUSHINDWA KWA KAFULILA.

kfuli.jpg

Kumekuwa na uvumi katika mitandao ya kijamii kuwa chama chetu cha ACT kimehusika katika kushindwa kwa David kafulila. Wengine wanaenda mbali zaidi kwa kumhusisha Zitto Z Kabwe katika hili.

Kama chama hakiwezi kujibu kila tuhuma, sababu kama kikianza kujitia kazi kujibu hakitaweza kufanya kazi zake, sababu watu hawaishi kusema na kila siku huibuka jipya.

Hata hivyo, hili mimi binafsi naomba kulijibu, na nina lijibu kama mwanachama tu wa ACT ambaye huona tabu chama chake kuzushiwa mambo yaso kweli na yenye lengo la kukitoa chama katika reli na kukiingiza katika majibizano.

Mosi.
Kama kuweka mgombea katika jimbo la Kigoma Kusini na kufanya siasa katika jimbo hilo ndio kunachukuliwa kuwa ni uhusika wetu katika kushindwa kwa Kafulila, hili linakuwa si sahihi hata kidogo.

Kama chama cha siasa tusingependa chama chochote kishinde Kigoma Kusini tafauti na ACT, na ndio maana tulipeleka chama, tukafanya siasa, tukaweka mgombea na tukafanya kampeni, na kampeni zetu nchi nzima zilijikita katika masuala ya wananchi na taifa lao. Hatukajaribu hata kidogo kujadili mambo kinyume na hivyo.

Kila chama kilikuwa na haki hii katika jimbo lile lakini pia kilikuwa na wajibu huu kwa wanachama wake! Huu huwezi kuuita mpango makhususi wa kumuangusha Kafulila bali ni mpango makhususi wa kushinda jimbo, na kila chama na kila mgombea alikuwa na mpango huu, hata Kafulila alikuwa na mpango huu, na katu hatuwezi kuuita ni hujuma kwetu.

Pili.
Kutochaguliwa tena Kafulila hakujasabishwa na ACT bali kumesababishwa na uhusiano uso ridhisha kati ya Kafulila na wapiga kura wake. Kweli kabisa Kafulila atabaki kuwa mbunge wa kukumbukwa na kwa vyovyote vile pengo lake litaonekana katika bunge hili jipya. Uhusiano wa Kafulila na wapiga kura wake haukuwa mzuri kutokana na sababu zifuatazo.

1. Kafulila amekuwa mbunge wa kitaifa zaidi kuliko kuwa mbunge wa Kigoma Kusini, amejitahidi sana kulisemea taifa juu ufisadi na mambo mengine ya kitaifa.

Wakati akifanya hivyo, jimbo lake lina changamoto nyingi, na wapiga kura walikuwa wanamuhitaji mbunge wao lakini yeye alikuwa na anashughulishwa zaidi na escrow na mambo ya kufananayo. Barabara za jimbo lake ni tatizo, ameshindwa kupambana kushinikiza miradi ya kimaendeleo ifanyike katika jimbo lake kwa wingi.

Wapiga kura walikuwa wanalalamika huku wakitoa mifano jinsi Zitto alivyopambana kuhakikisha Kigoma inaunganishwa na mikoa mingine, hususani ushiriki wake katika ujengwaji wa daraja la Kikwete, daraja ambalo halijafungua fursa kwa Kigoma Kaskazini tu lakini pia kwa Kigoma nzima hata Zitto aonekane mbunge wa Kigoma.

Wakati wakulima na wajasiria mali wa Kigoma Kaskazini wakinufaika na huduma ya hifadhi ya jamii, Kigoma Kusini hicho kitu hakina nguvu na wala hakisisitizwi kama kilivyosisitizwa na Zitto Kigoma Kaskazini.

2. Kitendo cha Kafulila kwenda kumnadi Lowassa Kigoma, mtu ambaye wanaKigoma bado wanamtazama kwa jicho la ufisad pia kumesababisha Kafulila kupotea kama alivyopotea Wenje. Walimuona Kafulila mnafiki na asiyesimamia anacho kiamini, huwezi kumnadi mtu uliyemtukana kwa miaka mitano katika majukwaa ya siasa kwa kusema afaa kuwa rais na bado wenye akili zao wakuelewe.

Naomba mjue, Lowassa baadhi ya mikoa au majimbo alikuwa turufu ya ushindi, lakini katika mikoa na majimbo alikuwa galasa lisilo na madhara mbele ya turufu. Mkoa wa Kigoma na Mwanza ni miongoni mwa mikoa ambayo Lowassa alikuwa galasa lisilo na madhara! Kafulila alikosea sana kwa kumnadi Lowassa na kumshambulia Zitto.

Huwezi kumshambulia Zitto Kigoma kisha wanaKigoma wakuache, mtu ambaye wanamtazama kama alama ya kufunguka Kigoma. Kafulila alimshambulia Zitto jukwaani na katika mitandao ya kijamii lakini pia akampamba Lowassa katika majukwaa, wanaKigoma wakaamua kumkata. Hili sio kosa la ACT bali ni la Kafulila mwenyewe!

3. Kama kuna ugomvi basi si ACT na Kafulila bali wanaKigoma na Kafulila. Kafulila aliwatukana wanaKigoma kuwa wao wanachojua ni kulima mawese na si kuanzisha chama, na hawahitaji chama cha siasa. Sababu kwanini walipoikubali CHADEMA au NCCR hawakuambiwa kuwa si watu kuanzisha chama? Ina maana kwao ni kosa kuikubali ACT? Kwanini chama wanachokikubali Kafulia akiite cha Kigoma ikiwa vyama vyote huwa vya kitaifa? Maswali haya majibu yake yalikuwa ni matusi kwa wanaKIGOMA.

Haya yalionekana ni matusi kwa wanaKigoma kiasi wamzomee akiwa jukwaani. Maneno yale aliyasema Kigoma mjini, lakini yalisambaa haraka Tanzania nzima, na wanaKigoma wakaonesha machungu yao kupitia sanduku la kura.

Hili haliwezi kuwa kosa la ACT, na wanaKigoma na baadhi ya watanzania wanaofurahia kushindwa kwa Kafulila hakuwez kuwa kosa pia la ACT, ingawa pia ni kweli wengi wa wanao shangilia kushindwa kwa Kafulila ni wanaKIGOMA na pia wanaKIGOMA hawa wana vyama vyao, na wapo baadhi ni ACT.

3. Chama kilichopambana kwa kufa na kupona kuhakikisha Kafulila harudi bungeni ni CCM, na kilitumia ofisi ya Wilaya na ya mkurugenzi katika kufanikisha hili, ACT hatukushiriki katika hili na kama chama hatuwezi kufurahia uvunjifu wa sheria katika zoezi la uchaguzi. Kweli pia Kigoma Kusini kulikuwa na viashiria vya wizi wa kura, lakini ni ajabu mtu akianza kuishutumu ACT juu ya hili.

Hata hivyo, kama Kafulila angemzidi wa CCM kwa kura zaidi ya eflu ishirini kwa mfano, hata CCM wangeiba vip wasingeweza kuziba utafauti huo wa kura. Kafulila kapata ushindi mwembamba mno kama alivyoshinda Wenje kwa ushindi huo mwembamba. Ushindi wa kuzidi kura 100 kunatoa mwanya kwa CCM kupiga goli la mkono.

Kama Kafulila angekuwa na adabu kwa wapiga kura na kwa wakigoma wenzake, asingepata ushindi mwembamba, hili ni funzo kubwa sana kwa wabunge walioshinda sasa. Mkichaguliwa kuwa wabunge msiote pembe, cheo dhamana tu!

Nakutakia maisha mema ya kulima mawese.

Njano5
0784845394/762845394
 
Saafi huyu mbili2 naamini yupo humu jamvini na huu ujumbe utakua umemfikia
 
ACT NA KUSHINDWA KWA KAFULILA.

attachment.php


Kumekuwa na uvumi katika mitandao ya kijamii kuwa chama chetu cha ACT kimehusika katika kushindwa kwa David kafulila. Wengine wanaenda mbali zaidi kwa kumhusisha Zitto Z Kabwe katika hili.

Kama chama hakiwezi kujibu kila tuhuma, sababu kama kikianza kujitia kazi kujibu hakitaweza kufanya kazi zake, sababu watu hawaishi kusema na kila siku huibuka jipya.

Hata hivyo, hili mimi binafsi naomba kulijibu, na nina lijibu kama mwanachama tu wa ACT ambaye huona tabu chama chake kuzushiwa mambo yaso kweli na yenye lengo la kukitoa chama katika reli na kukiingiza katika majibizano.

Mosi.
Kama kuweka mgombea katika jimbo la Kigoma Kusini na kufanya siasa katika jimbo hilo ndio kunachukuliwa kuwa ni uhusika wetu katika kushindwa kwa Kafulila, hili linakuwa si sahihi hata kidogo.

Kama chama cha siasa tusingependa chama chochote kishinde Kigoma Kusini tafauti na ACT, na ndio maana tulipeleka chama, tukafanya siasa, tukaweka mgombea na tukafanya kampeni, na kampeni zetu nchi nzima zilijikita katika masuala ya wananchi na taifa lao. Hatukajaribu hata kidogo kujadili mambo kinyume na hivyo.

Kila chama kilikuwa na haki hii katika jimbo lile lakini pia kilikuwa na wajibu huu kwa wanachama wake! Huu huwezi kuuita mpango makhususi wa kumuangusha Kafulila bali ni mpango makhususi wa kushinda jimbo, na kila chama na kila mgombea alikuwa na mpango huu, hata Kafulila alikuwa na mpango huu, na katu hatuwezi kuuita ni hujuma kwetu.

Pili.
Kutochaguliwa tena Kafulila hakujasabishwa na ACT bali kumesababishwa na uhusiano uso ridhisha kati ya Kafulila na wapiga kura wake. Kweli kabisa Kafulila atabaki kuwa mbunge wa kukumbukwa na kwa vyovyote vile pengo lake litaonekana katika bunge hili jipya. Uhusiano wa Kafulila na wapiga kura wake haukuwa mzuri kutokana na sababu zifuatazo.

1. Kafulila amekuwa mbunge wa kitaifa zaidi kuliko kuwa mbunge wa Kigoma Kusini, amejitahidi sana kulisemea taifa juu ufisadi na mambo mengine ya kitaifa.

Wakati akifanya hivyo, jimbo lake lina changamoto nyingi, na wapiga kura walikuwa wanamuhitaji mbunge wao lakini yeye alikuwa na anashughulishwa zaidi na escrow na mambo ya kufananayo. Barabara za jimbo lake ni tatizo, ameshindwa kupambana kushinikiza miradi ya kimaendeleo ifanyike katika jimbo lake kwa wingi.

Wapiga kura walikuwa wanalalamika huku wakitoa mifano jinsi Zitto alivyopambana kuhakikisha Kigoma inaunganishwa na mikoa mingine, hususani ushiriki wake katika ujengwaji wa daraja la Kikwete, daraja ambalo halijafungua fursa kwa Kigoma Kaskazini tu lakini pia kwa Kigoma nzima hata Zitto aonekane mbunge wa Kigoma.

Wakati wakulima na wajasiria mali wa Kigoma Kaskazini wakinufaika na huduma ya hifadhi ya jamii, Kigoma Kusini hicho kitu hakina nguvu na wala hakisisitizwi kama kilivyosisitizwa na Zitto Kigoma Kaskazini.

2. Kitendo cha Kafulila kwenda kumnadi Lowassa Kigoma, mtu ambaye wanaKigoma bado wanamtazama kwa jicho la ufisad pia kumesababisha Kafulila kupotea kama alivyopotea Wenje. Walimuona Kafulila mnafiki na asiyesimamia anacho kiamini, huwezi kumnadi mtu uliyemtukana kwa miaka mitano katika majukwaa ya siasa kwa kusema afaa kuwa rais na bado wenye akili zao wakuelewe.

Naomba mjue, Lowassa baadhi ya mikoa au majimbo alikuwa turufu ya ushindi, lakini katika mikoa na majimbo alikuwa galasa lisilo na madhara mbele ya turufu. Mkoa wa Kigoma na Mwanza ni miongoni mwa mikoa ambayo Lowassa alikuwa galasa lisilo na madhara! Kafulila alikosea sana kwa kumnadi Lowassa na kumshambulia Zitto.

Huwezi kumshambulia Zitto Kigoma kisha wanaKigoma wakuache, mtu ambaye wanamtazama kama alama ya kufunguka Kigoma. Kafulila alimshambulia Zitto jukwaani na katika mitandao ya kijamii lakini pia akampamba Lowassa katika majukwaa, wanaKigoma wakaamua kumkata. Hili sio kosa la ACT bali ni la Kafulila mwenyewe!

3. Kama kuna ugomvi basi si ACT na Kafulila bali wanaKigoma na Kafulila. Kafulila aliwatukana wanaKigoma kuwa wao wanachojua ni kulima mawese na si kuanzisha chama, na hawahitaji chama cha siasa. Sababu kwanini walipoikubali CHADEMA au NCCR hawakuambiwa kuwa si watu kuanzisha chama? Ina maana kwao ni kosa kuikubali ACT? Kwanini chama wanachokikubali Kafulia akiite cha Kigoma ikiwa vyama vyote huwa vya kitaifa? Maswali haya majibu yake yalikuwa ni matusi kwa wanaKIGOMA.

Haya yalionekana ni matusi kwa wanaKigoma kiasi wamzomee akiwa jukwaani. Maneno yale aliyasema Kigoma mjini, lakini yalisambaa haraka Tanzania nzima, na wanaKigoma wakaonesha machungu yao kupitia sanduku la kura.

Hili haliwezi kuwa kosa la ACT, na wanaKigoma na baadhi ya watanzania wanaofurahia kushindwa kwa Kafulila hakuwez kuwa kosa pia la ACT, ingawa pia ni kweli wengi wa wanao shangilia kushindwa kwa Kafulila ni wanaKIGOMA na pia wanaKIGOMA hawa wana vyama vyao, na wapo baadhi ni ACT.

3. Chama kilichopambana kwa kufa na kupona kuhakikisha Kafulila harudi bungeni ni CCM, na kilitumia ofisi ya Wilaya na ya mkurugenzi katika kufanikisha hili, ACT hatukushiriki katika hili na kama chama hatuwezi kufurahia uvunjifu wa sheria katika zoezi la uchaguzi. Kweli pia Kigoma Kusini kulikuwa na viashiria vya wizi wa kura, lakini ni ajabu mtu akianza kuishutumu ACT juu ya hili.

Hata hivyo, kama Kafulila angemzidi wa CCM kwa kura zaidi ya eflu ishirini kwa mfano, hata CCM wangeiba vip wasingeweza kuziba utafauti huo wa kura. Kafulila kapata ushindi mwembamba mno kama alivyoshinda Wenje kwa ushindi huo mwembamba. Ushindi wa kuzidi kura 100 kunatoa mwanya kwa CCM kupiga gili la mkono.

Kama Kafulila angekuwa na adabu kwa wapiga kura na kwa wakigoma wenzake, asingepata ushindi mwembamba, hili ni funzo kubwa sana kwa wabunge walioshinda sasa. Mkichaguliwa kuwa wabunge msiote pembe, cheo dhamana tu!

Nakutakia maisha mema ya kulima mawese.

Njano5
0784845394/762845394

Hiki chama kinakufa hata asilimia moja hamjapata wagombea ubunge nchi nzima ameshinda mmoja kina mwigamba siwatakufa njaa bila ruzuku
 
Kafulila hakufanya uchambuzi wa kina wa athari za kumbeba lowassa na kumtukana zitto na kuwashambulia waha wote.
Lakibi miye sishangai pesa bwana hizo kalamba hela za lowassa sasa kakuona cha mtema kuni
 
Jamani, uchaguzi umeisha. Washindi wameishapatikana, wapeni ushirikiano wafanye kazi kulliko kundelea kujeruhi taifa kwa kuendeleza mipasho na utengano.
 
Hiki chama kinakufa hata asilimia moja hamjapata wagombea ubunge nchi nzima ameshinda mmoja kina mwigamba siwatakufa njaa bila ruzuku

chama kina mwaka mmoja tu, ni ujinga ukianza kutusakama kwa matokeo ya uchaguzi huu, uchaguz wa kwanza kwetu. kwa miaka ishirini mmeshindwa kuingia ikulu, tena hadi kwa msaada toka kwa fisad lowassa.
 
Kuna majimbo yalikuwa targeted ili wabunge wake wasiurudi tena bungeni kwa sababu mbali mbali. hili nalo lilikuwa ni moja wapo. Pole sana Kafulila ila Mwenyezi Mungu muweza wa yote atakulipia tu, kwani malipo huwa ni hapa hapa duniani.

Aluta .....
 
Hiki chama kinakufa hata asilimia moja hamjapata wagombea ubunge nchi nzima ameshinda mmoja kina mwigamba siwatakufa njaa bila ruzuku

heko kaka chama chao hicho hakina muda tutakiona chali.
kiongozi mwenyewe zitto
 
NCCR wameshinda wangapi mkuu?

Huyo msaliti mkuu alikuwa na mbwembwe nyingi kuwa kigoma yote itaenda kwa wasaliti. Alisambaza pich nchi nzima kuonyesha ana influence matokeo tumeyaona wasaliti wamchemsha vibaya sana. Kafulila kashinda wamembania tu. Afande sele kura 1200 hata mgombe udiwani amemshinda mchange kura 3000 tu. Ni ukweli kuwa 2010 CDM ilimbeba sana.
 
zit msaliti sana hii dhambi itamsuta kafuta upinxani kigoma
 
Msaliti Mkuu alijidai ana wafuasi wengi vijana mbona chama kipo kama chauma tu pamoja na kuwa na msaliti mkuu hata ije miaka 10 mbele wasaliti hawawezi kufinga mbali watakuwa wamesambaratika au kuungana na magamba tu.
 
Hiki chama kinakufa hata asilimia moja hamjapata wagombea ubunge nchi nzima ameshinda mmoja kina mwigamba siwatakufa njaa bila ruzuku

Unahangaika na ACT chama kichanga kabisaa! Teh teh teh niambie Chaggadema mmepata wabunge wangapi maana uchaguzi wa mwaka huu pamoja na kubebwa na mafisadi mmeangukia pua! Ni lazima Dr. Slaa apigiwe makoti!
 
Kama taifa tumepoteza mtu muhimu sana. Wanakigoma hawajatutendea haki. Mnamuadhibu mtu muhimu namna hiyo wakati maslahi ya taifa ni maslahi ya kigoma pia? Ubinafsi, ubinafsi, ubinafsi wa wanakigoma!!!!


 
Mbona huko huko kigoma Ukawa wamebeba jimbo namadiwani pia msaliti mkuu kashindwa kuzuia ushindi wa Ukawa na kuupeleka kwa wasaliti. maana wasaliti mnafurahi kafulila kuporwa ushindi wake.
 
ACT nani asie jua kwamba ni branch la ccm ata uongee mpaka povu likutoke hata hela ya kampeni mmepigwa tafu na ccm
 
marumbano ya kijinga ambayo hayajawahi kutokea kwa wapinzani miaka 20, huu ni ubwete kubeza mtu aliyeshindwa, mbona ccm wameshindwa kibao hamuwasemi? CHADEMA imemsaidia JPM kuondoa mawaziri mzigo.
 
ACT NA KUSHINDWA KWA KAFULILA.

View attachment 303514

Kumekuwa na uvumi katika mitandao ya kijamii kuwa chama chetu cha ACT kimehusika katika kushindwa kwa David kafulila. Wengine wanaenda mbali zaidi kwa kumhusisha Zitto Z Kabwe katika hili.

Kama chama hakiwezi kujibu kila tuhuma, sababu kama kikianza kujitia kazi kujibu hakitaweza kufanya kazi zake, sababu watu hawaishi kusema na kila siku huibuka jipya.

Hata hivyo, hili mimi binafsi naomba kulijibu, na nina lijibu kama mwanachama tu wa ACT ambaye huona tabu chama chake kuzushiwa mambo yaso kweli na yenye lengo la kukitoa chama katika reli na kukiingiza katika majibizano.

Mosi.
Kama kuweka mgombea katika jimbo la Kigoma Kusini na kufanya siasa katika jimbo hilo ndio kunachukuliwa kuwa ni uhusika wetu katika kushindwa kwa Kafulila, hili linakuwa si sahihi hata kidogo.

Kama chama cha siasa tusingependa chama chochote kishinde Kigoma Kusini tafauti na ACT, na ndio maana tulipeleka chama, tukafanya siasa, tukaweka mgombea na tukafanya kampeni, na kampeni zetu nchi nzima zilijikita katika masuala ya wananchi na taifa lao. Hatukajaribu hata kidogo kujadili mambo kinyume na hivyo.

Kila chama kilikuwa na haki hii katika jimbo lile lakini pia kilikuwa na wajibu huu kwa wanachama wake! Huu huwezi kuuita mpango makhususi wa kumuangusha Kafulila bali ni mpango makhususi wa kushinda jimbo, na kila chama na kila mgombea alikuwa na mpango huu, hata Kafulila alikuwa na mpango huu, na katu hatuwezi kuuita ni hujuma kwetu.

Pili.
Kutochaguliwa tena Kafulila hakujasabishwa na ACT bali kumesababishwa na uhusiano uso ridhisha kati ya Kafulila na wapiga kura wake. Kweli kabisa Kafulila atabaki kuwa mbunge wa kukumbukwa na kwa vyovyote vile pengo lake litaonekana katika bunge hili jipya. Uhusiano wa Kafulila na wapiga kura wake haukuwa mzuri kutokana na sababu zifuatazo.

1. Kafulila amekuwa mbunge wa kitaifa zaidi kuliko kuwa mbunge wa Kigoma Kusini, amejitahidi sana kulisemea taifa juu ufisadi na mambo mengine ya kitaifa.

Wakati akifanya hivyo, jimbo lake lina changamoto nyingi, na wapiga kura walikuwa wanamuhitaji mbunge wao lakini yeye alikuwa na anashughulishwa zaidi na escrow na mambo ya kufananayo. Barabara za jimbo lake ni tatizo, ameshindwa kupambana kushinikiza miradi ya kimaendeleo ifanyike katika jimbo lake kwa wingi.

Wapiga kura walikuwa wanalalamika huku wakitoa mifano jinsi Zitto alivyopambana kuhakikisha Kigoma inaunganishwa na mikoa mingine, hususani ushiriki wake katika ujengwaji wa daraja la Kikwete, daraja ambalo halijafungua fursa kwa Kigoma Kaskazini tu lakini pia kwa Kigoma nzima hata Zitto aonekane mbunge wa Kigoma.

Wakati wakulima na wajasiria mali wa Kigoma Kaskazini wakinufaika na huduma ya hifadhi ya jamii, Kigoma Kusini hicho kitu hakina nguvu na wala hakisisitizwi kama kilivyosisitizwa na Zitto Kigoma Kaskazini.

2. Kitendo cha Kafulila kwenda kumnadi Lowassa Kigoma, mtu ambaye wanaKigoma bado wanamtazama kwa jicho la ufisad pia kumesababisha Kafulila kupotea kama alivyopotea Wenje. Walimuona Kafulila mnafiki na asiyesimamia anacho kiamini, huwezi kumnadi mtu uliyemtukana kwa miaka mitano katika majukwaa ya siasa kwa kusema afaa kuwa rais na bado wenye akili zao wakuelewe.

Naomba mjue, Lowassa baadhi ya mikoa au majimbo alikuwa turufu ya ushindi, lakini katika mikoa na majimbo alikuwa galasa lisilo na madhara mbele ya turufu. Mkoa wa Kigoma na Mwanza ni miongoni mwa mikoa ambayo Lowassa alikuwa galasa lisilo na madhara! Kafulila alikosea sana kwa kumnadi Lowassa na kumshambulia Zitto.

Huwezi kumshambulia Zitto Kigoma kisha wanaKigoma wakuache, mtu ambaye wanamtazama kama alama ya kufunguka Kigoma. Kafulila alimshambulia Zitto jukwaani na katika mitandao ya kijamii lakini pia akampamba Lowassa katika majukwaa, wanaKigoma wakaamua kumkata. Hili sio kosa la ACT bali ni la Kafulila mwenyewe!

3. Kama kuna ugomvi basi si ACT na Kafulila bali wanaKigoma na Kafulila. Kafulila aliwatukana wanaKigoma kuwa wao wanachojua ni kulima mawese na si kuanzisha chama, na hawahitaji chama cha siasa. Sababu kwanini walipoikubali CHADEMA au NCCR hawakuambiwa kuwa si watu kuanzisha chama? Ina maana kwao ni kosa kuikubali ACT? Kwanini chama wanachokikubali Kafulia akiite cha Kigoma ikiwa vyama vyote huwa vya kitaifa? Maswali haya majibu yake yalikuwa ni matusi kwa wanaKIGOMA.

Haya yalionekana ni matusi kwa wanaKigoma kiasi wamzomee akiwa jukwaani. Maneno yale aliyasema Kigoma mjini, lakini yalisambaa haraka Tanzania nzima, na wanaKigoma wakaonesha machungu yao kupitia sanduku la kura.

Hili haliwezi kuwa kosa la ACT, na wanaKigoma na baadhi ya watanzania wanaofurahia kushindwa kwa Kafulila hakuwez kuwa kosa pia la ACT, ingawa pia ni kweli wengi wa wanao shangilia kushindwa kwa Kafulila ni wanaKIGOMA na pia wanaKIGOMA hawa wana vyama vyao, na wapo baadhi ni ACT.

3. Chama kilichopambana kwa kufa na kupona kuhakikisha Kafulila harudi bungeni ni CCM, na kilitumia ofisi ya Wilaya na ya mkurugenzi katika kufanikisha hili, ACT hatukushiriki katika hili na kama chama hatuwezi kufurahia uvunjifu wa sheria katika zoezi la uchaguzi. Kweli pia Kigoma Kusini kulikuwa na viashiria vya wizi wa kura, lakini ni ajabu mtu akianza kuishutumu ACT juu ya hili.

Hata hivyo, kama Kafulila angemzidi wa CCM kwa kura zaidi ya eflu ishirini kwa mfano, hata CCM wangeiba vip wasingeweza kuziba utafauti huo wa kura. Kafulila kapata ushindi mwembamba mno kama alivyoshinda Wenje kwa ushindi huo mwembamba. Ushindi wa kuzidi kura 100 kunatoa mwanya kwa CCM kupiga goli la mkono.

Kama Kafulila angekuwa na adabu kwa wapiga kura na kwa wakigoma wenzake, asingepata ushindi mwembamba, hili ni funzo kubwa sana kwa wabunge walioshinda sasa. Mkichaguliwa kuwa wabunge msiote pembe, cheo dhamana tu!

Nakutakia maisha mema ya kulima mawese.

Njano5
0784845394/762845394

....siioni pointi ya maana uliyoandika hapa zaidi ya kujaza propaganda za kipuuzi...
Kuwa Kafulila alikua mbunge wa kitaifa zaidi hakufanya chochote jimboni kwake;nyie na huyo baba yenu mlifanya nini kigoma kaskazini?
Umejaa unafiki mwingi,unajidai kuwasemea wana kigoma hayo mamlaka umepewa na nani?
Mpuuzi wewe unahalalisha wizi wa kura sababu eti kafulila hakumzidi mpinzani wake kwa kura zaidi ya elfu ishirini..!!?!!
Hakika nimeamini; Act ni chama cha kinafiki,kilichojaa wanafiki,kinachoongozwa kwa misingi ya kinafiki.
Kafulila nenda mahakamani kadai haki yako,wachana na hawa marafiki wa ccm, wanaojidai ni chama cha kigoma wakati wenyewe wameambulia mbunge mmoja tu, tena rafiki wa ccm.!!
#vivakafulila!
#nevergiveup!!
 
Kama taifa tumepoteza mtu muhimu sana. Wanakigoma hawajatutendea haki. Mnamuadhibu mtu muhimu namna hiyo wakati maslahi ya taifa ni maslahi ya kigoma pia? Ubinafsi, ubinafsi, ubinafsi wa wanakigoma!!!!



Uchaguzi wa mwaka 2020 mchukueni aje kugombea Moshi. Watu wa Kigoma tuacheni na ubinafsi wetu tumeshaamua Kafulila chaliii!!
 
Back
Top Bottom