Acha wafunge mipaka tutakutana tena

prucho

Member
Jul 22, 2016
39
94
USIOGOPE SHIKILIA HAPO HAPO.

Na, Mwl. Pasaka O. Rucho.

Aliyewahi kuwa Rais wa Marekani aliwahi kusema "the only thing we have to fear is fear itself" kwa lugha yetu jambo pekee tunalopaswa kuliogopa ni uoga wenyewe.

Kuna sintofahamu kati yetu Tanzania na ndugu zetu wa jumuiya ya Afrika Mashariki haswa kwa upande wa Kenya, ambako siku ya jana tarehe 16/05/2020 akilihutubia taifa Rais wa Kenya alisema ameufunga mpaka wake na Tanzania pamoja na Somalia kwa siku 30 kama njia ya kupambana na Corona.

Sitaki kuzungumzia sana mpaka wao na Somalia ila nataka nizungumzie mpaka wetu na Kenya, naomba niwakumbushe majirani zangu wa Kenya, Corona ilianzia China siyo Tanzania, wasitake kututendea kama wa China sisi bado ni ndugu zao.

Zoezi la kufunga mpaka na kuendelea kutaka kuitenga Tanzania ni miongoni mwa dhambi za usaliti ambazo zinaendelezwa ndani ya jumuiya ya Afrika Mashariki.

Kwa wale wafuatiliaji wa habari 12/05/2020 aliyekuwa waziri wa mambo ya nje akihojiwa na DW alisema diplomasia yetu na dunia imeshuka sana kwa awamu hii imeshuka sana na nchi majirani zitaendelea kutufungia mipaka.

Mh.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania JPM, the only thing to fear is fear itself, hawa watu hawajaanza kututenga leo achana na upupu wa Membe, kwani mwaka 2013, mahusiano yetu na nchi hizo ulikuwa mzuri?, Membe alikuwa hatembei? Mbona mahusiano yaliharibika?

Mwalimu Nyerere aliwahi kusema mtu akizoea kula nyama ya mtu hawezi acha, majirani zetu wamezoea kututenga hawawezi acha hata kidogo.

Akilihutubia bunge Rais mstaafu Kikwete 2013 baada ya majirani zetu hawa kututenga kwa sababu kuwa.
.Tanzania imekuwa kikwazo kwa maendeleo ya jumuiya
.Tanzania haina moyo wala dhamira ya dhati ya kuendeleza jumuiya.

Rais kikwete alisema "licha ya kuwa tunatengwa lakini sisi Tanzania hatupuuzi maazimio ya jumuiya ila yapo mengine yanakwaza" akaenda mbali na kusema kuwa "hakutukanaye hakuchagulii tusi " mwisho akamalizia kwa kusema "kinachotupa taabu ni msimamo wetu".

Tatizo hili la 2013,limejirudia tena 2020 kwa nchi hizo Marais wa nchi hizo bado ni wale wale sisi tulishabadilisha Rais, lakini usaliti wao umebaki pale pale.

Kinachotupa taabu ni msimamo wetu, majirani zetu wanataka tuwekwe lockdown kama maembe?
Tuwekwe lockdown kama mbuzi, ngombe na udagaa?

MH.JPM, wasikutishe sisi ungetuweka lockdown tungekufa wengi sana kwa mawazo na njaa, unawaona wanavyoteseka, kipindi nchi zingine zinafungua lockdown na mipaka wenyewe ndipo wanatufungia hapana usiwaze mh. Rais tuko kwenye mstari sahihi.

Mh.Rais Ulisema ugonjwa huu tunaweza kuishi nao kama surua na ukimwi, na WHO wakaufyataaa, sikiliza shikilia hapo hapo si mara ya kwanza kututenga hata mwl.Nyerere walimchokoza akawatandika.

Mh.Rais nashukuru mpaka wetu hujafunga,ila wao wamefunga mtu akifunga chumba chake acha afunge ila najua atafungua tuuu, usiogope kamatia hapo hapo.

Mwisho nitoe rai kwa Watanzania wenzangu tuungane na Mh.Rais katika mapambano haya tufanye kazi kwa bidii, tumwombe mwenyezi Mungu ambaye ndo tegemeo letu, na tusiogope kufungiwa mipaka, ipo siku wakijua thamani yetu watafungua.

0756231744.
 
Uganda, kenya na Rwanda wamekutanishwa na unafiki wana mabifu yao ya kufa

Baada ya miezi mitatu watarudi kuomba ushirikiano tena
 
Your economy will never recover you yellow squirrel.
 
Naona umeandika pambio tu.
Anyway wanafunga kwa ajili yao wenyewe.. si kwa ajili ya tanzania.
Wanafanya maamuzi wao kama wao. Not otherwise.
Hizo nchi ni huru na zina maamuzi yake.
Wana sheria zao na maamuzi yao.
 
Acha wafunge maana haieleweki corona imeisha Tanganyika au tunaugulia nyumbani kwa kunywa tangawizi na limao
 
Nzige wametaga mayai mengi sana kenya, ni jeshi la maangamizi kwa kijani chenu mnachojivunia.

Msijesema sikuwaonya kabla.
 
Wacha ujinga
Nani anajibembeleza kwa Wakenya
Waache Wafunge
Na majibu Utayaona
Ni Raia wa upande gani wata lalamikia hilo
 
Chukueni tahadhari acheni kulia lia, mbona mumefungiwa kote SADC na EAC ila kwa Kenya ndio mnalia na kung'aka sana.
Hao Watanzania wote tuliowagundua na corona walikua wanang'ang'ania kuja kutuambukiza.
Nyie ambukizaneni huko maana mumedhihirisha hamthamini afya za walalahoi wenu, mnawaacha watu wasongamane kwenye vilabu vya pombe hamtaki kufunga chochote, mumeangukia pua kwenye hili la corona full kujichokea na kukata tamaa.
Msituletee balaa lenu kisa undugu, sisi tunajitambua na tuko makini sana, bora uchumi ushuke kwa kipindi hiki kidogo lakini tubaki salama, tusiendeshwe na umaskini kama mnavyofanya huko.
 
Chukueni tahadhari acheni kulia lia, mbona mumefungiwa kote SADC na EAC ila kwa Kenya ndio mnalia na kung'aka sana.
Hao Watanzania wote tuliowagundua na corona walikua wanang'ang'ania kuja kutuambukiza.
Nyie ambukizaneni huko maana mumedhihirisha hamthamini afya za walalahoi wenu, mnawaacha watu wasongamane kwenye vilabu vya pombe hamtaki kufunga chochote, mumeangukia pua kwenye hili la corona full kujichokea na kukata tamaa.
Msituletee balaa lenu kisa undugu, sisi tunajitambua na tuko makini sana, bora uchumi ushuke kwa kipindi hiki kidogo lakini tubaki salama, tusiendeshwe na umaskini kama mnavyofanya huko.
Wewe bwege kweli

Kenyata amewafanya mabwege na nyie mnakubali!

Lockdown gani ya kihuni mnaifanya saa 11 jioni wakati jua tayari limeshazama?

Rais wenu anajikomba kwa mabeberu ili mwakani wasimpeleke tena The Hague kama wanavyofanyaga

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chukueni tahadhari acheni kulia lia, mbona mumefungiwa kote SADC na EAC ila kwa Kenya ndio mnalia na kung'aka sana.
Hao Watanzania wote tuliowagundua na corona walikua wanang'ang'ania kuja kutuambukiza.
Nyie ambukizaneni huko maana mumedhihirisha hamthamini afya za walalahoi wenu, mnawaacha watu wasongamane kwenye vilabu vya pombe hamtaki kufunga chochote, mumeangukia pua kwenye hili la corona full kujichokea na kukata tamaa.
Msituletee balaa lenu kisa undugu, sisi tunajitambua na tuko makini sana, bora uchumi ushuke kwa kipindi hiki kidogo lakini tubaki salama, tusiendeshwe na umaskini kama mnavyofanya huko.
Haya endeleeni kufunga mipaka tuu,huku hakuna cha lockdown wala mama yake Lockdown tunaendelea kupiga kazi kama kawaida huku tukichukua tahadhari kama raisi wetu mpendwa alivyotushauri.Si mtaufungua huo mpaka tuu au mtaendelea kukaa ndani ndegele
 
Back
Top Bottom