Acheni Mara Moja Tabia Hii Wanawake & Wanaume

Acheni Mara Moja Tabia Hii Wanawake & Wanaume

Kinkunti El Perdedo

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2020
Posts
5,505
Reaction score
13,776
Wanawake

Sifa kuu ya mwanamke ni usafi ndio maana kuna ule msemo maarufu wa "mwanamke usafi" na ni ukweli ulio wazi mwanamke msafi hupendwa na kila mtu lakini kwanini uonekane msafi wa mwili tu lakini vitu vinavyo kustili kuwa katika usafi hauvithamini baada ya kuvitumia?

Hivi mwanamke unaye jiona msomi, mrembo, smart nk, una anza vipi kutupa "taulo ya kike(pedi)" kwenye mazingira ya wazi ya umma baada ya kuitumia? Hivi hujihisi aibu kuweka sehemu ya utu wako wa ndani naya Siri public?

Limekuwa jambo la kawaida kuona pedi zimetupwa hovyo mitaani jambo hili linatia kinyaa na aibu sio siri,hivi ina maana huwezi choma pedi baada ya kutumia? Mbona ch*pi zenu zilizo isha hatuzioni mitaa Kama pedi zenu?

Mama zetu wa zamani licha ya mazingira magumu ya wakati huo walijitahidi sana kulinda heshima zao mbele ya jamii hasa kulinda maungo yao ya ndani,walikuwa wanatumia vitambaa kujistili lakini ulikuwa huwezi kuta kitaa hicho kimetupwa mitaani hovyo Kama mnavyo fanya nyie mnajiona mlio elimika kuliko wao ila ni ukweli ulio wazi kwamba walikuwa smart kuliko nyie wa digitali.

Ewe Mama uliye ndani humu muelimishe binti yako aliye vunja ungo asitupe pedi hovyo baada ya kutumia badala yake achome moto Kama mnavyo choma ch*pi zenu zikichoka."TABIA YA KUTUPA PEDI HOVYO IKOMEE KABISA."

Mwanaume

Hivi mwanaume uliye kamilika na unaye jiamini na wengine mkiwa baba wa familia una anza vipi kukujoa kwenye kopo na kutupa kopo hilo nje huku likiwa limejaa mkojo wako?

Na kwa utafiti wangu usio rasmi dana tabia hii ya kukojoa kwenye makopo inafanywa sana na watu wenye magari maana makopo mengi yenye mikojo utayakuta pembezoni mwa barabara, jambo hili linatia kinyaa na fedhea kwa wanaume wote kuonekana wasio jitambua kwa tabia za wachache.

Kumbuka Kuna watu wanakusanya hayo makopo Kama sehemu ya ajira yao ili kujipatia ridhiki ya siku,na Kuna wengine wanatumia makopo hayo hayo kuuzia maziwa ya mtindi pembezoni mwa barabara.Hivyo unaweza kuta kopo ambalo uliweka mkojo wako wa pombe ndo hilo hilo unakuja kulinunua likiwa na maziwa ndani. TABIA HII IKOME
 
Tabia ni kama ngozi ya mwili na kamwe haibadiliki haijalishi kiwango chako cha elimu, Kabila wala Dini.
 
Tabia ni kama ngozi ya mwili na kamwe haibadiliki haijalishi kiwango chako cha elimu, Kabila wala Dini.
Kwa kulitambua hilo ndio maana wanadamu walijenga magereza kwa ajili ya kuwa shape watu kitabia na hatuwezi kaa kimya sababu tu tabia ni Kama ngozi mkuu hapana
 
Mkuu naona unawapangia watu namna ya kutoa taka mwili zao.

Ungeweka picha ya hizo pedi au kopo za mkojo ungesaidia kwa tusiofahamu
 
Mkuu naona unawapangia watu namna ya kutoa taka mwili zao.

Ungeweka picha ya hizo pedi au kopo za mkojo ungesaidia kwa tusiofahamu
Mkuu hili nalo sema mbona lipo Sana na lipo wazi sijampangia mtu namna ya kutoa taka mwili nacho pinga mimi ni namna ya uhifadhi usio rasmi wa hizo taka mwili
 
Janga lingine la uchafuzi wa mazingira ni ma pampers ya watoto, yamekua janga kuu kama mifuko ya plastic, yamezagaa hovyo hovyo, yanaziba mitaro nk, wahusika waliangalie hilo
 
Na kwa utafiti wangu usio rasmi Sana tabia hii ya kukojoa kwenye makopo inafanywa Sana na watu wenye magari maana makopo mengi yenye mikojo utayakuta pembezoni mwa barabara,jambo hili linatia kinyaa na fedhea kwa wanaume wote kuonekana wasio jitambua kwa tabia za wachache.
Imenikumbusha miaka kadhaa Ubungo Bus Terminal, kuna chupa za mikojo zilikuwa zinatupwa hovyohovyo usiku, siku moja alfajiri bus likakanyaga chupa yenye mikojo ikapasuka na kurushia abiria mikojo, kwa kile kishindo nahisi wengine walimwagikiwa midomoni maana ilikuwa giza kila mmoja alikimbilia anakojua yeye, ikawa kila bus linapogeuza abiria wanakimbia kama vile wanakimbia kukamatwa na polisi
 
Janga lingine la uchafuzi wa mazingira ni ma pampers ya watoto, yamekua janga kuu kama mifuko ya plastic, yamezagaa hovyo hovyo, yanaziba mitaro nk, wahusika waliangalie hilo
Wanalijua sana ila wakilianzisha tu, wamegusa ndevu za simba usalama wa vibarua vyao hatarini
 
Imenikumbusha miaka kadhaa Ubungo Bus Terminal, kuna chupa za mikojo zilikuwa zinatupwa hovyohovyo usiku, siku moja alfajiri bus likakanyaga chupa yenye mikojo ikapasuka na kurushia abiria mikojo, kwa kile kishindo nahisi wengine walimwagikiwa midomoni maana ilikuwa giza kila mmoja alikimbilia anakojua yeye, ikawa kila bus linapogeuza abiria wanakimbia kama vile wanakimbia kukamatwa na polisi
mkuu umenifanya nicheke vibaya Sana
 
Janga lingine la uchafuzi wa mazingira ni ma pampers ya watoto, yamekua janga kuu kama mifuko ya plastic, yamezagaa hovyo hovyo, yanaziba mitaro nk, wahusika waliangalie hilo
Asante mkuu pia Kuna maeneo ya shughuli za kijamii hayana vyoo kabisa
 
Wanawake

Sifa kuu ya mwanamke ni usafi ndio maana kuna ule msemo maarufu wa "mwanamke usafi" na ni ukweli ulio wazi mwanamke msafi hupendwa na kila mtu lakini kwanini uonekane msafi wa mwili tu lakini vitu vinavyo kustili kuwa katika usafi hauvithamini baada ya kuvitumia ?

Hivi mwanamke unaye jiona msomi,mrembo,smart nk,una anza vipi kutupa "taulo ya kike(pedi)" kwenye mazingira ya wazi ya umma baada ya kuitumia? Hivi hujihisi aibu kuweka sehemu ya utu wako wa ndani naya Siri public?

Limekuwa jambo la kawaida kuona pedi zimetupwa hovyo mitaani jambo hili linatia kinyaa na aibu sio siri,hivi ina maana huwezi choma pedi baada ya kutumia? Mbona ch*pi zenu zilizo isha hatuzioni mitaa Kama pedi zenu?

Mama zetu wa zamani licha ya mazingira magumu ya wakati huo walijitahidi Sana kulinda heshima zao mbele ya jamii hasa kulinda maungo yao ya ndani,walikuwa wanatumia vitambaa kujistili lakini ulikuwa huwezi kuta kitaa hicho kimetupwa mitaani hovyo Kama mnavyo fanya nyie mnajiona mlio elimika kuliko wao ila ni ukweli ulio wazi kwamba walikuwa smart kuliko nyie wa digitali.

Ewe Mama uliye ndani humu muelimishe binti yako aliye vunja ungo asitupe pedi hovyo baada ya kutumia badala yake achome moto Kama mnavyo choma ch*pi zenu zikichoka."TABIA YA KUTUPA PEDI HOVYO IKOMEE KABISA"

Mwanaume

Hivi mwanaume uliye kamilika na unaye jiamini na wengine mkiwa baba wa familia una anza vipi kukujoa kwenye kopo ? na kutupa kopo hilo nje uku likiwa limejaa mkojo wako?

Na kwa utafiti wangu usio rasmi Sana tabia hii ya kukojoa kwenye makopo inafanywa Sana na watu wenye magari maana makopo mengi yenye mikojo utayakuta pembezoni mwa barabara,jambo hili linatia kinyaa na fedhea kwa wanaume wote kuonekana wasio jitambua kwa tabia za wachache.

Kumbuka Kuna watu wanakusanya hayo makopo Kama sehemu ya ajira yao ili kujipatia ridhiki ya siku,na Kuna wengine wanatumia makopo hayo hayo kuuzia maziwa ya mtindi pembezoni mwa barabara.Hivyo unaweza kuta kopo ambalo uliweka mkojo wako wa pombe ndo hilo hilo unakuja kulinunua likiwa na maziwa ndani.TABIA HII IKOME
Tumeshaliongea sana hili hapa JamiiForums na Binafsi nilishaanzisha 'Threads' Mbili za Kulikemea hili ambalo huwa linanipa mno Kinyaa na sijui kwanini huwa nina bahati mbaya ya Kukutana nalo hasa Mitaa ya Uswahilini ambayo nimebobea nayo 24/7.

Asante na Kongole nawe pia kwa Kulisemea hili kwa mara nyingine huenda likapata Msukumo zaidi na Wahusika ( Wanawake ) kubadilika kwani kwa 100% linawadhalilisha na Kudhoofisha zaidi Utu wao kama Jeshi muhimu Ulimwenguni.
 
Kwenye foleni kali wanaume wakibanwa huwa wanajisaidia
Kwenye chupa za maji,na wakimaliza
Wanarusha nje

Ova
 
Tumeshaliongea sana hili hapa JamiiForums na Binafsi nilishaanzisha Threads Mbili za Kulikemea hili ambalo huwa linanipa mno Kinyaa na sijui kwanini huwa nina bahati mbaya ya Kukutana nalo hasa Mitaa ya Uswahilini ambayo nimebobea nayo 24/7.
Ni kukosa akili mkuu yaani dunia ya Sasa ambapo watu wanajiona walio elimika wanafanya ujinga kuliko hata watu walio ishi karne ya Socrates
 
Janga lingine la uchafuzi wa mazingira ni ma pampers ya watoto, yamekua janga kuu kama mifuko ya plastic, yamezagaa hovyo hovyo, yanaziba mitaro nk, wahusika waliangalie hilo
Alafu kunguru anabeba ndomana utakuta kwako kuna pampers

Ustaarabu zero

Ova
 
Imenikumbusha miaka kadhaa Ubungo Bus Terminal, kuna chupa za mikojo zilikuwa zinatupwa hovyohovyo usiku, siku moja alfajiri bus likakanyaga chupa yenye mikojo ikapasuka na kurushia abiria mikojo, kwa kile kishindo nahisi wengine walimwagikiwa midomoni maana ilikuwa giza kila mmoja alikimbilia anakojua yeye, ikawa kila bus linapogeuza abiria wanakimbia kama vile wanakimbia kukamatwa na polisi
 
Back
Top Bottom