Juzi juzi tu kuna dada mmoja jirani yangu ameteleza kwenye ngazi na kujigonga vibaya sehemu za kisogoni wakati akijaribu kuwakimbia marafiki zake waliokua na ndoo ya maukoko na maji machafu wakimkimbiza ili wammwagie. Mdada alichanika sehemu ya nyuma ya kichwa na ilibidi majirani tuingilie kati kumkimbiza hospitali ambapo alishonwa nyuzi kadhaa huku wale waliokua wanamkimbiza wakiishia kutoa tu mimacho kama mataahira bila kumpa msaada wowote.