Acha shule fanya biashara

Bullshit

JF-Expert Member
Nov 30, 2016
1,300
1,495
Huu ni ushauri kutoka kwa rafiki yangu.

Hello JamiiForums,

Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 26. Nimeajiriwa na vilevile nina biashara yangu binafsi, lakini nina ndoto za kurudi shule ambayo inaweza kunichukua miaka saba hivi.

Nimepata pingamizi kutoka kwa rafiki wangu wa karibu akidai kuwa haoni kama nina uhitaji wa elimu.

Aliendelea kwa kusema kwamba ulimwengu wa sasa elimu iko mikononi mwako ni wewe sasa kuitumia maana watu wengi wanasoma ili waajiriwe na haoni sababu ya mimi kufanya hivyo, na pia nina mwanzo mzuri wa maisha naweza kutumia akili yangu kupanunua na kukuza biashara yangu.

Muda utakaopoteza shule ni muda wa wewe kuitwa millionea.

Aliniambia nifanyie tathmini miaka saba ya shule na miaka saba ya kufanya biashara. Alimaliza kwa kuniambia kwamba yeye binafsi alijutia sana muda alioupoteza chuo kikuu na elimu ya chuo haikumsaidia kitu, kilichomsaidia kufikia mafanikio yake ni akili yake binafsi, juhudi zake binafisi na kujiamini. Laiti asingeenda chuo miaka minne (4) pale chuo, ilitosha yeye kufanya kitu cha kumpa maandeleo.

Mwana JamiiForums, na wewe unaweza kutoa mtazamo wako.

Asante na karibu!
 
Mtu unatakiwa usome katika kiwango anagalao cha degree moja ndipo uanze michakato ya biashara kama unaona unakipaji nayo maana biashara ni kipaji pia; sio kila mtu anaweza kufanya biashara.

Kiwango cha wastani wa degree kitakusaidi kufanya biashara kitaalamu zaidi pia kitakusaidi kuweza kuwasiliana na taasisi za kifedha kwa urahisi zaidi ili kuinua biashara yako au kupata wadau bora wa kukuza biashara yako.

Kwa mfano, utakuwa na uelewa wa kutosha na kuweza kufanya biashara za hisa au hatifungate bila shida yoyote.

Usije ukaishia darasa la saba au elimu ya sekondari halafu ukakataa kupata elimu ya juu.

Anangalau uwe na degree yoyote Ile.
 
Alimaliza kwa kuniambia kwamba yeye binafsi alijutia sana muda alioupoteza chuo kikuu na elimu ya chuo haikumsaidia kitu,

Huyo hakujiwekeza toka mwanzo. Kusoma ni uwekezaji. You invest in yourself. Kabla ya kuanza kusoma inabidi ujue unajiwekeza kwenye nini ili mwisho wa siku uwe nani au ufanye nini. Ukishapata jibu ndiyo unaanza kusoma ili ufikie lengo. Mfano, nataka kuanzisha dispensary mbeleni, naanza kusoma kwa nguvu masomo ya sayansi ili niende chuo kikuu kusomea udaktari. Nikimaliza nasaka mtaji wa kuanzisha dispensary; napanga nyumba naanza ka-dispensary kangu kadogo.

Mtu kama mimi siwezi kujutia kuwa elimu niliyopata hainisaidii au nilipoteza muda kusoma. Wanaosoma bora liende ndio wenye mitizamo kama huyo.
 
Kama umeishia darasa la saba tu, nakushauri utafute muda ukasome. Ila kama umeishia form 4, huko mbele hakuna jipya sana litakalokusaidia kwenye kile unachokifanya. Mimi nilimaliza chuo nimeajiriwa kampuni mbili, ila elimu niliyokuwa na apply kazini ni ya form 4 tu, ukiacha zile training ambazo hata mhitimu wa form 4 mwenye kichwa kizuri angezielewa.

Nimejiajiri na bado sija-apply elimu yangu ya form 6 au chuo, japo inaniwezesha kulewa mambo mengi kwenye habari na matukio ya kila siku duniani, tofauti na ningeishia form 4.
 
Huyo hakujiekewa toka mwanzo
Kusoma Ni uwekezaji.You invest in yourself.Kabla ya kuanza kusoma inabidi ujue unakljiwekeza kwenye Nini ili mwisho wa siku uwe Nani au ufanye Nini.Ukishapa jibu ndio unaanza kusoma ili ufikie lengo.Mfano nataka kuanzisha dispensary mbeleni .Naanza kusoma kwa nguvu masomo ya sayansi ili niende chuo kikuu kusomea udaktari.Nikimaliza nasaka mtaji wa kuanzisha dispensary .Napanga nyumba naanza kadispensary kangu kadogo

Mtu Kama Mimi siwezi jutia kuwa elimu nilisoma hainisaidii au nilipoteza muda kusoma.Wanaosoma Bora liende ndio wenye mitizamo Kama huyo.
Hahaaa! We jamaa bana, kuwapa wenzako haya maushauri ni rahisi sana, ila nadhani hujawahi kuwa na ndugu aliyesotea ajira.
 
Umri wa mtu kuanza biashara kubwa ni miaka 24, na ndiyo umri wa wengi kumaliza digrii.

Ushauri wangu wakati mtu anaendelea kukua, awe masomoni hadi hiyo miaka 24, baada ya hapo ruksa aingie kwenye biashara.

Anakuwa na ufahamu mkubwa na umri. Pia, mkubwa wa kumwezesha kufanya mambo yake.
 
Hahaaa, we jamaa bana kuwapa wenzako haya maushauri ni rahisi sana, ila nadhani hujawahi kuwa na ndugu aliyesotea ajira

Wahindi, Waarabu na Wapemba, ulishasikia wanalilia ajira? Watoto wao husoma madigrii kwa ajili ya kuendesha biashara zao. Hao akina Mohamed Dewji wana digrii kibao. Mtu mfano anasoma Digrii ya Kilimo, nyumbani kuna eneo kubwa la shamba akirudi analala anaamka anasibiri ajira.

Mtu anasomea ualimu ili mwisho wa siku iwe nini? Unakuta kamaliza kakaa tu hawezi fungua hata shule ya chekechea chumba cha kupanga. Unakuta wasio na digrii za ualimu ndiyo wenye shule za chekechea mitaani na wanapata pesa hasa. Msomi wa digrii ya ualimu yupo yupo tu anasubiri ajira ya ualimu wa sekondari, chekechea hawezi!
 
Mtu unatakiwa usome katika kiwango anagalao cha degree moja ndipo uanze michakato ya biashara Kama unaona unakipaji nayo, maana biashara Ni kipaji pia, sio kila mtu anaweza kufanya biashara.
Kiwango cha wastani wa degree kitakusaidi kufanya biashara kitaalamu zaidi pia kitakusaidi kuweza kuwasiliana na taasisi za kifedha kwa urahisi zaidi ili kuinua biashara yako au kupata wadau bora wa kukuza biashara yako.
Kwa mfano Utakuwa na uelewa wa kutosha na kuweza kufanya biashara za hisa au hatifungate bila shida yoyote.
Usije ukaishia darasa la Saba au Elimu ya Sekondari halafu ukakataa kupata Elimu ya juu.
Anangalao uwe na degree yoyote Ile.
Good Hint!
 
Wahindi ,waarabu ,wapemba ulishasikia wanalilia ajira? Watoto wao husoma madigrii kwa ajili ya kuendesha biashara zao.Hao Akina Mohamed dewji Wana digrii kibao .Mtu mfano anasoma digrii ya kilimo nyumbani Kuna eneo kubwa la shamba akirudi analala anaamka anasibiri ajira!!!

Mtu anasomea ualimu ili mwisho wa siku.iwe Nini? Unakuta kamaliza kakaa tu hawezi fungua hata Shule ya chekechea chumba Cha kupanga.Unakuta wasio na digrii za ualimu ndio wenye Shule za chekechea mitaani na wanapata pesa hasa.Msomi wa digrii ya ualimu.yupo yupo tu anasubiri ajira ya ualimu wa secondary chekechea hawezi!!!!!

Unajua India ni moja kati ya nchi ambazo zina tatizo kubwa sana la ajira duniani? So usifikiri Watanzania wanaolalamika kukosa ajira ni wajinga sana. Hawa Wahindi unaowaona hapa Tz ni wachache ambao familia zao zilishajijenga tangia mwanzo, hivyo watoto wao hawana shida na ajira.

Sasa unategemea Watanzania wote wawe kama akina Mo Dewji?
 
Unajua India ni moja kati ya nchi ambazo zina tatizo kubwa sana la ajira duniani? So usifikiri Watanzania wanaolalamika kukosa ajira ni wajinga sana,
Hawa wahindi unaowaona hapa Tz ni wachache ambao familia zao zilishajijenga tangia mwanzo, hivyo watoto wao hawana shida na ajira
Sasa unategemea watanzania wote wawe kama akina Mo Dewji?
Vizuri sana madam watanzania bana wanaangalia wahindi wa kariakoo ndio wanafikiri india nzima wahindi wapo hivyo.
 
Wahindi ,waarabu ,wapemba ulishasikia wanalilia ajira? Watoto wao husoma madigrii kwa ajili ya kuendesha biashara zao.Hao Akina Mohamed dewji Wana digrii kibao .Mtu mfano anasoma digrii ya kilimo nyumbani Kuna eneo kubwa la shamba akirudi analala anaamka anasibiri ajira!!!

Mtu anasomea ualimu ili mwisho wa siku.iwe Nini? Unakuta kamaliza kakaa tu hawezi fungua hata Shule ya chekechea chumba Cha kupanga.Unakuta wasio na digrii za ualimu ndio wenye Shule za chekechea mitaani na wanapata pesa hasa.Msomi wa digrii ya ualimu.yupo yupo tu anasubiri ajira ya ualimu wa secondary chekechea hawezi!!!!!
Kujiweka ndani ya box nikusoma ili uje kujiajiri kwenye ulichosomea. Mjasiriamali aliye timamu hajiungi kwenye hilo box simple ili uwe millionea unayekuwa uwe na vyanzo nya mapato visivyopungua saba. Je, kwa box hilo ulojifunga siutakufa maskini tu? Wakina Mengi wamewekeza kwenye niche kibao, Bakhresa, Mo n.k wamewekeza sehemu kibao.

Mimi nimesomea uwalimu ila nimejiajiri kwenye entertainment industry na hapa sijapata mtaji wa maana nitafanya usafiri, chakula, viwanda n.k. kulazimisha kujiajiri kwenye ulichosomea huna tofauti na aliyeajiriwa wote mupo ndani ya box.
 
Mimi nimesomea uwalimu ila nimejiajiri kwenye Entertainment industry nahapa sijapata mtaji wamaana nitafanya usafiri, chakula, viwanda nk...kulazimisha kujiajiri kwenye ulichosomea huna tofauti na aliyeajiriwa wote muko ndani ya Box.

Umepoteza pesa zako bure kusoma huko kwingine hujasomea unafanya kibabaishaji tu. Waganda na Wakenya wakisomea ualimu kama wewe wanaungana, mfano, wewe umesomea ualimu wa masomo ya sayansi unaungana na waliosomea masomo ya arts munatafuta majengo ya kupangisha mnafungua shule wamiliki ninyi wenyewe na walimu ninyi wenyewe.

Mwalimi kwenda kuwa DJ ni misallocation of resources. Elimu kazi yake kunoa talent yako kwenye eneo husika. Sasa wewe na u-DJ, si unababaisha tu huko?

Mengi alianza kama mhasibu akajenga capital huko ndio akaanza kuanzisha biashara zingine kwa kutumia wataalanu waliosomea maeneo husika.

Kwa mwalimu kuanza na entertainment business ni kuanza maisha kwa mguu wa kushoto. Ungekuwa ulisomea ualimu wa muziki nikupongeza kuwa uko sahihi, lakini kama umesomea mengine na unaanza biashara ya ku-burn CD na kuingiza nyimbo kwenye simu za watu hapo hapajakaa vizuri.
 
Umepoteza pesa zako bure kusoma huko kwingine hujasomea unafanya kibabaishaji tu.Waganda na Wakenya wakisomea ualimu Kama wewe wanaungana mfano wewe umrsomea ualimu wa masomo ya sayansi unaungana na waliosomea masomo ya Arts mnatafuta majengo ya kupangisha mnafingua Shule wamiliki ninyi wenyewe na walimu ninyi wenyewe
Mwalimi kwenda kuwa DJ Ni mis allocation of resources.Elimu Kazi yake kunoa talent yako kwenye eneo husika .Sasa wewe na u DJ si unababaisha tu huko.
Mengi alianza Kama mhasibu akajenga capital huko ndio akaanza kuanzisha biashara zingine kwa kutumia wataalanu waliosomea maeneo husika.
Kwa mwalimu kuanza na entertainment business Ni kuanza maisha kwa mguu wa kushoto.Ungekuwa ulisomea ualimu wa muziki nikupongeza kuwa uko sahihi.Lakini Kama umesomea mengine.na unaanza biashara ya KU burn CD na kuingiza nyimbo kwenye simu za watu hapo hapajakaa vizuri
life has no limits mkuu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom